< Psalm 6 >
1 Auf den Siegesspender, mit Saitenspiel, ein Gesang, ein Lied, von David. Herr! Straf mich nicht in Deinem Zorn! In Deinem Grimme züchtige mich nicht!
Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Mtindo wa sheminithi. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, usinikemee katika hasira yako, wala usiniadhibu katika ghadhabu yako.
2 Herr! Sei mir gnädig! Ich vergehe, Herr! Verschone mich! Erschüttert ist mein Leib.
Unirehemu Bwana, kwa maana nimedhoofika; Ee Bwana, uniponye, kwa maana mifupa yangu ina maumivu makali.
3 Die Seele ist mir ganz verwirrt. Und Du, Herr, ach wie lange noch?
Nafsi yangu ina uchungu mwingi. Mpaka lini, Ee Bwana, mpaka lini?
4 Noch einmal rette mir du Leben, Herr! Hilf mir um Deiner Gnade willen!
Geuka Ee Bwana, unikomboe, uniokoe kwa sababu ya fadhili zako.
5 Im Tode denkt man Deiner nicht. Wer lobte Dich im Schattenreich? - (Sheol )
Hakuna mtu anayekukumbuka akiwa amekufa. Ni nani awezaye kukusifu akiwa kuzimu? (Sheol )
6 Von meinem Seufzen bin ich müde; ich bade jede Nacht mein Bett und netze meine Ruhestatt mit Tränen.
Nimechakaa kwa kulia kwa huzuni; usiku kucha nafurikisha kitanda changu kwa machozi; nimelowesha viti vyangu vya fahari kwa machozi.
7 Vor Kummer schlaflos ist mein Auge beim Blick auf alle meine Widersacher.
Macho yangu yamedhoofika kwa kuhuzunika, yamedhoofika kwa sababu ya adui zangu wote.
8 Weicht, Übeltäter all', von mir! Mein lautes Weinen hört der Herr.
Kaeni mbali nami, ninyi nyote mtendao mabaya, kwa maana Bwana amesikia kulia kwangu.
9 Mein Flehen hört der Herr; der Herr nimmt meine Bitte an.
Bwana amesikia kilio changu kwa huruma, Bwana amekubali sala yangu.
10 Beschämt, bestürzt sei'n alle meine Feinde! Zurück! In einem Augenblicke seien sie zuschanden!
Adui zangu wote wataaibika na kufadhaika, watarudi nyuma kwa aibu ya ghafula.