< Psalm 17 >
1 Ein Gebet, von David. - Gerechte Sache höre, Herr! Mein Flehen merk! Vernimm mein Beten mit den Lippen sonder Trug!
Sala ya Daudi. Sikia, Ee Bwana, kusihi kwangu kwa haki, sikiliza kilio changu. Tega sikio kwa ombi langu, halitoki kwenye midomo ya udanganyifu.
2 Nur Recht ergeht von Deinem Angesicht; untrüglich schauen Deine Augen.
Hukumu yangu na itoke kwako, macho yako na yaone yale yaliyo haki.
3 Wenn Du das Herz mir prüftest, in der Nacht es überraschtest und gründlich mich durchforschtest, fändst Du nicht, daß ich gedacht, was meinen Mund nicht überschreiten durfte.
Ingawa unauchunguza moyo wangu na kunikagua usiku, ingawa umenijaribu, hutaona chochote. Nimeamua kwamba kinywa changu hakitatenda dhambi.
4 Und bei den Löhnen für die Leute gab ich acht nach Deines Mundes Worten auf den Lebensunterhalt.
Kuhusu matendo ya wanadamu: kwa neno la midomo yako, nimejiepusha na njia za wenye jeuri.
5 Und meine Schritte hielten fest an Deinen Gleisen nicht wankten meine Tritte.
Hatua zangu zimeshikamana na njia zako; nyayo zangu hazikuteleza.
6 So rufe ich zu Dir, daß Du mich, Gott, erhörest! Neige Dein Ohr zu mir! Auf meine Rede höre!
Ee Mungu, ninakuita, kwa kuwa utanijibu, nitegee sikio lako na usikie ombi langu.
7 Erzeige Deine Wundergüte, Retter derer, die vor ihren Widersachern bei Deiner Rechten Zuflucht suchen!
Uonyeshe ajabu ya upendo wako mkuu, wewe uokoaye kwa mkono wako wa kuume wale wanaokukimbilia kutokana na adui zao.
8 Dem Augensterne gleich behüte mich! Verbirg mich in dem Schatten Deiner Flügel
Nilinde kama mboni ya jicho lako, unifiche chini ya kivuli cha mbawa zako
9 vor Frevlern, die mich überfallen, vor meinen Feinden, die mich voller Gier bedrängen!
kutokana na waovu wanaonishambulia, kutokana na adui wauaji wanaonizunguka.
10 Fühllos verschließen sie ihr Herz; im Übermute spricht ihr Mund.
Huifunga mioyo yao iliyo migumu, vinywa vyao hunena kwa majivuno.
11 Sie stürzen sich auf mich, umringen mich; zu Boden senken sie die Augen. -
Wamenifuatia nyayo zangu, sasa wamenizingira, wakiwa macho, waniangushe chini.
12 Er gleicht dem Löwen, der auf Beute lauert, dem Jungleu im Verstecke.
Wamefanana na simba mwenye njaa awindaye, kama simba mkubwa anyemeleaye mafichoni.
13 Auf, Herr! Tritt ihm entgegen! Wirf ihn nieder! Errette mich vor Bösewichten durch Dein Schwert,
Inuka, Ee Bwana, pambana nao, uwaangushe, niokoe kutokana na waovu kwa upanga wako.
14 vor Leuten, Herr, durch Deine Hand, vor Leuten, deren Teil im Leben nur die Welt, ja, durch Dein Schwert vor solchen, die ein Schlemmerleben führen, und die samt ihren Kindern voll gesättigt sind, und die, was übrigbleibt, den Enkeln hinterlassen können!
Ee Bwana, mkono wako uniokoe na watu wa jinsi hii, kutokana na watu wa ulimwengu huu ambao fungu lao liko katika maisha haya. Na wapate adhabu ya kuwatosha. Watoto wao na wapate zaidi ya hayo, hukumu na iendelee kwa watoto wa watoto wao.
15 Ich aber schaue durch Gerechtigkeit Dein Angesicht und labe mich an Deinem Anblick voll Begier.
Na mimi katika haki nitauona uso wako, niamkapo, nitaridhika kwa kuona sura yako.