< Psalm 63 >

1 Ein Lied, von David, als er in der Wüste Juda war. Dich such ich, Gott, mein Gott; nach Dir lechzt meine Seele; nach Dir sehnt sich mein Fleisch. Wie in dem dürren, trocknen, wasserlosen Lande,
Zaburi ya Daudi. Wakati alipokuwa katika Jangwa la Yuda. Ee Mungu, wewe ni Mungu wangu, nakutafuta kwa moyo wote; nafsi yangu inakuonea kiu, mwili wangu unakuonea wewe shauku, katika nchi kame na iliyochoka mahali ambapo hapana maji.
2 so schau ich aus nach Dir, um Deine Pracht zu sehen und Deine Majestät im Heiligtum.
Nimekuona katika mahali patakatifu na kuuona uwezo wako na utukufu wako.
3 Denn köstlicher ist Deine Huld als Leben. Dich preisen meine Lippen.
Kwa sababu upendo wako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakuadhimisha.
4 So preise ich Dich lebenslang; in Deinem Namen will ich regen meine Hände.
Nitakusifu siku zote za maisha yangu, na kwa jina lako nitainua mikono yangu.
5 Gleichwie von Fett und Öl wird meine Seele satt; mit Jubellippen singt mein Mund,
Nafsi yangu itatoshelezwa kama kwa wingi wa vyakula; kwa midomo iimbayo kinywa changu kitakusifu wewe.
6 wenn ich auf meinem Lager Dein gedenke, in mitternächtiger Stunde sinne über Dich,
Kitandani mwangu ninakukumbuka wewe, ninawaza juu yako makesha yote ya usiku.
7 Du möchtest Schutz mir sein, daß ich im Schatten Deiner Flügel jauchze.
Kwa sababu wewe ndiwe msaada wangu, chini ya uvuli wa mbawa zako naimba.
8 An Dir hängt meine Seele; ich klammere mich an Deine Rechte.
Nafsi yangu inaambatana nawe, mkono wako wa kuume hunishika.
9 Die meine Seele gerne in der Wüste wüßten, sie mögen in der Erde Tiefe fahren!
Wale wanaotafuta uhai wangu wataharibiwa, watakwenda chini kwenye vilindi vya dunia.
10 Die sie dem Untergange überliefern wollen, die mögen der Schakale Beute werden!
Watatolewa wafe kwa upanga, nao watakuwa chakula cha mbweha.
11 Der König aber freue sich in Gott, und wer ihm Treue schwört, der jauchze! Der Lügner Mund wird zugestopft.
Bali mfalme atafurahi katika Mungu, wale wote waapao kwa jina la Mungu watamsifu, bali vinywa vya waongo vitanyamazishwa.

< Psalm 63 >