< Esra 2 >

1 Dies sind die Kinder aus den Landen, die heraufzogen aus dem Gefängnis, die Nebukadnezar, der König zu Babel, hatte gen Babel geführet, und wieder gen Jerusalem und nach Juda kamen, ein jeglicher in seine Stadt.
Basi hawa ndio watu wa jimbo waliotoka uhamishoni, ambao Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa amewachukua mateka hadi Babeli (walirudi Yerusalemu na Yuda, kila mmoja kwenye mji wake,
2 Und kamen mit Serubabel, Jesua, Nehemia, Seraja, Reelja, Mardochai, Bilsan, Mispar, Bigevai, Rehum und Baena. Dies ist nun die Zahl der Männer des Volks Israel:
wakiwa wamefuatana na Zerubabeli, Yeshua, Nehemia, Seraya, Reelaya, Mordekai, Bilshani, Mispari, Bigwai, Rehumu na Baana): Orodha ya wanaume kati ya watu wa Israeli ilikuwa:
3 der Kinder Pareos zweitausend hundert und zweiundsiebenzig;
wazao wa Paroshi 2,172
4 der Kinder Sephatja dreihundert und zweiundsiebenzig;
wazao wa Shefatia 372
5 der Kinder Arah, siebenhundert und fünfundsiebenzig;
wazao wa Ara 775
6 der Kinder Pahath-Moab, unter der Kindern Jesua, Joab, zweitausend achthundert und zwölf;
wazao wa Pahath-Moabu (wa jamaa ya Yeshua na Yoabu) 2,812
7 der Kinder Elam tausend zweihundert und vierundfünfzig;
wazao wa Elamu 1,254
8 der Kinder Sathu neunhundert und fünfundvierzig;
wazao wa Zatu 945
9 der Kinder Sakai siebenhundert und sechzig;
wazao wa Zakai 760
10 der Kinder Bani sechshundert und zweiundvierzig;
wazao wa Bani 642
11 der Kinder Bebai sechshundert und dreiundzwanzig;
wazao wa Bebai 623
12 der Kinder Asgad tausend zweihundert und zweiundzwanzig;
wazao wa Azgadi 1,222
13 der Kinder Adonikam sechshundert und sechsundsechzig;
wazao wa Adonikamu 666
14 der Kinder Bigevai zweitausend und sechsundfünfzig;
wazao wa Bigwai 2,056
15 der Kinder Adin vierhundert und vierundfünfzig;
wazao wa Adini 454
16 der Kinder Ater von Hiskia achtundneunzig;
wazao wa Ateri (kupitia Hezekia) 98
17 der Kinder Bezai dreihundert und dreiundzwanzig;
wazao wa Besai 323
18 der Kinder Jorah hundert und zwölf
wazao wa Yora 112
19 der Kinder Hasum zweihundert und dreiundzwanzig;
wazao wa Hashumu 223
20 der Kinder Gibbar fünfundneunzig;
wazao wa Gibari 95
21 der Kinder Beth-Lehem hundert und dreiundzwanzig;
watu wa Bethlehemu 123
22 der Männer Netopha sechsundfünfzig;
watu wa Netofa 56
23 der Männer von Anathoth hundert und achtundzwanzig;
watu wa Anathothi 128
24 der Kinder Asmaveth zweiundvierzig;
watu wa Azmawethi 42
25 der Kinder von Kiriath-Arim, Kaphira und Beeroth siebenhundert und dreiundvierzig;
wazao wa Kiriath-Yearimu, Kefira na Beerothi 743
26 der Kinder von Rama und Gaba sechshundert und einundzwanzig;
wazao wa Rama na Geba 621
27 der Männer von Michmas hundert und zweiundzwanzig;
watu wa Mikmashi 122
28 der Männer von Bethel und Ai zweihundert und dreiundzwanzig;
watu wa Betheli na Ai 223
29 der Kinder Nebo zweiundfünfzig;
wazao wa Nebo 52
30 der Männer von Magbis hundert und sechsundfünfzig;
wazao wa Magbishi 156
31 der Kinder des andern Elam tausend zweihundert und vierundfünfzig;
wazao wa Elamu ile ingine 1,254
32 der Kinder Harim dreihundert und zwanzig;
wazao wa Harimu 320
33 der Kinder Lod, Hadid und Ono siebenhundert und fünfundzwanzig;
wazao wa Lodi, Hadidi na Ono 725
34 der Kinder Jereho dreihundert und fünfundvierzig;
wazao wa Yeriko 345
35 der Kinder Senaa dreitausend sechshundert und dreißig;
wazao wa Senaa 3,630
36 der Priester: der Kinder Jedaja vom Hause Jesua neunhundert und dreiundsiebenzig;
Makuhani: wazao wa Yedaya (kwa jamaa ya Yeshua) 973
37 der Kinder Immer tausend und zweiundfünfzig;
wazao wa Imeri 1,052
38 der Kinder Pashur tausend zweihundert und siebenundvierzig;
wazao wa Pashuri 1,247
39 der Kinder Harim tausend und siebenzehn;
wazao wa Harimu 1,017
40 der Leviten: der Kinder Jesua und Kadmiel von den Kindern Hodavja vierundsiebenzig;
Walawi: wazao wa Yeshua na Kadmieli (kupitia jamaa ya Hodavia) 74
41 der Sänger: der Kinder Assaph hundert und achtundzwanzig;
Waimbaji: wazao wa Asafu 128
42 der Kinder der Torhüter: die Kinder Sallum, die Kinder Ater, die Kinder Talmon, die Kinder Akub, die Kinder Hatita und die Kinder Sobai, allesamt hundert und neununddreißig;
Mabawabu wa lango la Hekalu: wazao wa Shalumu, Ateri, Talmoni, Akubu, Hatita na Shobai 139
43 der Nethinim: die Kinder Ziha, die Kinder Hasupha, die Kinder Tabaoth,
Watumishi wa Hekalu: wazao wa Siha, Hasufa, Tabaothi,
44 die Kinder Keros, die Kinder Sieha, die Kinder Padon,
wazao wa Kerosi, Siaha, Padoni,
45 die Kinder Lebana, die Kinder Hagaba, die Kinder Akub,
wazao wa Lebana, Hagaba, Akubu,
46 die Kinder Hagab, die Kinder Samlai, die Kinder Hanan,
wazao wa Hagabu, Shalmai, Hanani,
47 die Kinder Giddel, die Kinder Gahar, die Kinder Reaja,
wazao wa Gideli, Gahari, Reaya,
48 die Kinder Rezin, die Kinder Nekoda, die Kinder Gasam,
wazao wa Resini, Nekoda, Gazamu,
49 die Kinder Usa, die Kinder Paseah, die Kinder Besai,
wazao wa Uza, Pasea, Besai,
50 die Kinder Asna, die Kinder Meunim, die Kinder Nephusim,
wazao wa Asna, Meunimu, Nefusimu,
51 die Kinder Bakbuk, die Kinder Hakupha, die Kinder Harhur,
wazao wa Bakbuki, Hakufa, Harhuri,
52 die Kinder Bazeluth, die Kinder Mehida, die Kinder Harsa,
wazao wa Basluthi, Mehida, Harsha,
53 die Kinder Barkom, die Kinder Sissera, die Kinder Thamah,
wazao wa Barkosi, Sisera, Tema,
54 die Kinder Neziah, die Kinder Hatipha;
wazao wa Nesia na Hatifa.
55 die Kinder der Knechte Salomos: die Kinder Sotai, die Kinder Sophereth, die Kinder Pruda,
Wazao wa watumishi wa Solomoni: wazao wa Sotai, Hasaferethi, Peruda,
56 die Kinder Jaela, die Kinder Darkon, die Kinder Giddel,
wazao wa Yaala, Darkoni, Gideli,
57 die Kinder Sephatja, die Kinder Hattil, die Kinder Pochereth von Zebaim, die Kinder Ami.
wazao wa Shefatia, Hatili, Pokereth-Hasebaimu na Ami.
58 Aller Nethinim und Kinder der Knechte Salomos waren zusammen dreihundert und zweiundneunzig.
Watumishi wa Hekalu wote na wazao wa watumishi wa Solomoni 392
59 Und diese zogen auch mit herauf: Mithel, Melah, Thel-Harsa, Cherub-Addon und Immer; aber sie konnten nicht anzeigen ihrer Väter Haus, noch ihren Samen, ob sie aus Israel wären.
Wafuatao walikuja kutoka miji ya Tel-Mela, Tel-Harsha, Kerubu, Adoni na Imeri, lakini hawakuweza kuthibitisha kwamba jamaa zao zilikuwa uzao wa Israeli:
60 Die Kinder Delaja, die Kinder Tobia, die Kinder Nekoda: sechshundert und zweiundfünfzig.
wazao wa Delaya, Tobia na Nekoda 652
61 Und von den Kindern der Priester: die Kinder Habaja, die Kinder Hakoz, die Kinder Barsillai, der aus den Töchtern Barsillais, des Gileaditers, ein Weib nahm und ward unter derselben Namen genannt.
Kutoka miongoni mwa makuhani: Wazao wa Hobaya, Hakosi, Barzilai (mtu aliyekuwa amemwoa binti wa Barzilai, Mgileadi, naye akaitwa kwa jina hilo).
62 Dieselben suchten ihre Geburtsregister und fanden keine; darum wurden sie vom Priestertum los.
Hawa walitafuta orodha za jamaa zao, lakini hawakuonekana humo, kwa hiyo waliondolewa kutoka kundi la makuhani kwa kuwa walihesabiwa kuwa najisi.
63 Und Hathirsatha sprach zu ihnen, sie sollten nicht essen vom Allerheiligsten, bis ein Priester stünde mit dem Licht und Recht.
Mtawala aliagiza kuwa wasile chochote miongoni mwa vyakula vitakatifu hadi kuwe kuhani atakayehudumu kwa Urimu na Thumimu.
64 Der ganzen Gemeine, wie ein Mann, war zweiundvierzigtausend dreihundert und sechzig,
Jumla ya watu wote waliorudi walikuwa 42,360;
65 ausgenommen ihre Knechte und Mägde, der waren siebentausend dreihundert, und siebenunddreißig. Und hatten zweihundert Sänger und Sängerinnen,
tena zaidi ya hao walikuwepo watumishi wa kiume na wa kike 7,337; pia walikuwamo waimbaji wanaume na wanawake 200.
66 siebenhundert und sechsunddreißig Rosse, zweihundert und fünfundvierzig Mäuler,
Walikuwa na farasi 736, nyumbu 245,
67 vierhundert und fünfunddreißig Kamele und sechstausend siebenhundert und zwanzig Esel.
ngamia 435 na punda 6,720.
68 Und etliche der obersten Väter, da sie kamen zum Hause des HERRN zu Jerusalem, wurden sie freiwillig zum Hause Gottes, daß man es setzte auf seine Stätte.
Walipofika kwenye nyumba ya Bwana huko Yerusalemu, baadhi ya viongozi wa jamaa walitoa sadaka za hiari kwa ajili ya kujenga upya nyumba ya Mungu katika eneo lake.
69 Und gaben nach ihrem Vermögen zum Schatz ans Werk einundsechzigtausend Gülden und fünftausend Pfund Silbers und hundert Priesterröcke.
Wakatoa kwa kadiri ya uwezo wao na kutia katika hazina darkoni 61,000 za dhahabu, mane 5,000 za fedha, na mavazi 100 ya ukuhani kwa ajili ya kazi hiyo.
70 Also setzten sich die Priester und die Leviten und etliche des Volks und die Sänger und die Torhüter und die Nethinim in ihre Städte und alles Israel in seine Städte.
Makuhani, Walawi, waimbaji, mabawabu, na watumishi wa Hekalu waliishi katika miji yao wenyewe, pamoja na baadhi ya watu wengine, nao Waisraeli waliosalia waliishi katika miji yao.

< Esra 2 >