< Psalm 106 >

1 Rühmet Jah! Danket Jahwe, denn er ist gütig; denn ewig währt seine Gnade.
Msifuni Bwana. Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
2 Wer kann die Machtthaten Jahwes ausreden, all seinen Ruhm verkündigen?
Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana au kutangaza kikamilifu sifa zake?
3 Wohl denen, die auf Recht halten, dem, der zu jeder Zeit Gerechtigkeit übt.
Heri wale wanaodumisha haki, ambao daima wanafanya yaliyo mema.
4 Gedenke meiner, Jahwe, nach der Huld, die du deinem Volke verheißen; suche mich heim mit deiner Hilfe,
Ee Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako, uwe msaada wangu unapowaokoa,
5 daß ich am Glücke deiner Auserwählten meine Lust schaue, mich an der Freude deines Volkes freue, mit deinem Eigentum mich rühme!
ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako, niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako, na kuungana na urithi wako katika kukusifu.
6 Wir haben gesündigt samt unsern Vätern, haben uns verschuldet, sind gottlos gewesen.
Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda, tumekosa na tumetenda uovu.
7 Unsere Väter in Ägypten begriffen deine Wunder nicht, gedachten nicht an deine große Gnade und empörten sich wider den Höchsten am Schilfmeer.
Wakati baba zetu walipokuwa Misri, hawakuzingatia maajabu yako, wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako, bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu.
8 Aber er half ihnen um seines Namens willen, um seine Stärke kund zu thun.
Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake, ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.
9 Er bedrohte das Schilfmeer, daß es vertrocknete, und führte sie durch die Fluten wie auf einer Trift.
Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka, akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani.
10 Er rettete sie aus der Gewalt dessen, der sie haßte, und befreite sie aus der Gewalt des Feindes.
Aliwaokoa mikononi mwa adui; kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.
11 Die Gewässer bedeckten ihre Bedränger; kein einziger von ihnen blieb übrig.
Maji yaliwafunika adui zao, hakunusurika hata mmoja.
12 Da glaubten sie an seine Worte, sangen seinen Ruhm.
Ndipo walipoamini ahadi zake, nao wakaimba sifa zake.
13 Eilends vergaßen sie seine Thaten, warteten nicht auf seinen Entschluß.
Lakini mara walisahau aliyowatendea, wala hawakungojea shauri lake.
14 Sie verfielen in der Steppe auf ein Gelüst und versuchten Gott in der Einöde.
Jangwani walitawaliwa na tamaa zao, walimjaribu Mungu nyikani.
15 Da gab er ihnen, was sie begehrten, und ließ die Darre in sie kommen.
Kwa hiyo aliwapa kile walichoomba, lakini akatuma juu yao ugonjwa wa kudhoofisha.
16 Und sie wurden eifersüchtig auf Mose im Lager, auf Aaron, den Heiligen Jahwes.
Kambini walimwonea wivu Mose, na pia Aroni aliyekuwa amewekwa wakfu kwa Bwana.
17 Die Erde that sich auf und verschlang Dathan und bedeckte die Rotte Abirams.
Ardhi ilifunguka ikawameza Dathani, ikawazika Abiramu na kundi lake.
18 Und Feuer zündete unter ihrer Rotte, die Flamme verbrannte die Gottlosen.
Moto uliwaka katikati ya wafuasi wao, mwali wa moto uliwateketeza waovu.
19 Sie machten ein Kalb am Horeb und warfen sich nieder vor einem Gußbild
Huko Horebu walitengeneza ndama, na kuabudu sanamu ya kusubu kwa chuma.
20 und vertauschten ihren Herrlichen mit dem Bild eines Stiers, der Gras frißt.
Waliubadilisha Utukufu wao kwa sanamu ya fahali, ambaye hula majani.
21 Sie vergaßen Gottes, ihres Erretters, der Großes in Ägypten gethan hatte,
Walimsahau Mungu aliyewaokoa, aliyekuwa ametenda mambo makuu huko Misri,
22 Wunderbares im Lande Hams, Furchtbares am Schilfmeer.
miujiza katika nchi ya Hamu na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu.
23 Da gedachte er, sie zu vertilgen, wenn nicht Mose, sein Auserwählter, vor ihm in die Bresche getreten wäre, um seinen Grimm vom Vertilgen wieder abzubringen.
Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza: kama Mose mteule wake, asingesimama kati yao na Mungu kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza.
24 Sie verschmähten das wonnige Land und glaubten seinem Worte nicht.
Kisha waliidharau ile nchi nzuri, hawakuiamini ahadi yake.
25 Sie murrten in ihren Zelten, hörten nicht auf die Stimme Jahwes.
Walinungʼunika ndani ya mahema yao, wala hawakumtii Bwana.
26 Da erhob er ihnen seine Hand und schwur, daß er sie in der Wüste fällen
Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba atawafanya waanguke jangwani,
27 und ihre Nachkommen unter die Völker zerstreuen und in die Länder versprengen wolle.
kuwatawanya wazao wao waanguke miongoni mwa mataifa, na kuwatawanya katika nchi zote.
28 Sie hingen sich an Baal Peor und aßen von den Opfern der toten Götzen.
Walijifunga nira na Baali wa Peori, wakala dhabihu zilizotolewa kwa miungu isiyo na uhai.
29 Und sie erzürnten ihn durch ihre Thaten; da fuhr eine Plage unter sie.
Waliichochea hasira ya Bwana, wakamkasirisha kwa matendo yao maovu, nayo tauni ikazuka katikati yao.
30 Pinehas aber trat auf und richtete, da ward der Plage Einhalt gethan.
Lakini Finehasi alisimama na kuingilia kati, nayo tauni ikazuiliwa.
31 Und das wurde ihm als Gerechtigkeit zugerechnet durch alle folgenden Geschlechter bis in Ewigkeit.
Hili likahesabiwa kwake haki, kwa vizazi visivyo na mwisho vijavyo.
32 Sodann erzürnten sie Gott am Hader-Wasser, und es erging Mose um ihretwillen übel.
Kwenye maji ya Meriba, walimkasirisha Bwana, janga likampata Mose kwa sababu yao;
33 Denn sie hatten seinem Geiste widerstrebt, und er redete unbedacht mit seinen Lippen.
kwa maana walimwasi Roho wa Mungu, na maneno yasiyofaa yakatoka midomoni kwa Mose.
34 Sie vertilgten nicht die Völker, die zu vertilgen Jahwe ihnen befohlen hatte.
Hawakuyaangamiza yale mataifa kama Bwana alivyowaagiza,
35 Sie ließen sich mit den Heiden ein und lernten ihre Werke;
bali walijichanganya na mataifa na wakazikubali desturi zao.
36 sie dienten ihren Götzen, und sie wurden ihnen zum Fallstrick.
Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.
37 Sie opferten Söhne und Töchter den Dämonen
Wakawatoa wana wao na binti zao dhabihu kwa mashetani.
38 und vergossen unschuldiges Blut, das Blut ihrer Söhne und Töchter, die sie den Götzen Kanaans opferten, daß das Land durch Blutschuld entweiht ward.
Walimwaga damu isiyo na hatia, damu za wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.
39 Sie verunreinigten sich durch ihre Werke und verübten Buhlerei mit ihren Thaten.
Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.
40 Da entbrannte der Zorn Jahwes gegen sein Volk, und er verabscheute sein Eigentum.
Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake na akauchukia sana urithi wake.
41 Er überlieferte sie in die Gewalt der Heiden, daß ihre Hasser über sie herrschten.
Akawakabidhi kwa mataifa na adui zao wakawatawala.
42 Und ihre Feinde bedrückten sie, und sie wurden unter ihre Gewalt gebeugt.
Adui zao wakawaonea na kuwatia chini ya mamlaka yao.
43 Viele Male errettete er sie; sie aber waren widerspenstig in ihrem Vorhaben und sanken durch ihre Verschuldung.
Mara nyingi aliwaokoa lakini walikuwa wamezama kwenye uasi, nao wakajiharibu katika dhambi zao.
44 Und er sah ihre Not an, als er ihr Flehen vernahm,
Lakini akaangalia mateso yao wakati aliposikia kilio chao;
45 und gedachte ihnen zu gut an seinen Bund und ließ sich's leid sein nach seiner großen Gnade.
kwa ajili yao akakumbuka agano lake, na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.
46 Er schaffte, daß sie Erbarmen fanden bei allen, die sie gefangen hielten.
Akawafanya wahurumiwe na wote waliowashikilia mateka.
47 Hilf uns, Jahwe, unser Gott, und sammle uns aus den Heiden, daß wir deinem heiligen Namen danken, uns deines Lobpreises rühmen!
Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe. Tukusanye tena kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.
48 Gepriesen sei Jahwe, der Gott Israels, von Ewigkeit bis zu Ewigkeit, und alles Volk spreche: Amen! Rühmet Jah!
Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Watu wote na waseme, “Amen!” Msifuni Bwana.

< Psalm 106 >