< 4 Mose 33 >

1 Dies sind der Israeliten Züge, auf denen sie aus Ägypterland nach ihren Scharen unter Mosis und Aarons Führung gezogen sind.
Hizi ndizo safari za wana wa Israeli hapo walipotoka katika nchi ya Misri pamoja na makundi yao ya kijeshi chini ya uongozi wa Musa na Haruni.
2 Moses schrieb ihre Ausfahrten zu ihren Zügen nieder auf des Herrn Befehl. Dies sind ihre Züge zu ihren Ausfahrten:
Musa aliandika maeneo yote tangu walipoondoka mpaka walipofika, kama alivyoamuriwa na BWANA. Hizi ndizo safari zao kama kutoka kwao kulivyokuwa kwa kila walipotoka.
3 Sie zogen von Ramses weg am fünfzehnten Tage des ersten Monats. Am Tage nach dem Passah zogen die Israeliten aus, in dichter Schar vor ganz Ägyptens Augen,
Mwezi wa kwanza walisafiri kutoka Ramesi, waliondoka siku ya kumi na tano. Asubuhi siku iliyofuata baada ya Pasaka, Wana wa Israeli waliondoka wazi wazi, mbele ya machoya Wamisri wote.
4 während die Ägypter verkündeten, daß der Herr bei ihnen jede Erstgeburt erschlagen und daß der Herr an ihren Göttern Strafgerichte vollzogen habe.
Hii ilitokea wakati Wamisiri walipokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza, ambao BWANA alikuwa amewaua miongoni mwao, kwa kuwa pia alikuwa ameiadhibu miungu yao.
5 Die Israeliten zogen nun von Ramses fort und lagerten in Sukkot.
Wana wa Israeli walisafiri kutoka Ramesi na kuweka kambi
6 Von Sukkot zogen sie fort und lagerten in Etam am Rande der Steppe.
Sukothi. Walisafiri toka Sukothi na kuweka kambi Ethamu, mwisho wa nyika.
7 Von Etam zogen sie fort und wandten sich nach Pihachirot vor Baalsephon und lagerten vor Migdol.
Wakasafiri kutoka Ethamu wakarudi mpaka Pi-Hahirothi, ambayo inaikabili Baali Zephoni, ambapo waliweka kambi kuikabili Migidoli
8 Sie zogen von Pihachirot fort und schritten mitten durch das Meer in die Wüste. Sie wanderten drei Tagereisen und lagerten in Mara.
Kisha wakasafiri toka mkabala wa Pi-Hairothi na kupita katikati ya bahari kuelekea nyikani. Wakasafiri safari ya siku tatu katika nyika ya Ethamu na kuweka kambi Mara.
9 Sie zogen von Mara fort und kamen nach Elim. In Elim waren zwölf Quellen und siebzig Palmbäume, und sie lagerten dort.
Wakasafiri kutoka Mara kufika Elimu. Pale Elimu kulikuwa na chemichemi kumi na mbili za maji na miti sabini ya mitende. hapo ndipo walipoweka kambi.
10 Sie zogen von Elim fort und lagerten am Schilfmeer.
Walisafiri kutoka Elimu na kuweka kambi karibu na Bahari ya Shamu.
11 Sie zogen vom Schilfmeer fort und lagerten in der Wüste Sin.
Walisafiri kutoka Bahari ya Shamu na kuweka kambi katika nyika ya Sini.
12 Von der Wüste Sin zogen sie fort und lagerten in Dophka.
Walisafiri kutoka nyika ya Sini na kuweka kambi Dofka.
13 Sie zogen von Dophka fort und lagerten in Alus.
Wakasafiri kutoka Dofka na kuweka kambi Alushi.
14 Von Alus zogen sie fort und lagerten in Raphidim. Da war kein Wasser für das Volk zum Trinken.
Wakasafiri kutoka Alushi na kuweka kambi Refidimu, ambapo watu walikosa maji ya kunywa.
15 Von Raphidim zogen sie fort und lagerten in der Wüste Sinai.
Walisafiri kutoka Refidimu na kuweka kambi kwenye nyika ya Sinai.
16 Von der Wüste Sinai zogen sie fort und lagerten bei den Gelüstegräbern.
Walisafiri kutoka nyika ya Sinai na kuweka kambi Kibrothi Hataava.
17 Von den Gelüstegräbern zogen sie nach Chaserot,
Walisafiri kutoka Kibrothi Hataava na kuweka kambi Hazerothi.
18 von Chaserot nach Ritma,
Walisafiri kutoka Hazerothi na kuweka kambi Rithima.
19 von Ritma nach Rimmon Peres,
Walisafiri kutoka Rithima na kuweka kambi Rimoni Perezi.
20 von Rimmon Peres nach Libna,
Walisafiri kutoka Rimoni Perezi na kuweka kambi Libna.
21 von Libna nach Rissa,
Walisafiri kutoka Libna na kuweka kambi Risa.
22 von Rissa nach Kehela,
Walisafiri kutoka Risa na kuweka kambi Kehelatha.
23 von Kehela zum Berge Sepher,
Walisafiri kutoka Kehelatha na kuweka kambi kwenye Mlima Sheferi.
24 vom Berge Sepher nach Charada,
Walisafiri kutoka Mlima Sheferi na kuweka kambi Harada.
25 von Charada nach Makhelot,
Walisafiri kutoka Harada na kuweka kambi Makelothi.
26 von Makhelot nach Tachat,
Walisafiri kutoka Makelothi na kuweka kambi Tahathi.
27 von Tachat nach Tarach,
Walisafiri kutoka Ttahalathi na kuweka kambi Tera.
28 von Tarach nach Mitka,
Walisafiri kutokaTera na kuweka kambi Mithika.
29 von Mitka nach Chasmon,
Walisafiri kutoka Mithika na kuweka kambi Hashimona.
30 von Chasmon nach Moserot,
Walisafiri kutoka Hashimona na kuweka kambi Moserothi.
31 von Moserot nach Bene Jaakan,
Walisafiri kutoka Moserothi na kuweka kambi Bene Jaakani.
32 von Bene Jaakan nach Chor Hagidgad,
Walisafiri kutoka Bene Jaakani na kuweka kambi Hori Hagidigadi.
33 von Chor Hagidgad nach Jotba,
Walisafiri kutoka Hori Hagidigadi na kuweka kambi Jotibatha.
34 von Jotba nach Abron,
Walisafiri kutoka Jotibatha na kuweka kambi Abrona.
35 von Abron nach Esiongeber,
Walisafiri kutoka Abrona na kuweka kambi Ezioni Geberi.
36 von Esiongeber in die Wüste Sin, das ist Kades,
Walisafiri toka Ezioini Geberi na kuweka kambi katika nyika ya Sini kule Kadeshi.
37 von Kades zum Berge Hor an der Grenze des Landes Edom.
Walisafiri kutoka Kadeshi na kuweka kambi Mlima Hori, Pembezoni mwa nchi ya Edomu.
38 Und der Priester Aaron stieg auf den Berg Hor nach des Herrn Befehl und starb hier, im vierzigsten Jahre nach dem Auszug der Israeliten aus Ägypterland, am ersten des fünften Monats.
Hapo ndipo Haruni kuhani alipoenda kwenye Mlima Hori kwa amri ya BWANA na kufa kule mwaka wa arobaini bada ya Wisraeli kutoka katika nchi ya Misri, katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano.
39 Aaron aber war 123 Jahre alt, als er auf dem Berge Hor starb.
Haruni alikuwa na umri wa mika 123 alipokufa pale juu ya Mlima Hori.
40 Da hörte der Kanaaniter, Arads König, der im Süden des Landes Kanaan saß, vom Anmarsch der Israeliten.
Wakanaani, mfalme wa Aradi, ambao waliishi kusini mwa nyika katika nchi ya Kanaani, walisikia juu ya ujio wa wana wa Israeli.
41 Sie zogen dann vom Berge Hor fort und lagerten in Salmon.
Walisafiri kutika Mlima Hori n a kuweka kambi Zalimona.
42 Von Salmon ging es nach Punon,
Walisafiri kutoka Zalimona na kuweka kambi Punoni.
43 Von Punon nach Obot,
Walisafiri kutoka Punoni na kuweka kambi Obothi.
44 Von Obot nach Ijje Haabarim im Gebiete Moabs,
Walisafiri kutoka Obothi na kuweka kambi Abarimu, katika mpaka wa Moabu.
45 von Ijjim nach Dibon Gad,
Walisafiri kutoka Abarimu na kuweka kambi Diboni Gadi.
46 von Dibon Gad nach Almon Diblataim,
Walisafiri kutoka Diboni Gadi na kuweka kambi Alimoni Diblathaimu.
47 von Almon Diblataim zum Ufergebirge von Nebo.
Walisafiri kutoka Alimoni Diblathaimu na kuweka kambi kwenye milima ya Abarimu mkabala na Nebo.
48 Vom Ufergebirge zogen sie fort und lagerten in den Steppen Moabs am Jordan bei Jericho,
Walisafiri kutoka mlima wa Abarimuna kuweka kambi kwenye nyanda za Moabu karibu na Yorodani huko Yeriko.
49 und zwar lagerten sie am Jordan von Bet Hajesimot bis Abel Hasittim in Moabs Steppen.
Waliweka kambi karibu na Yorodani, kutoka Bethi Jeshimothi mpaka Abeli Shitimu katika nyanda za Moabu.
50 Und der Herr sprach zu Moses in Moabs Steppen am Jordan bei Jericho:
Hapo BWANA alinenana Musa katika nyanda za Moabu karibu na Yorodani kule Yeriko akasema,
51 "Rede mit den Söhnen Israels und sprich zu ihnen: 'Zieht ihr über den Jordan ins Land Kanaan,
“Nena na wana wa Israeli uwaambie. 'Mtakapovuka mto Yorodani kuingia Kanaani,
52 dann müßt ihr alle Insassen des Landes vor euch vertilgen und alle ihre Bilder vernichten. Auch alle ihre Gußbilder sollt ihr vernichten und alle ihre Höhen verwüsten!
ndipo mtakapowafukuza wenyeji wote mbele yenu. Mtaziharibu sanamu zote za kuchongwa. Mtaziharibu sanamu zao za kusubu na kuharibu mahali pao pote palipoinuka.
53 Vom Lande ergreift Besitz und siedelt darin! Denn euch gebe ich das Land zum Besitz.
Mtachukua hiyo ardhi iwe mali yenu na muishi ndani yake, kwa sababu nimewapeni hiyo nchi iwe mali yenu.
54 Verteilt das Land nach euren Stämmen durch das Los! Dem, der viel zählt, sollt ihr seinen Besitz vermehren und dem, der wenig zählt, einen kleineren geben! Was jemandem durchs Los zufällt, soll ihm gehören! Nach euren väterlichen Stämmen sollt ihr es verteilen!
Mtairithi hiyo nchi kwa kupiga kura, kwa kufuata kila ukoo. Kwa zile koo kubwa kubwa mtawapa sehemu kubwa ya ardhi, na kwa zile koo ndogo ndogo mtawapa sehemu ndogo ya ardhi. Kura itakapoanguka kwenye kila ukoo, hiyo ardhi itakuwa mali yake. Mtairithi ardhi kufuata ukoo wa kabilla la jamaa zenu.
55 Vertreibt ihr aber nicht vor euch des Landes Insassen, dann werde, was ihr davon übriglaßt, euch zu Dornen in den Augen und zu Stacheln in den Seiten! Sie sollen euch bedrängen in eurem Lande, in dem ihr siedelt!
Lakini kama hamtawafukuza wenyeji wa nchi hiyo watoke mbele yenu, ndipo wale watu mtakaowaruhusu wakae nanyi watakapokuwa kama sindano machoni mwenu na miiba katika mbavu zenu. Watayafanya maisha yenu yawe magumu katika nchi mnayoishi.
56 Dann tue ich mit euch, was ich jenen zugedacht.'"
Ndipo itakapotokea kuwa kile ambacho Mimi ninakusudia kufanya kwa wale watu, Nitawafanyia pia ninyi'”

< 4 Mose 33 >