< Psalm 106 >

1 [Lobet Jehova! [Hallelujah!] ] Preiset [O. Danket] Jehova! denn er ist gut, denn seine Güte währt ewiglich.
Msifuni Yahwe. Mshukuruni Yahwe, kwa kuwa ni mwema, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
2 Wer wird aussprechen die Machttaten Gottes, hören lassen all sein Lob? [O. all seinen Ruhm]
Ni nani awezaye kuyahesabu mataendo makuu ya yahwe au kutangaza katika ukamilifu sifa zote za matendo yake ya kuaminika.
3 Glückselig die das Recht bewahren, der Gerechtigkeit übt zu aller Zeit!
Wamebarikiwa wale watendao yaliyo mema na matendo yao yaliyo haki siku zote.
4 Gedenke meiner, Jehova, mit der Gunst gegen dein Volk; suche mich heim mit deiner Rettung!
Ukumbuke, Ee Yahwe, unapowaonesha watu wako neema; unisaidie unapowaokoa.
5 Daß ich anschaue die Wohlfahrt deiner Auserwählten, mich erfreue an [O. mit] der Freude deiner Nation, mich rühme mit deinem Erbteil.
Ndipo nitaona mafanikio ya wateule wako, wakifurahia katika furaha ya taifa lako, na utukufu pamoja na urithi wako.
6 Wir haben gesündigt samt unseren Vätern, [O. wie unsere Väter] haben unrecht getan, [Eig. verkehrt gehandelt] haben gesetzlos gehandelt.
Tumefanya dhambi kama babu zetu, tumekosea, na kufanya uovu.
7 Unsere Väter in Ägypten beachteten nicht deine Wundertaten, gedachten nicht der Menge deiner Gütigkeiten und waren widerspenstig am Meere, beim Schilfmeere.
Baba zetu hawakuyatambua matendo yako ya ajabu katika Misri; walipuuzia matendo yako mengi ya uaminifu wa agano; waliasi penye bahari, bahari ya Shamu.
8 Aber er rettete sie um seines Namens willen, um kundzutun seine Macht.
Hata hivyo, yeye aliwaokoa kwa ajili ya jina lake ili kwamba aweze kuzifunua nguvu zake.
9 Und er schalt das Schilfmeer, und es ward trocken; und er ließ sie durch die Tiefen [O. Fluten; s. die Anm. zu Ps. 33,7] gehen wie durch eine Wüste.
Aliikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka. Kisha akawaongoza vilindini, kana kwamba ni jangwani.
10 Und er rettete sie aus der Hand des Hassers, und erlöste sie aus der Hand des Feindes.
Aliwaokoa kutoka mkononi mwa wale waliowachukia, na aliwaokoa kutoka mkononi mwa adui.
11 Und die Wasser bedeckten ihre Bedränger, nicht einer von ihnen blieb übrig.
Lakini maji yaliwafunika washindani wao; hakuna hata mmoja aliye okolewa.
12 Da glaubten sie seinen Worten, sie sangen sein Lob.
Ndipo waliyaamini maneno yake, nao waliimba sifa zake.
13 Schnell vergaßen sie seine Taten, warteten nicht auf seinen Rat; [Hier in dem Sinne von Plan, Ratschluß]
Lakini walisahau haraka kile alichofanya; hawakuyasubiri maelekezo yake.
14 Und sie wurden lüstern in der Wüste und versuchten Gott [El] in der Einöde.
Walikuwa na tamaa isiyotoshelezwa jangwani, wakamjaribu Mungu nyikani.
15 Da gab er ihnen ihr Begehr, aber er sandte Magerkeit in ihre Seelen.
Aliwapa ombi lao, lakini alituma gonjwa ambalo lilishambulia miili yao.
16 Und sie wurden eifersüchtig auf Mose im Lager, auf Aaron, den Heiligen Jehovas.
Katika kambi wakawa na wivu juu Musa na Haruni, kuhani mtakatifu wa Yahwe.
17 Die Erde tat sich auf, und verschlang Dathan und bedeckte die Rotte Abirams;
Nchi ilifunguka na ilimmeza Dathani na iliwafunika wafuasi wa Abiramu.
18 Und ein Feuer brannte unter ihrer Rotte, eine Flamme verzehrte die Gesetzlosen.
Moto uliwaka kati yao; moto uliwaangamiza waovu.
19 Sie machten ein Kalb am Horeb und bückten sich vor einem gegossenen Bilde;
Walitengeneza ndama huko Horebu na kuabudu sanamu ya kuyeyuka.
20 Und sie vertauschten ihre Herrlichkeit gegen das Bild eines Stieres, der Gras frißt.
Wakaubadili utukufu wa Mungu kuwa mfano wa ng'ombe alaye majani.
21 Sie vergaßen Gottes, [El] ihres Retters, der Großes getan in Ägypten,
Walimsahau Mungu wokozi wao, aliyefanya mambo makuu katika Misri.
22 Wundertaten im Lande Hams, Furchtbares am Schilfmeer.
Alifanya matendo ya ajabu katika nchi ya Hamu na matendo makuu penye Bahari ya Shamu.
23 Da sprach er, daß er sie vertilgen wollte, wenn nicht Mose, sein Auserwählter, vor ihm in dem Riß gestanden hätte, um seinen Grimm vom Verderben abzuwenden.
Mungu angetangaza uharibifu wao, kama sio Musa, mteule wake, aliingilia kati kugeuza hasira yake dhidi ya kuwaangamiza.
24 Und sie verschmähten das köstliche Land, glaubten nicht seinem Worte;
Kisha waliidharau nchi yenye matunda; hawakuiamini ahadi yake,
25 Und sie murrten in ihren Zelten, hörten nicht auf die Stimme Jehovas.
bali walilalamiaka katika mahema yao, na hawakumtii Yahwe.
26 Da schwur er ihnen, [Eig. erhob er ihnen seine Hand] sie niederzuschlagen in der Wüste,
Kwa hiyo aliinua mkono wake na kuapa kwao kuwa atawaacha wafe jangwani,
27 Und ihren Samen niederzuschlagen unter den [And. l.: zu vertreiben unter die] Nationen und sie zu zerstreuen in die Länder.
akitawanya uzao wao kati ya mataifa, na kuwatawanya katika nchi za kigeni.
28 Und sie hängten sich an Baal-Peor und aßen Schlachtopfer der Toten; [d. h. der toten Götzen]
Waliabudu Baal ya Poeri na walizila dhabihu zilizotolewa kwa wafu.
29 Und sie erbitterten ihn durch ihre Handlungen, und eine Plage brach unter sie ein.
Walimkasirisha kwa matendo yao, na pigo la gonjwa baya liliwashambulia kati yao.
30 Da stand Pinehas auf und übte Gericht, und der Plage ward gewehrt.
Ndipo Finehasi aliinuka kuingilia kati, na pigo likakoma.
31 Und es wurde ihm zur Gerechtigkeit gerechnet von Geschlecht zu Geschlecht bis in Ewigkeit.
Ilihesabika kwake kama tendo la haki kwa vizazi vyote hata milele.
32 Und sie erzürnten ihn an dem Wasser von Meriba, und es erging Mose übel ihretwegen;
Pia walimkasirisha Yahwe penye maji ya Meriba, na Musa aliteseka kwa ajili yao.
33 Denn sie reizten seinen Geist, so daß er [O. weil sie widerspenstig waren gegen seinen Geist, und er] unbedacht redete mit seinen Lippen.
Walimghadhabisha Musa naye akaongea haraka.
34 Sie vertilgten die Völker nicht, wie doch [W. welche] Jehova ihnen gesagt hatte;
Hawakuyaharibu mataifa kama Yahwe alivyowaamuru,
35 Und sie vermischten sich mit den Nationen und lernten ihre Werke;
bali walichangamana na mataifa na walijifunza njia zao
36 Und sie dienten ihren Götzen, und sie wurden ihnen zum Fallstrick.
nao waliabudu sanamu, nazo zikawa mtego kwao.
37 Und sie opferten ihre Söhne und ihre Töchter den Dämonen.
Waliwatoa wana wao na binti zao kwa mapepo.
38 Und sie vergossen unschuldiges Blut, das Blut ihrer Söhne und ihrer Töchter, welche sie den Götzen Kanaans opferten; und das Land wurde durch Blut entweiht.
Walimwaga damu isiyo na hatia, damu ya wana na binti zao, ambao waliwatoa kama dhabihu kwa sanamu za Kanaani, waliinajisi nchi kwa damu.
39 Und sie verunreinigten sich durch ihre Werke und hurten durch ihre Handlungen.
Walinajisiwa kwa matendo yao; katika matendo yao walikuwa kama malaya.
40 Da entbrannte der Zorn Jehovas wider sein Volk, und er verabscheute sein Erbteil;
Hivyo Yahwe aliwakasilikia watu wake, akawadharau watu wake mwenyewe.
41 Und er gab sie in die Hand der Nationen, und ihre Hasser herrschten über sie;
Akawaruhusu mataifa, na wale walio wachukia wakawatawala.
42 Und ihre Feinde bedrückten sie, und sie wurden gebeugt unter ihre Hand.
Maadui zao wakawaonea, wakatiishwa chini ya mamlaka yao.
43 Oftmals errettete er sie; sie aber waren widerspenstig in ihren Anschlägen, [Eig. in ihrem Ratschlag] und sie sanken hin durch ihre Ungerechtigkeit.
Mara nyingi alienda kuwasaidia, lakini waliendelea kuasi nao walishushwa chini kwa dhambi zao wenyewe.
44 Und er sah an ihre Bedrängnis, wenn er ihr Schreien hörte;
Hata hivyo, aliiangalia dhiki yao aliposikia kilio chao kwa ajili ya msaada.
45 Und er gedachte ihnen seinen Bund, und es reute ihn nach der Größe seiner Güte. [Eig. der Menge seiner Gütigkeiten]
Alikumbuka agano lake pamoja nao na alijirudi kwa sababu ya upendo wake thabiti.
46 Und er ließ sie Erbarmen finden vor allen, die sie gefangen weggeführt hatten.
Aliwafanya wote waliowateka wawahurumie.
47 Rette uns, Jehova, unser Gott, und sammle uns aus den Nationen, daß wir deinen heiligen Namen preisen, daß wir uns rühmen deines Lobes!
Utuokoe, Ee Yahwe, Mungu wetu. Utukusanye kutoka kati ya mataifa ili kwamba tuweze kulishukuru jina lako takatifu na utukufu katika sifa zako. Yahwe,
48 Gepriesen sei Jehova, der Gott Israels, von Ewigkeit zu Ewigkeit! Und alles Volk sage: Amen! Lobet Jehova! [Hallelujah!]
Mungu wa Israeli, na asifiwe toka milele na milele. watu wote walisema, “Amen.” Msifuni Yahwe. Kitabu cha tano.

< Psalm 106 >