< 1 Mose 10 >

1 Dies ist das Geschlecht der Kinder Noahs: Sem, Ham, Japheth. Und sie zeugeten Kinder nach der Sintflut.
Hawa ndio wazao wa Noa: Shemu, Hamu na Yafethi, ambao walizaa wana baada ya gharika.
2 Die Kinder Japheths sind diese: Gomer, Magog, Madai, Javan, Thubal, Mesech und Thiras.
Wana wa Yafethi walikuwa: Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Mesheki na Tirasi.
3 Aber die Kinder von Gomer sind diese: Askenas, Riphath und Thogarma.
Wana wa Gomeri walikuwa: Ashkenazi, Rifathi na Togarma.
4 Die Kinder von Javan sind diese: Elisa, Tharsis, Kittim und Dodanim.
Wana wa Yavani walikuwa: Elisha, Tarshishi, Kitimu na Rodanimu.
5 Von diesen sind ausgebreitet die Inseln der Heiden in ihren Ländern, jegliche nach ihrer Sprache, Geschlecht und Leuten.
(Kutokana na hawa mataifa ya Pwani yalienea katika nchi zao, kwa koo zao katika mataifa yao, kila moja kwa lugha yake.)
6 Die Kinder von Ham sind diese: Chus, Mizraim, Put und Kanaan.
Wana wa Hamu walikuwa: Kushi, Misraimu, Putu na Kanaani.
7 Aber die Kinder von Chus sind diese. Seba, Hevila, Sabtha, Raema und Sabtecha. Aber die Kinder von Raema sind diese: Scheba und Dedan.
Wana wa Kushi walikuwa: Seba, Havila, Sabta, Raama na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa: Sheba na Dedani.
8 Chus aber zeugete den Nimrod. Der fing an ein gewaltiger HERR zu sein auf Erden,
Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikua akawa mtu shujaa duniani.
9 und war ein gewaltiger Jäger vor dem HERRN. Daher spricht man: Das ist ein gewaltiger Jäger vor dem HERRN, wie Nimrod.
Alikuwa mwindaji hodari mbele za Bwana. Ndiyo sababu watu husema, “Kama Nimrodi, hodari wa kuwinda mbele za Bwana.”
10 Und der Anfang seines Reichs war Babel, Erech, Ackad und Kalne im Lande Sinear.
Vituo vyake vya kwanza katika ufalme wake vilikuwa Babeli, Ereki, Akadi na Kalne katika Shinari.
11 Von dem Land ist danach kommen der Assur und bauete Ninive und Rehoboth-Ir und Kalah,
Kutoka nchi ile alikwenda Ashuru, ambako alijenga Ninawi, Rehoboth-iri, Kala,
12 dazu Resen zwischen Ninive und Kalah. Dies ist eine große Stadt.
na Reseni, iliyo kati ya Ninawi na Kala; huo ndio mji mkubwa.
13 Mizraim zeugete Ludim, Anamim, Leabim, Naphthuhim,
Misraimu alikuwa baba wa: Waludi, Waanami, Walehabi, Wanaftuhi,
14 Pathrusim und Kasluhim. Von dannen sind kommen die Philistim und Kaphthorim.
Wapathrusi, Wakasluhi (hao ndio asili ya Wafilisti), na Wakaftori.
15 Kanaan aber zeugete Zidon, seinen ersten Sohn, und Heth,
Kanaani alikuwa baba wa: Sidoni mzaliwa wake wa kwanza, Hethi,
16 Jebusi, Emori, Girgasi,
Wayebusi, Waamori, Wagirgashi,
17 Hivi, Arki, Sini,
Wahivi, Waariki, Wasini,
18 Arvadi, Zemari und Hamathi. Daher sind ausgebreitet die Geschlechter der Kanaaniter.
Waarvadi, Wasemari na Wahamathi. Baadaye koo za Wakanaani zilitawanyika,
19 Und ihre Grenzen waren von Zidon an durch Gerar bis gen Gasa, bis man kommt gen Sodoma, Gomorrha, Adama, Zeboim und bis gen Lasa.
na mipaka ya Kanaani ilienea kutoka Sidoni kuelekea Gerari hadi Gaza, kisha kuelekea Sodoma, Gomora, Adma na Seboimu, hadi kufikia Lasha.
20 Das sind die Kinder Hams in ihren Geschlechtern, Sprachen, Ländern und Leuten.
Hawa ni wana wa Hamu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
21 Sem aber, Japheths, des größern, Bruder, zeugete auch Kinder, der ein Vater ist aller Kinder von Eber.
Shemu ambaye ni ndugu mkubwa wa Yafethi, kwake kulizaliwa wana pia. Shemu alikuwa baba wa wana wote wa Eberi.
22 Und dies sind seine Kinder: Elam, Assur, Arphachsad, Lud und Aram.
Wana wa Shemu walikuwa: Elamu, Ashuru, Arfaksadi, Ludi na Aramu.
23 Die Kinder aber von Aram sind diese: Uz, Hut, Gether und Mas.
Wana wa Aramu walikuwa: Usi, Huli, Getheri na Mesheki.
24 Arphachsad aber zeugete Salah, Salah zeugete Eber.
Arfaksadi alikuwa baba wa Shela, naye Shela akamzaa Eberi.
25 Eber zeugete zween Söhne. Einer hieß Peleg, darum daß zu seiner Zeit die Welt zerteilet ward; des Bruder hieß Jaketan.
Eberi akapata wana wawili: Mmoja wao aliitwa Pelegi, kwa kuwa wakati wake ndipo dunia iligawanyika; nduguye aliitwa Yoktani.
26 Und Jaketan zeugete Almodad, Saleph, Hazarmaveth, Jarah,
Yoktani alikuwa baba wa: Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,
27 Hadoram, Usal, Dikela,
Hadoramu, Uzali, Dikla,
28 Obal, Abimael, Seba,
Obali, Abimaeli, Sheba,
29 Ophir, Hevila und Jobab. Das sind alle Kinder von Jaketan.
Ofiri, Havila na Yobabu. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.
30 Und ihre Wohnung war von Mesa an, bis man kommt gen Sephar, an den Berg gegen den Morgen.
Nchi waliyoishi ilienea toka Mesha kuelekea Sefari kwenye nchi ya vilima iliyoko mashariki.
31 Das sind die Kinder von Sem in ihren Geschlechtern, Sprachen, Ländern und Leuten.
Hao ndio wana wa Shemu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
32 Das sind nun die Nachkommen der Kinder Noahs in ihren Geschlechtern und Leuten. Von denen sind ausgebreitet die Leute auf Erden nach der Sintflut.
Hizi ndizo koo za wana wa Noa, kufuatana na vizazi vyao, katika mataifa yao. Kutokana na hawa mataifa yalienea duniani kote baada ya gharika.

< 1 Mose 10 >