< 2 Samuel 22 >

1 Und David redete vor dem HERRN die Worte dieses Liedes zur Zeit, da ihn der HERR errettet hatte von der Hand aller seiner Feinde und von der Hand Sauls, und sprach:
Daudi alimwimbia Bwana maneno ya wimbo huu wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli.
2 Der HERR ist mein Fels und meine Burg und mein Erretter.
Akasema: “Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu,
3 Gott ist mein Hort, auf den ich traue, mein Schild und Horn meines Heils, mein Schutz und meine Zuflucht, mein Heiland, der du mir hilfst vom Frevel.
Mungu wangu ni mwamba wangu, ambaye kwake ninakimbilia, ngao yangu na pembe ya wokovu wangu. Yeye ni ngome yangu, kimbilio langu na mwokozi wangu, huniokoa kutoka kwa watu wenye jeuri.
4 Ich will den HERRN loben und anrufen, so werde ich von meinen Feinden erlöset werden.
Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
5 Denn es hatten mich umfangen die Schmerzen des Todes, und die Bäche Belials erschreckten mich.
“Mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
6 Der Höllen Bande umfingen mich, und des Todes Stricke überwältigten mich. (Sheol h7585)
Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol h7585)
7 Wenn mir angst ist, so rufe ich den HERRN an und schreie zu meinem Gott, so erhöret er meine Stimme von seinem Tempel, und mein Geschrei kommt vor ihn zu seinen Ohren.
Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu. Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika masikioni mwake.
8 Die Erde bebete und ward bewegt, die Grundfesten des Himmels regten sich und bebeten, da er zornig war.
“Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya mbingu ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
9 Dampf ging auf von seiner Nase und verzehrend Feuer von seinem Munde, daß es davon blitzte.
Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
10 Er neigete den Himmel und fuhr herab, und Dunkel war unter seinen Füßen.
Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
11 Und er fuhr auf dem Cherub und flog daher; und er schwebete auf den Fittichen des Windes.
Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
12 Sein Gezelt um ihn her war finster und schwarze dicke Wolken.
Alifanya giza hema lake la kujifunika: mawingu meusi ya mvua ya angani.
13 Von dem Glanz vor ihm brannte es mit Blitzen.
Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
14 Der HERR donnerte vom Himmel, und der Höchste ließ seinen Donner aus.
Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
15 Er schoß seine Strahlen und zerstreuete sie; er ließ blitzen und schreckte sie.
Aliipiga mishale na kutawanya adui, umeme wa radi na kuwafukuza.
16 Da sah man Wassergüsse, und des Erdbodens Grund ward aufgedeckt von dem Schelten des HERRN, von dem Odem und Schnauben seiner Nase.
Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwake Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwake.
17 Er schickte aus von der Höhe und holte mich und zog mich aus großen Wassern.
“Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
18 Er errettete mich von meinen starken Feinden, von meinen Hassern, die mir zu mächtig waren,
Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
19 die mich überwältigten zur Zeit meines Unfalls. Und der HERR ward meine Zuversicht.
Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
20 Er führete mich aus in den Raum; er riß mich heraus, denn er hatte Lust zu mir.
Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
21 Der HERR tut wohl an mir nach meiner Gerechtigkeit; er vergilt mir nach der Reinigkeit meiner Hände.
“Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
22 Denn ich halte die Wege des HERRN und bin nicht gottlos wider meinen Gott.
Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
23 Denn alle seine Rechte habe ich vor Augen und seine Gebote werfe ich nicht von mir;
Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
24 sondern ich bin ohne Wandel vor ihm und hüte mich vor Sünden.
Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
25 Darum vergilt mir der HERR nach meiner Gerechtigkeit, nach meiner Reinigkeit vor seinen Augen.
Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu, sawasawa na usafi wangu machoni pake.
26 Bei den Heiligen bist du heilig, bei den Frommen bist du fromm,
“Kwa yeye aliye mwaminifu unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia unajionyesha kutokuwa na hatia,
27 bei den Reinen bist du rein und bei den Verkehrten bist du verkehrt.
kwa aliye mtakatifu unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka unajionyesha kuwa mkaidi.
28 Denn du hilfst dem elenden Volk und mit deinen Augen niedrigest du die Hohen.
Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini macho yako ni juu ya wenye kiburi ili uwashushe.
29 Denn du, HERR, bist meine Leuchte. Der HERR machet meine Finsternis licht.
Wewe ni taa yangu, Ee Bwana. Bwana hulifanya giza langu kuwa mwanga.
30 Denn mit dir kann ich Kriegsvolk zerschmeißen und mit meinem Gott über die Mauern springen.
Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
31 Gottes Wege sind ohne Wandel, des HERRN Reden sind durchläutert; er ist ein Schild allen, die ihm vertrauen.
“Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu; neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
32 Denn ist ein Gott ohne den HERRN? Und wo ist ein Hort, ohne unser Gott?
Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
33 Gott stärket mich mit Kraft und weiset mir einen Weg ohne Wandel.
Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
34 Er machet meine Füße gleich den Hirschen und stellet mich auf meine Höhe.
Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
35 Er lehret meine Hände streiten und lehret meinen Arm den ehernen Bogen spannen.
Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
36 Und gibst mir den Schild deines Heils. Und wenn du mich demütigest, machst du mich groß.
Hunipa ngao yako ya ushindi, unajishusha chini ili kuniinua.
37 Du machst unter mir Raum zu gehen, daß meine Knöchel nicht gleiten.
Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
38 Ich will meinen Feinden nachjagen und sie vertilgen; und will nicht umkehren, bis ich sie umgebracht habe.
“Niliwafuatia adui zangu na nikawaseta, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
39 Ich will sie umbringen und zerschmeißen, und sollen mir nicht widerstehen; sie müssen unter meine Füße fallen.
Niliwaseta kabisa, nao hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
40 Du kannst mich rüsten mit Stärke zum Streit; du kannst unter mich werfen, die sich wider mich setzen.
Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
41 Du gibst mir meine Feinde in die Flucht, daß ich verstöre, die mich hassen.
Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
42 Sie lieben sich zu, aber da ist kein Helfer; zum HERRN, aber er antwortet ihnen nicht.
Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
43 Ich will sie zerstoßen wie Staub auf der Erde; wie Kot auf der Gasse will ich sie verstäuben und zerstreuen.
Niliwaponda kama mavumbi ya nchi; niliwaponda na kuwakanyaga kama tope barabarani.
44 Du hilfst mir von dem zänkischen Volk und behütest mich zum Haupt unter den Heiden; ein Volk, das ich nicht kannte, dienet mir.
“Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu wangu; umenihifadhi mimi kama kiongozi wa mataifa. Watu ambao sikuwajua wananitumikia,
45 Den fremden Kindern hat es wider mich gefehlet, und gehorchen mir mit gehorsamen Ohren.
nao wageni huja wakininyenyekea, mara wanisikiapo, hunitii.
46 Die fremden Kinder sind verschmachtet und zappeln in ihren Banden.
Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
47 Der HERR lebet; und gelobet sei mein Hort, und Gott, der Hort meines Heils, müsse erhaben werden,
“Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu, Mwamba, Mwokozi wangu!
48 der Gott, der mir die Rache gibt und wirft die Völker unter mich.
Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, ayawekaye mataifa chini yangu,
49 Er hilft mir aus von meinen Feinden. Du erhöhest mich aus denen, die sich wider mich setzen; du hilfst mir von den Frevlern.
aniwekaye huru toka kwa adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
50 Darum will ich dir danken, HERR, unter den Heiden und deinem Namen lobsingen,
Kwa hiyo nitakusifu, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.
51 der seinem Könige groß Heil beweiset und wohltut seinem Gesalbten David und seinem Samen ewiglich.
Humpa mfalme wake ushindi mkuu; huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.”

< 2 Samuel 22 >