< 4 Mose 33 >

1 Dies sind die Züge der Israeliten, in denen ihre Heerscharen unter der Führung Moses und Aarons den Wegzug aus Ägypten vollführt haben.
Hizi ndizo safari za wana wa Israeli hapo walipotoka katika nchi ya Misri pamoja na makundi yao ya kijeshi chini ya uongozi wa Musa na Haruni.
2 Und Mose verzeichnete nach dem Befehle Jahwes die Orte, von denen ihre Züge ausgingen; und dies sind ihre Züge von einem Ausgangsorte zum andern.
Musa aliandika maeneo yote tangu walipoondoka mpaka walipofika, kama alivyoamuriwa na BWANA. Hizi ndizo safari zao kama kutoka kwao kulivyokuwa kwa kila walipotoka.
3 Sie brachen auf von Raemses im ersten Monat, am fünfzehnten Tage des ersten Monats. Am Tage nach dem Passah zogen die Israeliten schlagbereit aus vor den Augen aller Ägypter,
Mwezi wa kwanza walisafiri kutoka Ramesi, waliondoka siku ya kumi na tano. Asubuhi siku iliyofuata baada ya Pasaka, Wana wa Israeli waliondoka wazi wazi, mbele ya machoya Wamisri wote.
4 während die Ägypter alle Erstgebornen begruben, die Jahwe ihnen getötet hatte; denn Jahwe hatte ihre Götter seine Macht fühlen lassen.
Hii ilitokea wakati Wamisiri walipokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza, ambao BWANA alikuwa amewaua miongoni mwao, kwa kuwa pia alikuwa ameiadhibu miungu yao.
5 Und die Israeliten brachen auf von Raemses und lagerten sich in Suchoth.
Wana wa Israeli walisafiri kutoka Ramesi na kuweka kambi
6 Und sie brachen auf von Suchoth und lagerten sich in Etham, welches am Rande der Steppe liegt.
Sukothi. Walisafiri toka Sukothi na kuweka kambi Ethamu, mwisho wa nyika.
7 Und sie brachen auf von Etham und wandten sich nach Pi-Hahiroth, welches östlich von Baal Zephon liegt, und lagerten sich östlich von Migdol.
Wakasafiri kutoka Ethamu wakarudi mpaka Pi-Hahirothi, ambayo inaikabili Baali Zephoni, ambapo waliweka kambi kuikabili Migidoli
8 Und sie brachen auf von Pi-Hahiroth und zogen mitten durch das Meer hinüber in die Steppe und wanderten drei Tagereisen weit in der Steppe von Etham und lagerten sich in Mara.
Kisha wakasafiri toka mkabala wa Pi-Hairothi na kupita katikati ya bahari kuelekea nyikani. Wakasafiri safari ya siku tatu katika nyika ya Ethamu na kuweka kambi Mara.
9 Und sie brachen auf von Mara und gelangten nach Elim; in Elim aber gab es zwölf Quellen und siebzig Palmbäume, und sie lagerten sich daselbst.
Wakasafiri kutoka Mara kufika Elimu. Pale Elimu kulikuwa na chemichemi kumi na mbili za maji na miti sabini ya mitende. hapo ndipo walipoweka kambi.
10 Und sie brachen auf von Elim und lagerten sich am Schilfmeer.
Walisafiri kutoka Elimu na kuweka kambi karibu na Bahari ya Shamu.
11 Und sie brachen auf vom Schilfmeer und lagerten sich in der Steppe Sin.
Walisafiri kutoka Bahari ya Shamu na kuweka kambi katika nyika ya Sini.
12 Und sie brachen auf aus der Steppe Sin und lagerten sich in Dophka.
Walisafiri kutoka nyika ya Sini na kuweka kambi Dofka.
13 Und sie brachen auf von Dophka und lagerten sich in Alus.
Wakasafiri kutoka Dofka na kuweka kambi Alushi.
14 Und sie brachen auf von Alus und lagerten sich in Raphidim; und das Volk hatte daselbst kein Wasser zu trinken.
Wakasafiri kutoka Alushi na kuweka kambi Refidimu, ambapo watu walikosa maji ya kunywa.
15 Und sie brachen auf von Raphidim und lagerten sich in der Steppe am Sinai.
Walisafiri kutoka Refidimu na kuweka kambi kwenye nyika ya Sinai.
16 Und sie brachen auf aus der Steppe am Sinai und lagerten sich bei den Lustgräbern.
Walisafiri kutoka nyika ya Sinai na kuweka kambi Kibrothi Hataava.
17 Und sie brachen auf von den Lustgräbern und lagerten sich in Hazeroth.
Walisafiri kutoka Kibrothi Hataava na kuweka kambi Hazerothi.
18 Und sie brachen auf von Hazeroth und lagerten sich in Rithma.
Walisafiri kutoka Hazerothi na kuweka kambi Rithima.
19 Und sie brachen auf von Rithma und lagerten sich in Rimmon Parez.
Walisafiri kutoka Rithima na kuweka kambi Rimoni Perezi.
20 Und sie brachen auf von Rimmon Parez und lagerten sich in Libna.
Walisafiri kutoka Rimoni Perezi na kuweka kambi Libna.
21 Und sie brachen auf von Libna und lagerten sich in Rissa.
Walisafiri kutoka Libna na kuweka kambi Risa.
22 Und sie brachen auf von Rissa und lagerten sich in Kehelatha.
Walisafiri kutoka Risa na kuweka kambi Kehelatha.
23 Und sie brachen auf von Kehelatha und lagerten sich am Berge Sapher.
Walisafiri kutoka Kehelatha na kuweka kambi kwenye Mlima Sheferi.
24 Und sie brachen auf vom Berge Sapher und lagerten sich in Harada.
Walisafiri kutoka Mlima Sheferi na kuweka kambi Harada.
25 Und sie brachen auf von Harada und lagerten sich in Makheloth.
Walisafiri kutoka Harada na kuweka kambi Makelothi.
26 Und sie brachen auf von Makheloth und lagerten sich in Thahath.
Walisafiri kutoka Makelothi na kuweka kambi Tahathi.
27 Und sie brachen auf von Thahath und lagerten sich in Tharah.
Walisafiri kutoka Ttahalathi na kuweka kambi Tera.
28 Und sie brachen auf von Tharah und lagerten sich in Mithka.
Walisafiri kutokaTera na kuweka kambi Mithika.
29 Und sie brachen auf von Mithka und lagerten sich in Hasmona.
Walisafiri kutoka Mithika na kuweka kambi Hashimona.
30 Und sie brachen auf von Hasmona und lagerten sich in Moseroth.
Walisafiri kutoka Hashimona na kuweka kambi Moserothi.
31 Und sie brachen auf von Moseroth und lagerten sich in Bene Jaakan.
Walisafiri kutoka Moserothi na kuweka kambi Bene Jaakani.
32 Und sie brachen auf von Bene Jaakan und lagerten sich in Hor Hagidgad.
Walisafiri kutoka Bene Jaakani na kuweka kambi Hori Hagidigadi.
33 Und sie brachen auf von Hor Hagidgad und lagerten sich in Jotbatha.
Walisafiri kutoka Hori Hagidigadi na kuweka kambi Jotibatha.
34 Und sie brachen auf von Jotbatha und lagerten sich in Abrona.
Walisafiri kutoka Jotibatha na kuweka kambi Abrona.
35 Und sie brachen auf von Abrona und lagerten sich in Eziongeber.
Walisafiri kutoka Abrona na kuweka kambi Ezioni Geberi.
36 Und sie brachen auf von Eziongeber und lagerten sich in der Steppe Zin, das ist Kades.
Walisafiri toka Ezioini Geberi na kuweka kambi katika nyika ya Sini kule Kadeshi.
37 Und sie brachen auf von Kades und lagerten sich am Berge Hor an der Grenze des Landes Edom.
Walisafiri kutoka Kadeshi na kuweka kambi Mlima Hori, Pembezoni mwa nchi ya Edomu.
38 Und Aaron, der Priester, stieg nach dem Befehle Jahwes hinauf auf den Berg Hor und starb daselbst, im vierzigsten Jahre nach dem Wegzuge der Israeliten aus Ägypten, im fünften Monat, am ersten des Monats.
Hapo ndipo Haruni kuhani alipoenda kwenye Mlima Hori kwa amri ya BWANA na kufa kule mwaka wa arobaini bada ya Wisraeli kutoka katika nchi ya Misri, katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano.
39 Hundertunddreiundzwanzig Jahre war Aaron alt, als er auf dem Berge Hor starb.
Haruni alikuwa na umri wa mika 123 alipokufa pale juu ya Mlima Hori.
40 Als aber der Kanaaniter, der König von Arad, der im südlichsten Teile des Landes Kanaan seinen Sitz hatte, vom Anrücken der Israeliten hörte. . .
Wakanaani, mfalme wa Aradi, ambao waliishi kusini mwa nyika katika nchi ya Kanaani, walisikia juu ya ujio wa wana wa Israeli.
41 Und sie brachen auf vom Berge Hor und lagerten sich in Zalmona.
Walisafiri kutika Mlima Hori n a kuweka kambi Zalimona.
42 Und sie brachen auf von Zalmona und lagerten sich in Phunon.
Walisafiri kutoka Zalimona na kuweka kambi Punoni.
43 Und sie brachen auf von Phunon und lagerten sich in Oboth.
Walisafiri kutoka Punoni na kuweka kambi Obothi.
44 Und sie brachen auf von Oboth und lagerten sich in Jje Ha-abarim im Gebiete Moabs.
Walisafiri kutoka Obothi na kuweka kambi Abarimu, katika mpaka wa Moabu.
45 Und sie brachen auf von Jjim und lagerten sich in Dibon Gad.
Walisafiri kutoka Abarimu na kuweka kambi Diboni Gadi.
46 Und sie brachen auf von Dibon Gad und lagerten sich in Almon Diblathaim.
Walisafiri kutoka Diboni Gadi na kuweka kambi Alimoni Diblathaimu.
47 Und sie brachen auf von Almon Diblathaim und lagerten sich am Gebirge Abarim östlich von Nebo.
Walisafiri kutoka Alimoni Diblathaimu na kuweka kambi kwenye milima ya Abarimu mkabala na Nebo.
48 Und sie brachen auf vom Gebirge Abarim und lagerten sich in den Steppen Moabs am Jordan gegenüber Jericho.
Walisafiri kutoka mlima wa Abarimuna kuweka kambi kwenye nyanda za Moabu karibu na Yorodani huko Yeriko.
49 Und zwar lagerten sie am Jordan von Beth Hajesimoth bis AbeI Hasittim in den Steppen Moabs.
Waliweka kambi karibu na Yorodani, kutoka Bethi Jeshimothi mpaka Abeli Shitimu katika nyanda za Moabu.
50 Und Jahwe redete mit Mose in den Steppen Moabs am Jordan gegenüber Jericho also:
Hapo BWANA alinenana Musa katika nyanda za Moabu karibu na Yorodani kule Yeriko akasema,
51 Rede mit den Israeliten und sprich zu ihnen: Wenn ihr über den Jordan hinüber ins Land Kanaan gezogen seid,
“Nena na wana wa Israeli uwaambie. 'Mtakapovuka mto Yorodani kuingia Kanaani,
52 so müßt ihr alle Bewohner des Landes vor euch austreiben und alle ihre Bildwerke vernichten. Auch alle ihre Gußbilder sollt ihr vernichten und alle ihre Opferhöhen verwüsten
ndipo mtakapowafukuza wenyeji wote mbele yenu. Mtaziharibu sanamu zote za kuchongwa. Mtaziharibu sanamu zao za kusubu na kuharibu mahali pao pote palipoinuka.
53 und sollt das Land in Besitz nehmen und darin wohnen; denn euch habe ich das Land verliehen, daß ihr es besitzen sollt.
Mtachukua hiyo ardhi iwe mali yenu na muishi ndani yake, kwa sababu nimewapeni hiyo nchi iwe mali yenu.
54 Und zwar sollt ihr das Land vermittelst des Loses zum Besitz angewiesen erhalten, Stamm für Stamm; dem, der viele Köpfe zählt, sollt ihr einen ausgedehnten Erbbesitz geben, und dem, der wenig zählt, einen kleinen Erbbesitz. Worauf immer das Los für ihn fällt, das soll ihm zu teil werden; Stamm für Stamm sollt ihr das Land zum Besitz angewiesen erhalten.
Mtairithi hiyo nchi kwa kupiga kura, kwa kufuata kila ukoo. Kwa zile koo kubwa kubwa mtawapa sehemu kubwa ya ardhi, na kwa zile koo ndogo ndogo mtawapa sehemu ndogo ya ardhi. Kura itakapoanguka kwenye kila ukoo, hiyo ardhi itakuwa mali yake. Mtairithi ardhi kufuata ukoo wa kabilla la jamaa zenu.
55 Würdet ihr aber die Bewohner des Landes nicht vor euch austreiben, so werden die, die ihr von ihnen übrig laßt, zu Dornen in euren Augen und zu Stacheln in euren Seiten werden und werden euch bedrängen in dem Land, in dem ihr euren Wohnsitz habt;
Lakini kama hamtawafukuza wenyeji wa nchi hiyo watoke mbele yenu, ndipo wale watu mtakaowaruhusu wakae nanyi watakapokuwa kama sindano machoni mwenu na miiba katika mbavu zenu. Watayafanya maisha yenu yawe magumu katika nchi mnayoishi.
56 und so werde ich euch widerfahren lassen, was ich gedachte ihnen widerfahren zu lassen!
Ndipo itakapotokea kuwa kile ambacho Mimi ninakusudia kufanya kwa wale watu, Nitawafanyia pia ninyi'”

< 4 Mose 33 >