< Sprueche 7 >

1 Mein Sohn, behalte meine Reden! Bei dir verwahr, was ich dich heiße!
Mwanangu, yatunze maneno yangu na ndani yako udhihifadhi amri zangu.
2 Bewahr dir meine Vorschriften, so wirst du leben, und meine Weisung wie den Augapfel!
Uzilinde amri zangu ili uishi na uyatunzetu mafundisho yangu kama mboni ya jicho.
3 Bind sie an deine Finger! Auf deines Herzens Tafel schreibe sie!
Uyafunge katika vidole vyako; uyaandike katika kibao cha moyo wako.
4 Zur Weisheit sprich: "Du bist mir Schwester", nenn Einsicht deine Freundin,
Mwambie hekima, “wewe ni dada yangu,” na ufahamu mwite jamaa yako,
5 auf daß sie dich vor einem andere Weib bewahre, vor einer Fremden, die einschmeichelnd redet!
ili ujitunze mwenyewe dhidi ya mwanake haramu, dhidi ya mwanamke mgeni mwenye maneno laini.
6 Durchs Fenster meines Hauses, durchs Gitter schaute ich hinaus.
Nilikuwa naangalia kwenye wavu wa dirisha la nyumba yangu.
7 Da sah ich einen Jüngling bei den noch Unerfahrenen, bemerkte bei den jungen Leuten einen Unvorsichtigen,
Nikawatazama watu mwenye ukosefu wa uzoefu, na miongoni mwa watu vijana nikamwona kijana asiye na akili.
8 der auf der Gasse nahe einer Ecke ging und in der Richtung meines Hauses schritt
Kijana huyo alishuka mtaani kwenye kona karibu na yule mwanamke, akaenda kwenye nyumba yake.
9 in Dämmerung, am Abende des Tags, in stiller Nachtzeit, in der Dunkelheit.
Ilikuwa katika utusiutusi wa siku muda wa jioni, wakati wa usiku na giza.
10 Da tritt auf einmal ihm das Weib entgegen im Dirnenanzug mit geschnürter Brust.
Akakutana na yule mwanake, amevaa kama kahaba, katika moyo wa udanyanyifu.
11 Unruhig trieb sie sich herum; zu Hause hatten ihre Füße keine Ruhe.
Alikuwa na kelele na upotovu; miguu yake haikutulia kwenye masikani.
12 Ein Schritt jetzt auf die Straße und auf den Markt ein Schritt; sie lauerte an jeder Ecke.
Alielekea mitaani, kisha sehemu ya sokoni, na katika kila upande alisubiri kwa kuviza.
13 Jetzt hascht sie ihn, küßt ihn; mit frecher Miene redet sie ihn an:
Basi akamshika na kumbusu, kwa uso wa nguvu akamwambia,
14 "Schlachtopfer darzubringen, lag mir ob; ich habe heute mein Gelübde nun entrichtet.
leo nimetoa sadaka yangu ya amani, nimelipa nadhili yangu,
15 Deswegen bin ich ausgegangen, um dich zu suchen. Ich habe dich gefunden.
hivyo nilikuja kukutana nawe, kuutafuta uso wako kwa hamu, na sasa nimekupata.
16 Mit Decken habe ich bedeckt mein Lager, mit buntem Linnen aus Ägypten.
Nimeweka matandiko juu ya kitanda changu, kitani za rangi kutoka Misri.
17 Mit Myrrhen habe ich besprengt mein Lager, mit Aloë und Zimtgewürz.
Kitanda changu nimenyunyizia manemane, udi na mdalasini.
18 So komm! Wir wollen bis zum Morgen an der Liebe uns berauschen, in Liebe uns genießen.
Njoo, tunywe tujishibishe kwa upendo wetu hata asubuhi; tupate furaha kuu kwa matendo ya mahaba.
19 Der Mann ist nicht daheim; er zog auf Reisen in die Ferne.
Maana mume wangu hayupo nyumbani kwake; amekwenda safari ya mbali.
20 Er nahm den Beutel samt dem Gelde mit sich; am Vollmondstag erst kehrt er wieder heim."
Alichukua mkoba wa fedha; atarudi siku ya mwezi mpevu.
21 So bringt sie ihn herum durch ihr verführerisches Reden und reißt ihn fort durch ihre glatten Lippen.
katika maneno yake mengi akamshinda; na kwa midomo yake laini anampotosha.
22 Er folgt ihr nach, der Harmlose, gleich einem Stier, den man zur Schlachtbank führt, gleich einem Hund zum Stricke,
Ghafula alimfuata kama maksai anayekwenda kwa mchinjaji, kama ayala aliyekamatwa kwa nguvu,
23 gleich einem Hirsch dahin, wo ihm ein Pfeil die Leber spaltet, gleich einem Vogel, der zur Schlinge eilt, und merkt es nicht, daß es sein Leben gilt.
mpaka mshale upasue ini lake. Alikuwa kama ndege anayekimbili kwenye mtego. Hakujua kuwa itamgharimu maisha yake.
24 Nun, Söhne, horcht auf mich! Auf meines Mundes Reden merket!
Na sasa, wanangu, nisikilizeni; zingatieni maneno ya kinywa changu.
25 Laß nicht dein Herz zu ihren Wegen biegen! Verirr dich nicht auf ihre Steige!
Moyo wako usiyageukie mapito yake; usipotoshwe katika mapito yake.
26 Denn viel sind der Erschlagenen, die sie gefällt, und viele sind's, die sie gemordet.
Amesababisha watu wengi kuanguka kwa kuwajeruhi; ameua watu wengi.
27 Die Wege, die zu ihrem Hause führen, sind Wege zu der Unterwelt. Sie führen zu des Todes Kammern. (Sheol h7585)
Nyumba yake ipo juu ya barabara ya kwenda kuzimu; huelekea chini kwenye vyumba vya mauti. (Sheol h7585)

< Sprueche 7 >