< Sprueche 18 >

1 Den Eigenwillen sucht, wer sich absondert; bei jeglicher Gelegenheit beginnt er Streit.
Yule ambaye hujitenga hutafuta matakwa yake mwenyewe na hupingana na hukumu zote za kweli.
2 Der Tor hat kein Gefallen an Belehrung; er möchte nur die eigene Meinung künden.
Mpumbavu hapati raha katika ufahamu, lakini hufunua kile kilichopo katika moyo wake.
3 Wo Frevel auftritt, dort tritt auch Verachtung auf, und Schmähung ist mit Hohn vereint.
Mtu mwovu anapokuja, dharau huja pamoja naye- sambamba na aibu na shutuma.
4 Aus eines Mannes Munde tiefe Worte sind Gewässer, ein Strom, der aus dem Born der Weisheit sprudelt.
Maneno ya kinywa cha mtu ni maji yenye kina kirefu; chemchemi ya hekima ni mkondo unaotiririka.
5 Daß man Partei für einen Frevler nimmt, daß man das Recht des Frommen beugt, nützt nichts.
Si vema kuwa na upendeleo kwa mwovu, wala haifai kukana haki kwa wale watendao mema.
6 Des Toren Lippen schaffen Streit; nach Schlägen ruft sein Mund.
Midomo ya mpumbavu huletea mafarakano na kinywa chake hukaribisha mapigo.
7 Des Toren Mund führt seinen Sturz herbei, und seine Lippen sind ein Strick für seinen Hals.
Kinywa cha mpumbavu ni uharibifu wake na hujinasa mwenye kwa midomo yake.
8 Des Ohrenbläsers Worte sind wie Hammerschläge; sie dringen tief ins Herz hinein.
Maneno ya mmbea ni kama chembe tamu na hushuka katika sehema za ndani sana kwenye mwili.
9 Wer lässig bei der Arbeit ist und wer den eigenen Besitz zerstört, sind Brüder.
Basi, ambaye ni mzembe katika kazi yake ni ndugu yake anayeharibu wengi.
10 Ein fester Turm des Herren Name; der Fromme läuft zu ihm und ist gesichert.
Jina la Yehova ni mnara imara; atendaye haki hukimbilia na kuwa salama.
11 Des Reichen Habe ist ihm eine feste Stadt, wie eine hohe Mauer um ihn her.
Mali ya tajiri ni mji wake imara na katika fikira zake ni kama ukuta mrefu.
12 Stolz geht dem Sturz voran, der Ehre Demut.
Moyo wa mtu huwa na kiburi kabla ya anguko lake, bali unyenyekevu hutangulia kabla ya heshima.
13 Gibt jemand Antwort schon, bevor er recht verstanden, so rechnet man es ihm als Torheit und als Schande.
Anayejibu kabla ya kusikiliza- ni upuuzi na aibu yake.
14 Ein männliches Gemüt kann seine Leiden meistern. Ein düsteres Gemüt, wer mag's erträglich finden?
Roho ya mtu itajinusuru na madhara, bali roho iliyopondeka nani anaweza kuivumilia?
15 Des Klugen Herz erwirbt sich Einsicht; Einsicht sucht auch des Weisen Ohr.
Moyo wa mwenye akili hujipatia maarifa na usikivu wa mwenye busara huitafuta.
16 Geschenke schaffen ihrem Geber Raum und öffnen ihm den Zutritt zu den Großen.
Zawadi ya mtu inaweza kufungua njia na kumleta mbele ya mtu muhimu.
17 In einem Streite hat der erste Recht; da kommt der andere und untersucht's aufs neue.
Wa kwanza kujitetea katika shitaka lake huonekana kuwa na haki hadi mpinzani wake aje na kumuuliza maswali.
18 Den Streitigkeiten macht das Los ein Ende; es trennt die Streitenden.
Kupiga kura kunamaliza mabishano na kuwatawanya wapinzani imara.
19 Ein Bruder kann an einer Festung sich vergehen, sind Streitigkeiten doch, was eine Bresche für die Burg.
Ndugu aliyechukizwa ni mgumu kushawishiwa kuliko mji wenye nguvu, na kugombana ni kama makomeo ya ngome.
20 Mit seines Mundes Frucht ersättigt jeder seinen Magen, von seiner Lippen Ernte kann er satt sich essen.
Tumbo la mtu litashiba kutoka kwenye tunda la kinywa chake; atatoshelezwa kwa mavuno ya midomo yake.
21 In dem Bereich der Zunge liegen Tod und Leben, und wer sie gern gebraucht, genießt auch ihre Frucht.
Uzima na kifo hutawaliwa kwa ulimi, na wale wenye kuupenda ulimi watakula tunda lake.
22 Wer je das Weib erforscht, hat einen guten Fund getan, und er erfreut sich der besonderen Huld des Herrn.
Yeye apataye mke anapata kitu chema na kupokea fadhila kutoka kwa Yehova.
23 Der Arme redet weinerlich; der Reiche aber spricht mit Nachdruck.
Mtu masikini huomba rehema, lakini mtu tajiri hujibu kwa ukali.
24 Gefährten gibt's, die gegenseitig sich zugrunde richten; und Freunde gibt's, anhänglicher als Brüder.
Anayejidai kwa marafiki wengi watamleta katika uharibifu, bali yupo rafiki ambaye huwa karibu kuliko ndugu.

< Sprueche 18 >