< Job 38 >
1 Dann antwortete Jahwe Hiob aus dem Wettersturm und sprach:
Ndipo Yahweh alimwita Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kumwambia,
2 Wer da verdunkelt Ratschluß mit Worten ohne Einsicht?
“Huyu ni nani aletaye giza katika mipango kwa njia ya maneno bila maarifa?
3 Auf, gürte deine Lenden wie ein Mann; so will ich dich fragen und du belehre mich!
Basi sasa jifunge kiunoni mwako kama mwanaume kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
4 Wo warst du, als ich die Erde gründete? Sag an, wenn du Einsicht besitzest?
Wewe ulikuwa wapi wakati nilipoitandaza misingi ya dunia? Niambie, kama unao ufahamu zaidi.
5 Wer hat ihre Maße bestimmt - du weißt es ja! - oder wer hat über sie die Meßschnur gespannt?
Je ni nani aliyeamuru vipimo vyake? Niambie, kama unajua, ni nani alivinyosha vipimo juu yake?
6 Worauf sind ihre Pfeiler eingesenkt, oder wer hat ihren Eckstein hingeworfen,
Misingi yake ilitandazwa juu ya nini? Ni nani aliyeliweka jiwe lake la pembeni
7 unter dem Jubel der Morgensterne allzumal, als alle Gottessöhne jauchzten?
wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja na wana wote wa Mungu walipopiga kelele kwa furaha?
8 Wer verwahrte hinter Thoren das Meer, als es hervorbrach, aus dem Mutterschoß hervorging,
Ni nani huifunga bahari kwa milango wakati inapofurika, kana kwamba inatoka katika tumbo,
9 als ich Gewölk zu seinem Kleide machte und dichte Finsternis zu seinen Windeln?
wakati nilipoyafanya mawingu kuwa ni mavazi yake, na giza nene kuwa mkanda wake wa kujifungia?
10 als ich ihm seine Grenze ausbrach und Riegel und Thore setzte
Hapo ilikuwa wakati nilipoweka bahari mpaka wangu, na nilipoweka makomeo yake na milango,
11 und sprach: “Bis hierher sollst du kommen und nicht weiter und hier soll sich brechen deiner Wogen Übermut!”
na wakati nilipoiambia, 'Unaweza kuja hapa kutoka mbali, lakini si zaidi; na hapa ndipo nitauweka mpaka kwa fahari ya mawimbi yako.'
12 Hast du je in deinem Leben dem Morgen geboten, dem Frührot seine Stätte angewiesen,
Je tangu mwanzo wa siku zako, ulishawahi kuigiza asubuhi ianze, na kuyafanya mapambazuko yajue sehemu yake katika mpangilio wa vitu,
13 die Säume der Erde zu fassen, daß die Frevler von ihr abgeschüttelt werden?
ili kwamba ishikilie sehemu za dunia ili watu waovu watikiswe mbali nayo.
14 Sie verwandelt sich wie Thon unter dem Siegel; sie stellen sich dar wie ein Gewand.
Dunia imebadilishwa katika mwonekano kama udongo unavyobadilika chini ya muhuri; vitu vyote husimama juu yake dhahiri kama cha kibindo cha nguo.
15 Und den Frevlern wird ihr Licht entzogen, und der schon erhobene Arm wird zerschmettert.
'Mwanga' wao umeondolewa kutoka kwa watu waovu; na mkono wao ulioinuliwa umevunjwa.
16 Bist du zu des Meeres Strudeln gelangt und bist du auf dem Grund der Tiefe gewandelt?
Je umeshaenda kwenye vyanzo vya maji ya bahari? Je umeshatembea sehemu za chini kabisa za kilindi?
17 Haben sich dir des Todes Thore aufgethan, und schautest du die Thore des tiefen Dunkels?
Je malango ya mauti yamefunuliwa kwako? Je umeshaona malango ya uvuli wa mauti?
18 Hast du der Erde Breiten überschaut? Sag an, wenn du das alles weißt!
Je umeifahamu dunia katika upana wake? Niambie kama unayajua yote hayo.
19 Wo hoch ist der Weg dahin, wo das Licht wohnt, und die Finsternis, - wo ist doch ihre Stätte,
Je iko wapi njia ya sehemu ya kupumzikia kwa mwanga, na kama ilivyo kwa giza, iko wapi sehemu yake?
20 daß du sie in ihr Gehege brächtest und die Pfade zu ihrem Hause kenntest?
Je unaweza kuuongoza mwanga na giza katika sehemu zake za kazi? Waweza kuitambua njia ya kurudi katika nyumba zao?
21 Du weißt es, denn damals wurdest du geboren, und deiner Tage Zahl ist groß!
Bila shaka unajua, kwa kuwa ulizaliwa wakati huo; hesabu ya siku zako ni kubwa sana!
22 Bist du zu den Speichern des Schnees gelangt und hast du die Speicher des Hagels erschaut,
Je ulishaingia katika ghala ya barafu, au umeshaiona ghala ya mawe ya mvua,
23 den ich aufgespart habe für die Drangsalszeit, für den Tag der Schlacht und des Kriegs?
vitu hivi nimeviweka kwa ajili ya siku za mateso, kwa siku za mapigano na vita?
24 Wo doch ist der Weg dahin, wo das Licht sich teilt, der Ost sich über die Erde verbreitet?
Je iko wapi njia ya mshindo wa mwanga hutokea au je upepo husambazwa kutoka mashariki juu ya dunia?
25 Wer hat dem Regen Kanäle gespalten und einen Weg dem Wetterstrahl,
Ni nani aliyezitengeneza mifereji ya gharika ya mvua, au ni nani aliyezifanya njia za milipuko ya radi,
26 um es regnen zu lassen auf menschenleeres Land, auf die Wüste, in der niemand wohnt,
na kuifanya mvua inyeshe juu ya nchi ambazo hakuna mtu aishiye ndani yake, na juu ya jangwa, ambayo ndani yake hakuna mtu yeyote,
27 um Öde und Wildnis zu sättigen und frischen Graswuchs sprießen zu lassen?
kwa kusudi la kutimiza mahitaji ya mikoa iliyo kame na yenye ukiwa, na kuyastawisha majani mororo?
28 Hat der Regen einen Vater, oder wer hat die Tautropfen gezeugt?
Je kuna baba wa mvua? Ni nani aliyeyafanya matone ya umande?
29 Aus wessen Schoße ging das Eis hervor, und des Himmels Reif, wer hat ihn geboren?
Je barafu ilitoka katika tumbo la nani? Na ni nani aliyeizaa theluji nyeupe katika anga?
30 Wie Stein verdichten sich die Wasser, und die Fläche der Flut hält fest zusammen.
Maji hujificha menyewe na kuwa kama jiwe; sehemu za juu za vilindi huwa kama barafu.
31 Vermagst du die Bande der Plejaden zu knüpfen oder die Fesseln des Orions zu lösen?
Je unaweza kuzifunga minyororo ya Kilimia, au kuvifungua vifundo vya Orioni?
32 Führst du die Tierkreisbilder heraus zu ihrer Zeit und leitest du den Bär samt seinen Jungen?
Je unaweza kuziongoza nyota kutokea katika nyakati zake? Je waweza kuongoza dubu pamoja na watoto wake?
33 Kennst du die Gesetze des Himmels oder bestimmst du seine Herrschaft über die Erde?
Je unazijua sheria za anga? Wewe uliweza kuanzisha sheria za anga juu ya dunia?
34 Erhebst du zur Wolke deine Stimme, daß Schwall von Wassern dich bedecke?
Je waweza kupaza sauti yako hadi mawinguni, ili kwamba maji mengi ya mvua yakufunike?
35 Entsendest du Blitze, daß sie hinfahren und zu dir sagen: Hier sind wir?
Je waweza kuagiza miali ya mwanga ili itokee, na kukwambia, 'Sisi tupo hapa'?
36 Wer hat ins Wolkendunkel Weisheit gelegt oder wer verlieh dem Luftgebilde Verstand?
Ni nani ameweka hekima katika mawingu au ni nani ameweka ufahamu kwa ukungu?
37 Wer zählt die Wolken mit Weisheit ab, und die Krüge des Himmels - wer legt sie um,
Nani anaweza kuyahesabu mawingu kwa maarifa yake? Na ni nani awezaye kuvimwaga viriba vya anga
38 wenn das Erdreich zu Gußwerk zusammenfließt, und die Schollen aneinander kleben?
wakati mavumbi yanapoungana kuwa kitu kigumu na mabonge ya dunia yanaposhikama kwa pamoja?
39 Erjagst du für die Löwin Beute und stillst du die Gier der jungen Löwen,
Je waweza kuwinda mawindo kwa ajili ya simba jike au kutosheleza hamu ya watoto wadogo wa simba
40 wenn sie sich in den Lagerstätten ducken, im Dickicht auf der Lauer liegen?
wakati wanapokwaruza kwaruza katika pango lao na kukaa katika kificho ili kulala katika hali ya kuvizia?
41 Wer bereitet dem Raben seine Zehrung, wenn seine Jungen zu Gott schreien, umherirren ohne Nahrung?
Ni nani aletaye mawindo kwa ajili ya kunguru wakati ambapo watoto wao wanapomlilia Mungu na kutangatanga kwa kukosa chakula?