< Psalm 148 >
1 Alleluja! Lobpreist den Herrn im Himmel! Lobpreist ihn in den Höhen!
Msifuni Yahwe. Msifuni Yahwe, ninyi mlio katika mbingu; msifuni yeye, ninyi mlio juu.
2 Lobpreist ihn, alle seine Engel! Lobpreist ihn, alle seine Scharen!
Msifuni yeye, enyi malaika wake wote; msifuni yeye, majeshi ya malaika wake wote.
3 Lobpreiset ihn, du Sonne und du Mond! Lobpreist ihn, all ihr hellen Sterne!
Msifuni yeye, enyi jua na mwezi; msifuni yeye, nyota zote zing'aazo.
4 Du höchster Himmel, preise ihn und ihr Gewässer überm Himmel!
Msifuni yeye, enyi mbingu zilizo juu zaidi na maji yaliyo juu ya anga.
5 Des Herren Namen sollen sie lobpreisen! Denn er gebot; da waren sie geschaffen.
Na vilisifu jina la Yahwe, maana aliamuru, navyo vikaumbwa.
6 Er läßt sie stehn für alle Zeiten und macht es zum Gesetz, das nimmer kraftlos wird.
Pia ameviimrisha milele na milele; naye alitoa amri ambayo haitabadilika.
7 Lobpreist den Herrn, die ihr auf Erden weilet, ihr Meerestiere, all ihr Meeresfluten!
Msifuni yeye kutoka nchi, ninyi viumbe wa baharini na viumbe vyote katika kina cha bahari,
8 Du Feuer, Hagel, Schnee und Sturmgewölk, du Sturmwind, seines Winks gewärtig.
moto na mvua ya mawe, theluji na mawingu, upepo wa dhoruba ukitimiza neno lake.
9 Ihr Bergeshöhen, all ihr Hügel, ihr Fruchtbäume, ihr Zedern all!
Msifuni yeye, enyi milima na vilima, miti ya matunda na mierezi yote,
10 Du Wild und all ihr zahmen Tiere, Gewürm und ihr beschwingten Vögel!
wanyama pori na wanyama wafugwao, viumbe vitambaavyo na ndege.
11 Ihr Erdenkönige, ihr Völker all, ihr Fürsten alle und ihr Erdenrichter!
Msifuni Yahwe, wafalme wa nchi na mataifa yote, wakuu na watawala wote wa nchi,
12 Ihr Jünglinge, ihr Jungfrauen, ihr Greise und ihr Jungen!
wote vijana wa kiume na vijana wa kike, wazee na watoto.
13 Lobpreisen sollen sie des Herren Namen! Denn hoch erhaben ist allein sein Name, und seine Herrscherwürde ist erhaben über Erd und Himmel.
Na walisifu jina la Yahwe, kwa kuwa jina lake pekee limetukuka na utukufu wake umeongezwa juu ya nchi na mbingu.
14 Und seinem Volk verleiht er große Macht. Lobpreisen dürfen ihn all seine Frommen, die Kinder Israels, das Volk, das ihm so nahe steht. Alleluja!
Naye ameyainua mapembe ya watu wake kwa ajili ya sifa kutoka kwa waaminifu wake wote, Waisraeli, watu wa karibu naye. Msifuni Yahwe.