< 4 Mose 33 >

1 Das sind die Reisen der Kinder Israel, die aus Ägyptenland gezogen sind nach ihrem Heer durch Mose und Aaron.
Hivi ndivyo vituo katika safari ya Waisraeli walipotoka Misri kwa vikosi chini ya uongozi wa Mose na Aroni.
2 Und Mose beschrieb ihren Auszug, wie sie zogen, nach dem Befehl des HERRN, und sind nämlich dies die Reisen ihres Zugs.
Kwa agizo la Bwana, Mose aliweka kumbukumbu ya vituo katika safari yao. Hivi ndivyo vituo katika safari yao:
3 Sie zogen aus von Raemses am fünfzehnten Tage des ersten Monden, des andern Tages der Ostern, durch eine hohe Hand, daß alle Ägypter sahen,
Waisraeli walisafiri kutoka Ramesesi katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza, siku iliyofuata Pasaka. Walitembea kwa ujasiri wazi mbele ya Wamisri wote,
4 und begruben eben die Erstgeburt, die der HERR unter ihnen geschlagen hatte; denn der HERR hatte auch an ihren Göttern Gerichte geübt.
waliokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza wote, ambao Bwana alikuwa amewaua katikati yao, kwa kuwa Bwana alikuwa ameleta hukumu juu ya miungu yao.
5 Als sie von Raemses auszogen, lagerten sie sich in Suchoth.
Waisraeli waliondoka Ramesesi na kupiga kambi huko Sukothi.
6 Und zogen aus von Suchoth und lagerten in Etham, welches liegt an dem Ende der Wüste.
Wakaondoka Sukothi na kupiga kambi huko Ethamu, pembeni mwa jangwa.
7 Von Etham zogen sie aus und blieben im Grunde Hiroth, welches liegt gegen Baal-Zephon, und lagerten sich gegen Migdol.
Wakaondoka Ethamu, wakageuka wakarudi Pi-Hahirothi, hadi mashariki ya Baal-Sefoni, wakapiga kambi yao karibu na Migdoli.
8 Von Hiroth zogen sie aus und gingen mitten durchs Meer in die Wüste; und reiseten drei Tagereisen in der Wüste Etham und lagerten sich in Mara.
Wakaondoka Pi-Hahirothi wakapita katikati ya bahari mpaka jangwani, na baada ya kusafiri kwa siku tatu katika Jangwa la Ethamu, walipiga kambi huko Mara.
9 Von Mara zogen sie aus und kamen gen Elim, darin waren zwölf Wasserbrunnen und siebenzig Palmen; und lagerten sich daselbst.
Wakaondoka Mara wakaenda Elimu, mahali ambapo palikuwa na chemchemi kumi na mbili na mitende sabini, huko wakapiga kambi.
10 Von Elim zogen sie aus und lagerten sich an das Schilfmeer.
Wakaondoka Elimu na kupiga kambi kando ya Bahari ya Shamu.
11 Von dem Schilfmeer zogen sie aus und lagerten sich in der Wüste Sin.
Wakaondoka kando ya Bahari ya Shamu na kupiga kambi katika Jangwa la Sini.
12 Von der Wüste Sin zogen sie aus und lagerten sich in Daphka.
Wakaondoka katika Jangwa la Sini, wakapiga kambi huko Dofka.
13 Von Daphka zogen sie aus und lagerten sich in Alus.
Wakaondoka Dofka, wakapiga kambi huko Alushi.
14 Von Alus zogen sie aus und lagerten sich in Raphidim; daselbst hatte das Volk kein Wasser zu trinken.
Wakaondoka Alushi, wakapiga kambi Refidimu, mahali ambapo hapakuwa na maji kwa ajili ya watu kunywa.
15 Von Raphidim zogen sie aus und lagerten sich in der Wüste Sinai.
Wakaondoka Refidimu na kupiga kambi katika Jangwa la Sinai.
16 Von Sinai zogen sie aus und lagerten sich in die Lustgräber.
Wakaondoka katika Jangwa la Sinai na kupiga kambi huko Kibroth-Hataava.
17 Von den Lustgräbern zogen sie aus und lagerten sich in Hazeroth.
Wakaondoka Kibroth-Hataava na kupiga kambi huko Haserothi.
18 Von Hazeroth zogen sie aus und lagerten sich in Rithma.
Wakaondoka Haserothi na kupiga kambi huko Rithma.
19 Von Rithma zogen sie aus und lagerten sich in Rimon-Parez.
Wakaondoka Rithma na kupiga kambi huko Rimon-Peresi.
20 Von Rimon-Parez zogen sie aus und lagerten sich in Libna.
Wakaondoka Rimon-Peresi na kupiga kambi huko Libna.
21 Von Libna zogen sie aus und lagerten sich in Rissa.
Wakaondoka Libna na kupiga kambi huko Risa.
22 Von Rissa zogen sie aus und lagerten sich in Kehelatha.
Wakaondoka Risa na kupiga kambi huko Kehelatha.
23 Von Kehelatha zogen sie aus und lagerten sich im Gebirge Sapher.
Wakaondoka Kehelatha na kupiga kambi kwenye mlima Sheferi.
24 Vom Gebirge Sapher zogen sie aus und lagerten sich in Harada.
Wakaondoka kwenye mlima Sheferi na kupiga kambi huko Harada.
25 Von Harada zogen sie aus und lagerten sich in Makeheloth.
Wakaondoka Harada na kupiga kambi huko Makelothi.
26 Von Makeheloth zogen sie aus und lagerten sich in Thahath.
Wakaondoka Makelothi na kupiga kambi huko Tahathi.
27 Von Thahath zogen sie aus und lagerten sich in Tharah.
Wakaondoka Tahathi na kupiga kambi huko Tera.
28 Von Tharah zogen sie aus und lagerten sich in Mithka.
Wakaondoka Tera na kupiga kambi huko Mithka.
29 Von Mithka zogen sie aus und lagerten sich in Hasmona.
Wakaondoka Mithka na kupiga kambi huko Hashmona.
30 Von Hasmona zogen sie aus und lagerten sich in Moseroth.
Wakaondoka Hashmona na kupiga kambi Moserothi.
31 Von Moseroth zogen sie aus und lagerten sich in Bne-Jakan.
Wakaondoka Moserothi na kupiga kambi huko Bene-Yakani.
32 Von Bne-Jakan zogen sie aus und lagerten sich in Horgidgad.
Wakaondoka Bene-Yakani na kupiga kambi huko Hor-Hagidgadi.
33 Von Horgidgad zogen sie aus und lagerten sich in Jathbatha.
Wakaondoka Hor-Hagidgadi na kupiga kambi huko Yotbatha.
34 Von Jathbatha zogen sie aus und lagerten sich in Abrona.
Wakaondoka Yotbatha na kupiga kambi huko Abrona.
35 Von Abrona zogen sie aus und lagerten sich in Ezeon-Gaber.
Wakaondoka Abrona na kupiga kambi huko Esion-Geberi.
36 Von Ezeon-Gaber zogen sie aus und lagerten sich in der Wüste Zin, das ist Kades.
Wakaondoka Esion-Geberi na kupiga kambi huko Kadeshi katika Jangwa la Sini.
37 Von Kades zogen sie aus und lagerten sich an dem Berge Hor, an der Grenze des Landes Edom.
Wakaondoka Kadeshi na kupiga kambi kwenye Mlima Hori, mpakani mwa Edomu.
38 Da ging der Priester Aaron auf den Berg Hor nach dem Befehl des HERRN und starb daselbst im vierzigsten Jahr des Auszugs der Kinder Israel aus Ägyptenland, am ersten Tage des fünften Monden,
Kwa amri ya Bwana, kuhani Aroni alipanda Mlima Hori, mahali alipofia katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano, mwaka wa arobaini baada ya Waisraeli kutoka Misri.
39 da er hundert und dreiundzwanzig Jahre alt war.
Aroni alikufa juu ya Mlima Hori akiwa na umri wa miaka 123.
40 Und Arad der König der Kanaaniter, der da wohnete gegen Mittag des Landes Kanaan, hörete, daß die Kinder Israel kamen.
Mfalme Mkanaani wa Aradi, ambaye aliishi huko Negebu ya Kanaani, akasikia kwamba Waisraeli wanakuja.
41 Und von dem Berge Horzogen sie aus und lagerten sich in Zalmona.
Wakaondoka kwenye mlima Hori na kupiga kambi huko Salmona.
42 Von Zalmona zogen sie aus und lagerten sich in Phunon.
Wakaondoka Salmona, wakapiga kambi huko Punoni.
43 Von Phunon zogen sie aus und lagerten sich in Oboth.
Wakaondoka Punoni, wakapiga kambi huko Obothi.
44 Von Oboth zogen sie aus und lagerten sich in Jgim, am Gebirge Abarim in der Moabiter Grenze.
Wakaondoka Obothi, wakapiga kambi huko Iye-Abarimu, mipakani mwa Moabu.
45 Von Jgim zogen sie aus und lagerten sich in Dibon-Gad.
Wakaondoka Iye-Abarimu, wakapiga kambi huko Dibon-Gadi.
46 Von Dibon-Gad zogen sie aus und lagerten sich in Almon-Diblathaim.
Wakaondoka Dibon-Gadi na kupiga kambi huko Almon-Diblathaimu.
47 Von Almon-Diblathaim zogen sie aus und lagerten sich in dem Gebirge Abarim gegen Nebo.
Wakaondoka Almon-Diblathaimu na kupiga kambi katika milima ya Abarimu, karibu na Nebo.
48 Von dem Gebirge Abarim zogen sie aus und lagerten sich in das Gefilde der Moabiter an dem Jordan gegen Jericho.
Wakaondoka kwenye milima ya Abarimu na kupiga kambi kwenye tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
49 Sie lagerten sich aber am Jordan von Beth-Jesimoth bis an die Breite Sittim, des Gefildes der Moabiter.
Huko kwenye tambarare za Moabu walipiga kambi kandokando ya Mto Yordani, kuanzia Beth-Yeshimothi mpaka Abel-Shitimu.
50 Und der HERR redete mit Mose in dem Gefilde der Moabiter an dem Jordan gegen Jericho und sprach:
Katika tambarare za Moabu kando ya Yordani kuvukia Yeriko, Bwana akamwambia Mose,
51 Rede mit den Kindern Israel und sprich zu ihnen: Wenn ihr über den Jordan gegangen seid in das Land Kanaan
“Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapovuka Mto Yordani kuingia Kanaani,
52 so sollt ihr alle Einwohner vertreiben vor eurem Angesicht und alle ihre Säulen und alle ihre gegossenen Bilder umbringen und alle ihre Höhen vertilgen,
wafukuzeni wakazi wote wa nchi iliyo mbele yenu. Haribuni sanamu zao zote za kuchongwa, na sanamu zilizotengenezwa kwa kuyeyusha chuma, na kupabomoa mahali pao pa ibada.
53 daß ihr also das Land einnehmet und drinnen wohnet; denn euch habe ich das Land gegeben, daß ihr's einnehmet.
Mtaimiliki nchi hiyo na kukaa huko, kwa kuwa nimewapeni ninyi kuimiliki.
54 Und sollt das Land austeilen durchs Los unter eure Geschlechter. Denen, deren viel ist, sollt ihr desto mehr zuteilen, und denen, deren wenig ist, sollt ihr desto weniger zuteilen. Wie das Los einem jeglichen daselbst fällt, so soll er's haben, nach den Stämmen ihrer Väter.
Mtaigawanya nchi hiyo kwa kupiga kura, kufuatana na koo zenu. Kwa kundi kubwa zaidi toa urithi mkubwa zaidi, na kwa kundi dogo zaidi urithi mdogo zaidi. Chochote kinachowaangukia kwa kura kitakuwa chao. Mtaigawanya nchi kufuatana na makabila ya babu zenu.
55 Werdet ihr aber die Einwohner des Landes nicht vertreiben vor eurem Angesicht, so werden euch die, so ihr überbleiben lasset, zu Dornen werden in euren Augen und zu Stacheln in euren Seiten und werden euch drängen auf dem Lande, da ihr innen wohnet.
“‘Lakini kama hamkuwafukuza wenyeji wakaao katika nchi hiyo, wale mtakaowaruhusu wabaki watakuwa kama sindano kwenye macho yenu na miiba kwenu kila upande. Watawasumbua katika nchi mtakayoishi.
56 So wird's denn gehen, daß ich euch gleich tun werde, was ich gedachte ihnen zu tun.
Kisha nitawatenda ninyi kile ambacho nimepanga kuwatenda wao.’”

< 4 Mose 33 >