< Job 36 >
1 Elihu fuhr nun weiter fort:
Elihu akaendelea kusema:
2 "Ein wenig warte noch, daß ich dich unterweise! Denn noch spricht manches auch für Gott.
“Nivumilie kidogo zaidi nami nitakuonyesha kwamba yako mengi zaidi ya kusemwa kwa ajili ya Mungu.
3 Ich muß nur meinen Vortrag weiter ausdehnen; doch werde ich mein Tun rechtfertigen.
Ninayapata maarifa yangu kutoka mbali, nami nitamhesabia haki Muumba wangu.
4 Denn nimmer sollen meine Worte dich enttäuschen, die ich an dich, Rechthaber, richte.
Uwe na hakika kwamba maneno yangu si ya uongo; mmoja aliye mkamilifu katika maarifa yuko pamoja na wewe.
5 Sieh, Gott ist fest und widerspricht sich nicht; er ist durchaus von festem Sinn.
“Mungu ni mwenye nguvu, lakini hamdharau mwanadamu; ni mwenye nguvu, naye ni thabiti katika shauri lake.
6 Er schenkt dem Frevler nicht das Leben; dem Armen aber gibt er Recht.
Hawaachi waovu waendelee kuishi, bali huwapa walioteswa haki yao.
7 Von Frommen zieht er nicht die Augen ab; sogar mit Königen läßt er auf dem Thron sie sitzen, in Pracht und Herrlichkeit, und werden sie dann stolz,
Yeye haondoi macho yake kwa wenye haki; huwaketisha penye viti vya enzi pamoja na wafalme na kuwatukuza milele.
8 so legt man sie in Ketten, und sie werden so gefesselt in des Elends Stricken.
Lakini ikiwa watu wamefungwa kwenye minyororo, wakiwa wameshikiliwa na kamba za mateso,
9 Dann hält er ihnen vor ihr Treiben, ihre Sünden, daß sie stolz geworden.
huwaonyesha yale waliyoyatenda, kwamba wametenda dhambi kwa majivuno.
10 Und so tut er ihr Ohr der Warnung auf und heißt sie umkehren von Sünden.
Huwafanya wao kusikia maonyo, na huwaagiza kutubu uovu wao.
11 Gehorchen sie in Unterwürfigkeit, dann fließen ihre Tage in Glückseligkeit, in Wonne ihre Jahre hin.
Kama wakitii na kumtumikia, wataishi siku zao zilizobaki katika mafanikio, na miaka yao katika utoshelevu.
12 Doch wenn sie nicht gehorchen, rennen sie ins Dunkle und sie sterben in Verblendung.
Lakini wasiposikiliza, wataangamia kwa upanga, nao watakufa pasipo maarifa.
13 Ruchlose Leute aber wecken Zorn und rufen nicht um Hilfe, wenn er sie fesselt.
“Wasiomcha Mungu moyoni mwao huficha chuki; hata anapowafunga, hawamwombi msaada.
14 Hin stirbt so in der Jugendfrische ihre Seele, ihr Leben in der Vollkraft.
Wanakufa wangali vijana, miongoni mwa wanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
15 In seinem Elend rettet er den Armen, dieweil er in der Not ihr Ohr eröffnet.
Bali wao wanaoteseka huwaokoa katika mateso yao, na kuzungumza nao katika dhiki zao.
16 Er lockt auch dich aus der Bedrängnis Rachen. An ihre Stelle träte Freiheit, unbeengt, und deines Tisches Schüssel würde voll von Fett.
“Yeye anakubembeleza utoke katika mataya ya dhiki, ili kukuweka mahali palipo na nafasi mbali na kizuizi, hadi kwenye meza yako ya faraja iliyojaa vyakula vizuri.
17 Bist du von frevelhaftem Urteil aber voll, dann trifft auch dich gerechtes Urteil.
Lakini sasa umelemewa na hukumu kwa ajili ya uovu; hukumu na haki vimekukamata.
18 Denn Zorn verführe dich nicht zu dem Übermaße, der Streit um Lösung soll dich nicht verleiten.
Uwe mwangalifu ili yeyote asikushawishi kwa utajiri; usipotoshwe kwa fungu kubwa la rushwa.
19 Wird's dein Geschrei in Ordnung bringen? Unnötig sind ja all die Kraftanstrengungen.
Je, utajiri wako hata nguvu zako nyingi vinaweza kukusaidia usiingie kwenye dhiki?
20 Nicht wünsche dir die Nacht herbei! An ihre Stelle treten Unruhen.
Usiutamani usiku uje, ili uwaburute watu mbali na nyumba zao.
21 Nimm dich in acht und kehre nimmer dich dem Frevel zu! Du hast dazu mehr Lust als zu dem Leiden.
Jihadhari usigeukie uovu, ambao unaupenda zaidi kuliko mateso.
22 Sieh, Gott ist groß in seiner Macht. Wer ist ein Lehrer gleich wie er?
“Mungu ametukuzwa katika nguvu zake. Ni nani aliye mwalimu kama yeye?
23 Wer stellt ihn über seinen Weg zur Rede? Wer sagt nur: 'Du hast schlecht gehandelt'?
Ni nani aliyemwelekeza katika njia zake, au kumwambia, ‘Wewe umetenda yasiyo sawa’?
24 Bedenk, daß du sein Tun des Irrtums zeihst, das andere in Lobliedern besingen!
Kumbuka kuzitukuza kazi zake, ambazo watu wamezisifu katika wimbo.
25 Und alle Menschen haben ihre Lust daran; die Sterblichen betrachten es seit fernsten Zeiten.
Wanadamu wote wameiona; watu wanaikazia macho kwa mbali.
26 Sieh, Gott ist alt, weit über unsere Begriffe, und unerforschlich seiner Jahre Zahl.
Tazama jinsi Mungu alivyo mkuu, kupita ufahamu wetu! Hesabu ya miaka yake haitafutiki.
27 Er zählt die Wassertropfen ab, daß sie in seinen Nebel hin als Regen sickern,
“Yeye huvuta juu matone ya maji, ayachujayo kama mvua kutoka kwenye vijito;
28 den Wolken rieseln lassen, auf viele Menschen niederträufelnd.
mawingu huangusha chini maji yake, nayo mvua nyingi huwanyeshea wanadamu.
29 Wer vollends hätte Einsicht in der Wolken Weite, in das Gedröhne seines Wohngezeltes,
Ni nani ajuaye jinsi ayatandazavyo mawingu, jinsi angurumavyo kutoka hemani mwake.
30 wenn er darin sein Rollen weithin tönen läßt und dann des Meeres Quellen niederrinnen?
Tazama jinsi anavyotandaza umeme wa radi kumzunguka, naye huvifunika vilindi vya bahari.
31 Denn damit gibt er Völkern Nahrung, stellt Speise her in großer Menge.
Hivi ndivyo atawalavyo mataifa, na kuwapa chakula kwa wingi.
32 Er birgt den Blitzstrahl in den Händen, befiehlt ihm, wo er einzuschlagen hat.
Huujaza mkono wake kwa umeme wa radi, na kuuagiza kulenga shabaha yake.
33 Er zeigt ihm seinen Freund; den Frevler aber läßt er ihn durchbohren."
Ngurumo zake hutangaza dhoruba inayokuja; hata mifugo hujulisha kukaribia kwake.