< Job 26 >

1 Hiob antwortete und sprach:
Kisha Ayubu akajibu:
2 Wie trefflich hast du der Ohnmacht geholfen, den kraftlosen Arm gestützt,
“Tazama jinsi ulivyomsaidia mtu asiye na uwezo! Jinsi ulivyouokoa mkono ulio dhaifu!
3 wie trefflich den Unverständigen beraten und Weisheit in Fülle geoffenbart!
Ni shauri gani ulilompa yeye asiye na hekima? Nayo ni busara gani kubwa uliyoonyesha!
4 Wem hast du deine Reden vorgetragen, und wessen Geist hat aus dir gesprochen?
Ni nani aliyekusaidia kutamka maneno hayo? Nayo ni roho ya nani iliyosema kutoka kinywani mwako?
5 Die Schatten selbst werden in Beben versetzt unter den Wassern und ihren Bewohnern.
“Wafu wako katika maumivu makuu, wale walio chini ya maji na wale waishio ndani yake.
6 Nackt liegt die Unterwelt vor ihm, und unverhüllt der Abgrund. (Sheol h7585)
Mauti iko wazi mbele za Mungu; Uharibifu haukufunikwa. (Sheol h7585)
7 Er spannt den Norden über dem Leeren aus, läßt die Erde schweben über dem Nichts.
Hutandaza anga la kaskazini mahali patupu; naye huiningʼiniza dunia mahali pasipo na kitu.
8 Er bindet die Wasser in seine Wolken ein, ohne daß unter ihnen das Gewölk zerreißt.
Huyafungia maji kwenye mawingu yake, hata hivyo mawingu hayapasuki kwa uzito wake.
9 Er verhüllt den Anblick seines Throns, indem er sein Gewölk darüber breitet.
Huufunika uso wa mwezi mpevu, akitandaza mawingu juu yake.
10 Eine Grenze zog er über den Wassern hin, da, wo sich scheiden Licht und Finsternis.
Amechora mstari wa upeo juu ya uso wa maji, ameweka mpaka wa nuru na giza.
11 Des Himmels Säulen werden ins Wanken gebracht und entsetzen sich vor seinem Dräun.
Nguzo za mbingu nazo zatetemeka, zinatishika anapozikemea.
12 Durch seine Macht hat er das Meer erregt und durch seine Einsicht Rahab zerschmettert.
Kwa nguvu zake aliisukasuka bahari; kwa hekima yake alimkata Rahabu vipande vipande.
13 Durch seinen Hauch wird der Himmel heiter, seine Hand durchbohrte den flüchtigen Drachen.
Aliisafisha anga kwa pumzi yake; kwa mkono wake alimchoma joka aendaye mbio.
14 Und das sind nur die Säume seines Waltens - welch' leis Geflüster nur, das wir vernehmen! Doch wer erfaßt die Donnersprache seiner Allgewalt!
Haya ni mambo madogo tu katika matendo yake; tazama jinsi ulivyo mdogo mnongʼono tunaousikia kumhusu! Ni nani basi awezaye kuelewa ngurumo za nguvu zake?”

< Job 26 >