< Psalm 132 >

1 Ein Stufenlied. - Sei, Herr, zugunsten Davids eingedenk all dessen, was er gesprochen,
Wimbo wa kwenda juu. Ee Bwana, mkumbuke Daudi na taabu zote alizozistahimili.
2 wie er dem Herrn geschworen, dem Starken Jakobs hat gelobt:
Aliapa kiapo kwa Bwana na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:
3 "Ich gehe nimmer in mein Wohngezelt, besteige nicht mein Ruhebett,
“Sitaingia nyumbani mwangu au kwenda kitandani mwangu:
4 Versage meinen Augen Schlaf und Schlummer meinen Augenwimpern,
sitaruhusu usingizi katika macho yangu, wala kope zangu kusinzia,
5 bis daß ich eine Stätte finde für den Herrn, für Jakobs Starken eine Wohnung." -
mpaka nitakapompatia Bwana mahali, makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
6 Nun hörten wir davon zu Ephrat und fanden sie im Waldgefilde.
Tulisikia habari hii huko Efrathi, tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara:
7 "Zu seiner Wohnung laßt uns gehen, vor seiner Füße Schemel niederfallen!"
“Twendeni kwenye makao yake, na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;
8 Auf, Herr, zu Deiner Ruhestätte, Du und die Lade Deiner Herrscherwürde!
inuka, Ee Bwana, uje mahali pako pa kupumzikia, wewe na Sanduku la nguvu zako.
9 Mit Heil laß Deine Priester sich bekleiden, und Deine Frommen mögen jubeln! -
Makuhani wako na wavikwe haki, watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”
10 Um David, Deines Dieners willen, weis nicht zurück, den Du gesalbt!"
Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako, usimkatae mpakwa mafuta wako.
11 Der Herr schwur David Dauer zu. Er geht davon nicht ab. "Auf deinen Thron erheb ich einen von deiner Leibesfrucht.
Bwana alimwapia Daudi kiapo, kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua: “Nitamweka mmoja wa wazao wako mwenyewe katika kiti chako cha enzi,
12 Bewahren deine Söhne meinen Bund und meine Zeugnisse, wie ich sie lehre, dann dürfen ihre Söhne allezeit auf deinem Throne sitzen!" -
kama wanao watashika Agano langu na sheria ninazowafundisha, ndipo wana wao watarithi kiti chako cha enzi milele na milele.”
13 Der Herr hat Sion sich erkoren, zum Wohnsitz sich ersehen:
Kwa maana Bwana ameichagua Sayuni, amepaonea shauku pawe maskani yake:
14 "Das sei in Ewigkeit mein Ruhesitz, ich throne hier; denn hier gefällt es mir.
“Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele; hapa ndipo nitakapoketi nikitawala, kwa sababu nimepaonea shauku:
15 Ich segne seine Jugend und gebe seinen Armen Brot in Fülle.
Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele: nitashibisha maskini wake kwa chakula.
16 Mit Heil bekleid ich seine Priester, und frohe Lust sei seiner Frommen Teil!
Nitawavika makuhani wake wokovu, nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.
17 Ich lasse Davids Macht ersprossen, dem richt ich eine Leuchte her, den ich gesalbt.
“Hapa nitamchipushia Daudi pembe, na kuweka taa kwa ajili ya masiya wangu.
18 In Schande hüll ich seine Feinde, dieweil auf ihm ein Diadem erglänzt."
Adui zake nitawavika aibu, bali taji kichwani pake itangʼaa sana.”

< Psalm 132 >