< 1 Mose 5 >

1 Das ist die Urkunde der Geschlechterfolge Adams: Damals, als Gott den Adam schuf, machte er ihn in Gottes Ähnlichkeit.
Hii ni orodha ya vizazi vya Adamu. Katika siku ambayo Mungu alimuumba mtu, aliwaumba katika mfano wake mwenyewe.
2 Männlich und weiblich schuf er sie. Dann segnete er sie und hieß sie "Mensch", damals, als sie geschaffen worden waren.
Mwanaume na mwanamke aliwaumba. Akawabariki na akawaita Adam wakati walipoumbwa.
3 Und Adam war 130 Jahre alt; da zeugte er in seiner Ähnlichkeit nach seinem Bild einen Sohn und hieß ihn Set.
Wakati Adamu alipokuwa ameishi miaka 130, akamzaa mwana katika sura yake mwenyewe, kwa mfano wake, na akamuita jina lake Sethi.
4 Der Tage Adams waren es nach Sets Zeugung 800 Jahre und er zeugte noch Söhne und Töchter.
Baada ya Adamu kumzaa Sethi, aliishi miaka mia nane. Akawazaa wana wengi waume na wake.
5 Und aller Tage Adams waren 930 Jahre. Da starb er.
Adamu akaishi miaka 930 kisha akafariki.
6 Set war 105 Jahre alt; da zeugte er Enos.
Wakati Sethi alipokuwa ameishi miaka 105, akamzaa Enoshi.
7 Und Set lebte nach des Enos Zeugung 807 Jahre und zeugte noch Söhne und Töchter.
Baada ya kumzaa Enoshi, akaishi miaka 807 na akawazaa wana wengi waume na wake.
8 Und aller Tage Sets waren 912 Jahre; da starb er.
Sethi akaishi miaka 912 kisha akafariki.
9 Enos war 90 Jahre alt; da zeugte er Kenan.
Wakati Enoshi alipokuwa ameishi miaka tisini, akamzaa Kenani.
10 Und Enos lebte nach Kenans Zeugung 815 Jahre und zeugte noch Söhne und Töchter.
Baada ya kumzaa Kenani, Enoshi aliishi miaka 815. Akazaa wana wengi wa ume na wake.
11 Und aller Tage des Enos waren 905 Jahre; da starb er.
Enoshi aliishi miaka 905 na kisha akafariki.
12 Und Kenan war 70 Jahre alt; da zeugte er Mahalalel.
Wakati Kanani alipokuwa ameishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli.
13 Und Kenan lebte nach Mahalalels Zeugung 840 Jahre und zeugte noch Söhne und Töchter.
Baada ya kumzaa Mahalaleli, Kenani aliishi miaka 840. Akawazaa wana wengi wa ume na wake.
14 Und aller Tage Kenans waren 910 Jahre; da starb er.
Kenani aliishi miaka 910, na kisha akafariki.
15 Und Mahalalel war 65 Jahre alt; da zeugte er Jered.
Mahalaleli alipokuwa ameishi miaka sitini na tano, alimzaa Yaredi.
16 Und Mahalalel lebte nach Jereds Zeugung 830 Jahre und zeugte noch Söhne und Töchter.
Baada ya kumzaa Yaredi, Mahalaleli aliishi miaka 830. Akazaa wana wengi wa ume na wake.
17 Und aller Tage Mahalalels waren 895 Jahre; da starb er.
Mahalaleli aliishi miaka 895 na kisha akafariki.
18 Und Jered war 162 Jahre alt; da zeugte er Henoch.
Yaredi alipokuwa ameishi miaka 162, alimzaa Henoko.
19 Und Jered lebte nach Henochs Zeugung 800 Jahre und zeugte noch Söhne und Töchter.
Baada ya kumzaa Henoko, Yaredi aliishi miaka mianane. Akazaa wana wengi waume na wake.
20 Und aller Tage Jereds waren 962 Jahre; da starb er.
Yaredi aliishi miaka 962 na kisha akafariki.
21 Und Henoch war 65 Jahre alt; da zeugte er Metuselach.
Henoko alipokuwa ameishi miaka sitini na tano, akamzaa Methusela.
22 Nach Metuselachs Zeugung wandelte Henoch mit Gott 300 Jahre und zeugte noch Söhne und Töchter.
Henoko akaenenda na Mungu miaka miatatu baada ya kumzaa Methusela. Aliwazaa wana wengi wa ume na wake.
23 Und aller Tage Henochs waren 365 Jahre.
Henoko aliishi miaka 365.
24 Und Henoch wandelte mit Gott, und plötzlich war er nicht mehr da, weil ihn Gott weggenommen hatte.
Henoko alienenda na Mungu, na kisha alitoweka, kwa kuwa Mungu alimtwaa.
25 Und Metuselach war 187 Jahre alt; da zeugte er Lamech.
Wakati Methusela alipokuwa ameishi miaka 187, alimzaa Lameki.
26 Und Metuselach lebte nach Lamechs Zeugung 782 Jahre und zeugte noch Söhne und Töchter.
Baada ya kumzaa Lameki, Methusela aliishi miaka 782. Akawazaa wana wengi wa ume na wake.
27 Und aller Tage Metuselachs waren 969 Jahre; da starb er.
Methusela aliishi miaka 969. Kisha akafariki.
28 Und Lamech war 182 Jahre alt; da zeugte er einen Sohn.
Wakati Lameki alipokuwa ameishi miaka 182, alimzaa mwana.
29 Und er hieß seinen Sohn Noe und sprach: "Dieser soll uns Trost bringen, nach unserer Arbeit und unserer Hände Mühen, aus eben diesem Boden, den der Herr verflucht hat."
Akamuita jina lake Nuhu, akisema, “Huyu ndiye atatupatia pumziko kutoka katika kazi yetu na kutoka katika kazi ya taabu ya mikono yetu, ambayo lazima tuifanye kwa sababu ya ardhi ambayo Yahwe ameilaani.”
30 Und Lamech lebte nach Noes Zeugung 595 Jahre und zeugte noch Söhne und Töchter.
Lameki aliishi miaka 595 baada ya kumzaa baba wa Nuhu. Akazaa wanawengi wa ume na wake.
31 Und aller Tage Lamechs waren 777 Jahre; da starb er.
Lameki aliishi miaka 777. Kisha akafariki.
32 Und Noe war 500 Jahre alt; da zeugte Noe Sem, Cham und Japhet.
Baada ya Nuhu kuishi miaka miatano, akamzaa Shemu, Hamu, na Yafethi.

< 1 Mose 5 >