< Psalm 107 >

1 "Dem Herrn sagt Dank! Denn er ist gut. Auf ewig währet seine Huld."
Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
2 So singen die vom Herrn Erlösten, die er aus Feindes Hand befreit
Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
3 und aus den Ländern sammelt von Morgen, Abend, Mitternacht und Süden. -
wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
4 Sie irren in der Steppenwüste und finden keine Bahn zur Wohnstatt hin.
Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
5 Sie leiden Durst und Hunger, und ihre Seele sinkt darob in Ohnmacht.
Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
6 Sie schreien zu dem Herrn in ihrer Not; Er rettet sie aus ihren Ängsten
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
7 und leitet sie auf rechtem Wege, die Wohnstatt zu erreichen.
Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
8 Sie sollen dankbar sein dem Herrn für seine Gnade, für seine Wunder an den Menschenkindern,
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
9 daß er ihr Lechzen stillt und ihren Hunger mit dem Nötigen befriedigt! -
kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
10 In Finsternis und Todesschatten sitzen sie, gebannt in Elend und in Eisen;
Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
11 denn Gottes Worten widerspenstig, verschmähen sie des Höchsten Rat.
kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
12 Durch Mühsal beugt er ihren Sinn; sie werden machtlos; niemand hilft.
Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
13 Sie schrein zum Herrn in ihrer Not; er rettet sie aus ihren Ängsten.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
14 Aus Finsternis und Todesschatten führt er sie, und ihre Fesseln sprengt er auf.
Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
15 Sie sollen dankbar sein dem Herrn für seine Gnade, für seine Wunder an den Menschenkindern,
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
16 daß er zertrümmert eherne Pforten und Eisenriegel bricht! -
kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
17 Die Kranken leiden schwer ob ihres Sündenwandels und wegen ihrer Missetaten,
Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
18 daß sie vor jeder Speise ekelt und sie des Todes Pforten schon berühren.
Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
19 Sie schreien zu dem Herrn in ihrer Not; er rettet sie aus ihren Ängsten.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
20 Er schickt sein Wort, macht sie gesund und rettet sie vor ihren Grüften.
Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
21 Sie sollen dankbar sein dem Herrn für seine Gnade, für seine Wunder an den Menschenkindern,
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
22 ihm Dankesopfer bringen, jubelnd seine Taten künden! -
Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
23 Die auf der See in Schiffen fahren und ihr Geschäft auf großen Wassern treiben,
Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
24 erblicken hier des Herren Werke und seine Wunder mit der tiefen Flut.
Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
25 Ein Sturm erhebt sich auf sein Wort, und seine Wellen türmen sich.
Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
26 Sie steigen bis zum Himmel, fahren in die Tiefen. Ihr Leben ist gefährdet.
Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
27 Sie tanzen, schwanken wie Betrunkene. Dahin ist ihre ganze Kunst.
Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
28 Sie schrein zum Herrn in ihrer Not; er rettet sie aus ihren Ängsten.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
29 Er macht den Sturm zum Säuselwind; da legen sich des Meeres Wellen.
Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
30 Sie jubeln, daß sie stille liegen und er sie an ihr Endziel führt.
Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
31 Sie sollen dankbar sein dem Herrn für seine Gnade, für seine Wunder an den Menschenkindern
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
32 und ihn vor allem Volk erheben und ihn im Kreis der Alten loben! -
Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
33 Er macht zur Wüste Ströme, zu dürrem Lande Quellenorte,
Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
34 ein fruchtbar Land zum salzigen Grund, der Bosheit der Bewohner wegen.
nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
35 Er macht zum Wasserteich die Wüste und dürres Land zum Quellenort;
Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
36 die Hungrigen läßt er hier wohnen; Sie bauen eine Wohnstatt dort,
aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
37 besäen Felder, pflanzen Weinberge, die lohnend Früchte tragen.
Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
38 Er segnet sie, daß sie sich riesig mehren, und läßt ihr Vieh sich nicht vermindern.
Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
39 Vermindern sie sich, werden sie gebeugt von Druck und Elend und von Jammer,
Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
40 dann gießt auf Fürsten er Verachtung aus und führt sie in die unwegsame Öde.
Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
41 Doch aus dem Elend hebt er Arme auf und macht Geschlechter Herden gleich.
Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
42 Das sehen Redliche und freuen sich, und jeder Frevelmund verstummt. -
Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
43 Wer weise ist, beachtet dies, und Anerkennung finden so des Herren Gnadentaten.
Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.

< Psalm 107 >