< Psalm 72 >
1 Von Salomo. Gott, gieb dein Gericht dem Könige und deine Gerechtigkeit dem Königssohn.
Mpe mfalme amri ya haki yako, Mungu, haki yako kwa wana wa mfalme.
2 Möge er dein Volk mit Gerechtigkeit richten und deine Elenden mit Recht.
Naye awaamue watu wako kwa haki na maskini wako kwa haki sawa.
3 Mögen die Berge dem Volke Heil tragen, und die Hügel, durch Gerechtigkeit.
Milima iwazalie watu amani; vilima navyo vizae haki.
4 Er wird den Elenden im Volke Recht schaffen; er wird den Kindern des Armen helfen und den Gewaltthätigen zermalmen.
Naye awahukumu watu maskini; awaokoe watoto wa wahitaji na kuwavunja vipande vipande wenye kuwatesa.
5 Er wird dauern, so lange wie die Sonne und im Angesichte des Mondes Geschlecht auf Geschlecht!
Na wakuheshimu wewe wakati wa jua, na kwa kipindi cha kudumu kwa mwezi katika vizazi vyote.
6 Er wird sich herabsenken wie Regen auf die frischgemähte Aue, wie Regenschauer, die das Land befeuchten.
Naye apate kuja kama mvua juu ya nyasi zilizokatwa, kama manyuyu yanyunyizayo nchi.
7 In seinen Tagen wird der Fromme blühn, und Fülle des Friedens herrschen, bis kein Mond mehr ist.
Mwenye haki na astawi kwa wakati wake, na amani iwepo kwa wingi mpaka mwezi utakapotoweka.
8 Und er wird herrschen von Meer zu Meer und vom Euphratstrome bis zu den Enden der Erde.
Na awe na mamlaka toka bahari na bahari, na kutoka Mto hadi miisho ya dunia.
9 Vor ihm werden die Widersacher ihre Kniee beugen, und seine Feinde müssen Staub lecken.
Na wote waishio jangwani wainame mbele zake; adui zake na walambe mavumbi.
10 Die Könige von Tarsis und den Inseln werden Geschenke entrichten, die Könige von Saba und Seba Tribut herzubringen.
Wafalme wa Tashishi na visiwa walete kodi; wafalme wa Sheba na Seba watoe zawadi.
11 Und alle Könige werden sich vor ihm niederwerfen, alle Völker ihm dienen.
Hakika wafalme wote wamwinamie yeye; mataifa yote yamtumikie yeye.
12 Denn er rettet den Armen, der um Hilfe schreit, und den Elenden und den, der keinen Helfer hat.
Kwa kuwa yeye humsaidia mhitaji na maskini asiye na msaidizi.
13 Er erbarmt sich des Geringen und Armen und den Seelen der Armen hilft er.
Yeye huwahurumia maskini na wahitaji, na huokoa maisha ya wahitaji.
14 Aus Bedrückung und Gewaltthat erlöst er ihre Seele, und kostbar ist ihr Blut in seinen Augen.
Huyaokoa maisha yao dhidi ya mateso na vurugu, na damu yao ni ya thamani machoni pake.
15 Und er wird leben, und man wird ihm vom Golde Sabas geben; man wird beständig für ihn beten, allezeit wird man ihn segnen.
Naye apate kuishi! Na dhahabu za Sheba apewe yeye. Watu wamuombee yeye siku zote; Mungu ambariki daima.
16 Es wird Überfluß von Korn im Lande sein, auf dem Gipfel der Berge; seine Frucht wird rauschen, wie der Libanon, und aus der Stadt werden sie hervorblühn, wie die Pflanzen aus der Erde.
Kuwepo na nafaka nyingi katika ardhi; juu ya milima kuwe na mawimbi ya mimea. Matunda yake yawe kama Lebanoni; watu wasitawi katika miji kama nyansi za kondeni.
17 Sein Name wird ewig währen; im Angesichte der Sonne wird sein Name sprossen. Mit ihm werden sich alle Geschlechter der Erde einander Segen wünschen, alle Völker werden ihn glücklich preisen.
Jina lake lidumu milele; jina lake ilindelee kama vile jua ling'aavyo; watu wabarikiwe katika yeye; mataifa yote wamwite mbarikiwa.
18 Gepriesen sei Jahwe Gott, der Gott Israels, der allein Wunder thut,
Yahwe Mungu, Mungu wa Israel, atukuzwe, ambaye pekee hufanya mambo ya ajabu.
19 und gepriesen sei sein herrlicher Name in Ewigkeit, und alle Lande müssen erfüllt werden von seiner Herrlichkeit! Amen, Amen!
Jina lake tukufu litukuzawe milele, nayo nchi yote ijazwe na utukufu wake. Amina, Amina.
20 Zu Ende sind die Gebete Davids, des Sohnes Isais.
Maombi ya Daudi mwana wa Yese yamemalizika. Kutatu cha tatu