< Psalm 111 >

1 Lobet Jehova! Preisen will ich Jehova von ganzem Herzen im Kreise der Aufrichtigen und in der Gemeinde.
Msifuni Bwana. Nitamtukuza Bwana kwa moyo wangu wote, katika baraza la wanyofu na katika kusanyiko.
2 Groß sind die Taten Jehovas, sie werden erforscht von allen, die Lust an ihnen haben.
Kazi za Bwana ni kuu, wote wanaopendezwa nazo huzitafakari.
3 Majestät und Pracht ist sein Tun; und seine Gerechtigkeit besteht ewiglich.
Kazi zake zimejaa fahari na utukufu, haki yake hudumu daima.
4 Er hat ein Gedächtnis gestiftet seinen Wundertaten; gnädig und barmherzig ist Jehova.
Amefanya maajabu yake yakumbukwe, Bwana ni mwenye neema na huruma.
5 Er hat Speise gegeben denen, die ihn fürchten; er gedenkt in Ewigkeit seines Bundes.
Huwapa chakula wale wanaomcha, hulikumbuka agano lake milele.
6 Er hat seinem Volke kundgemacht die Kraft seiner Taten, um ihnen zu geben das Erbteil der Nationen.
Amewaonyesha watu wake uwezo wa kazi zake, akiwapa nchi za mataifa mengine.
7 Die Taten seiner Hände sind Wahrheit und Recht; zuverlässig sind alle seine Vorschriften,
Kazi za mikono yake ni za uaminifu na haki, mausia yake yote ni ya kuaminika.
8 festgestellt auf immer, auf ewig, ausgeführt in Wahrheit und Geradheit.
Zinadumu milele na milele, zikifanyika kwa uaminifu na unyofu.
9 Er hat Erlösung gesandt seinem Volke, seinen Bund verordnet auf ewig; heilig und furchtbar ist sein Name.
Aliwapa watu wake ukombozi, aliamuru agano lake milele: jina lake ni takatifu na la kuogopwa.
10 Die Furcht Jehovas ist der Weisheit Anfang; gute Einsicht haben alle, die sie ausüben. Sein Lob besteht ewiglich.
Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, wote wanaozifuata amri zake wana busara. Sifa zake zadumu milele.

< Psalm 111 >