< Sprueche 6 >

1 Mein Sohn, wenn du Bürge geworden bist für deinen Nächsten, für einen anderen deine Hand eingeschlagen hast;
Mwanangu, kama utaweka pesa zako kuwa dhamana kwa mkopo wa jirani yako; kama ukitoa ahadi yako katika mkopo wa mtu usiyemjua,
2 bist du verstrickt durch die Worte deines Mundes, gefangen durch die Worte deines Mundes:
basi umejiwekea mtego mwenyewe na umenaswa kwa maneno ya kinywa chako.
3 tue denn dieses, mein Sohn, und reiße dich los, da du in deines Nächsten Hand gekommen bist; gehe hin, wirf dich nieder, und bestürme deinen Nächsten;
Mwanagu, ukinaswa kwa maneno yako mwenyewe, fanya haya ili kujiokoa, kwa kuwa umeangukia kwenye mikono ya jirani yako; nenda unyenyekee na ufanye shauri mbele ya jirani yako.
4 gestatte deinen Augen keinen Schlaf, und keinen Schlummer deinen Wimpern;
Usiruhusu usingizi katika macho yako wala kope za macho yako kusinzia.
5 reiße dich los wie eine Gazelle aus der Hand, und wie ein Vogel aus der Hand des Vogelstellers.
Jiokoe mwenyewe kama swala kutoka katika mkono wa mwindaji, kama ndege kutoka katika mkono wa mwinda ndege.
6 Geh hin zur Ameise, du Fauler, sieh ihre Wege und werde weise.
Wewe mtu mvivu, mwangalie mchwa, zitafakari njia zake ili kupata busara.
7 Sie, die keinen Richter, Vorsteher und Gebieter hat,
Hana akida, afisa au mtawala,
8 sie bereitet im Sommer ihr Brot, hat in der Ernte ihre Nahrung eingesammelt.
lakini huandaa chakula chake wakati wa joto na wakati wa mavuno huweka hazina ili kula baadaye.
9 Bis wann willst du liegen, du Fauler? wann willst du von deinem Schlafe aufstehen?
Ewe mtu mvivu, utalala hata lini? Wakati gani utainuka usingizini?”
10 Ein wenig Schlaf, ein wenig Schlummer, ein wenig Händefalten, um auszuruhen:
Lala kidogo, sizia kidogo, kunja mikono kupumzika kidogo” -
11 und deine Armut wird kommen wie ein rüstig Zuschreitender, und deine Not wie ein gewappneter Mann. [W. ein Mann des Schildes]
ndipo umasikini wako utakapokujia kama mporaji na uhitaji wako kama askari wa vita.
12 Ein Belialsmensch, ein heilloser Mann ist, wer umhergeht mit Verkehrtheit [O. Verziehung] des Mundes,
Mtu asiyefaa-mtu mwovu- huishi kwa kauli za udanganyifu wake,
13 mit seinen Augen zwinkt, mit seinen Füßen scharrt, mit seinen Fingern deutet.
akipepesa macho yake, akiashilia kwa miguu yake na kusonta kwa videle vyake.
14 Verkehrtheiten sind in seinem Herzen; er schmiedet Böses zu aller Zeit, streut Zwietracht aus.
Hufanya njama za uovu kwa hila ya moyo wake; daima huchochea faraka.
15 Darum wird plötzlich sein Verderben kommen; im Augenblick wird er zerschmettert werden ohne Heilung. -
Kwa hiyo msiba wake utamkumba kwa ghafula, punde atavunjika vibaya wala hatapona.
16 Sechs sind es, die Jehova haßt, und sieben sind seiner Seele ein Greuel:
Kuna vitu sita ambavyo Yehova huvichukia, saba ambavyo ni chukizo kwake.
17 Hohe Augen, eine Lügenzunge, und Hände, die unschuldiges Blut vergießen;
Macho ya mtu mwenye kiburi, ulimi wa uongo, mikono inayomwaga damu ya watu maasumu,
18 ein Herz, welches heillose Anschläge schmiedet, Füße, die eilends zum Bösen hinlaufen;
moyo unaobuni njama mbaya, miguu inayokimbilia maovu upesi,
19 wer Lügen ausspricht als falscher Zeuge, und wer Zwietracht ausstreut zwischen Brüdern.
shahidi asemaye uongo na apandaye faraka kati ya ndugu.
20 Mein Sohn, bewahre das Gebot deines Vaters, und verlaß nicht die Belehrung deiner Mutter;
Mwanangu, itii amri ya baba yako na wala usiyaache mafundisho ya mama yako.
21 binde sie stets auf dein Herz, knüpfe sie um deinen Hals.
Uyafunge katika moyo wako siku zote; yafunge kwenye shingo yako.
22 Wenn du einhergehst, wird sie dich leiten; wenn du dich niederlegst, [O. wenn du liegst] wird sie über dich wachen; und erwachst du, so wird sie mit dir reden.
utembeapo, yatakuongoza; ulalapo yatakulinda, na uamkapo yatakufundisha.
23 Denn das Gebot ist eine Leuchte, und die Belehrung ein Licht; und die Zurechtweisung der Zucht sind der Weg des Lebens:
Maana amri ni taa, na mafundisho ni nuru; kinga za kuadilisha za njia ya uzima.
24 um dich zu bewahren vor dem bösen Weibe, vor der Glätte der Zunge einer Fremden. [Eig. Ausländerin]
Yanakulinda dhidi ya mwanamke malaya, dhidi ya maneno laini ya uzinzi.
25 Begehre nicht in deinem Herzen nach ihrer Schönheit, und sie fange dich nicht mit ihren Wimpern!
Moyoni mwako usiutamani uzuri wake wala usitekwe katika kope zake.
26 Denn um eines hurerischen Weibes willen kommt man bis auf einen Laib Brot, und eines Mannes Weib stellt einer kostbaren Seele nach. -
Kulala na malaya inaweza kugharimu bei ya kipande cha mkate, lakini mke wa mtu mwingine inagharimu uzima wako wote.
27 Sollte jemand Feuer in seinen Busen nehmen, [Eig. wegnehmen [vom Herde]] ohne daß seine Kleider verbrennten?
Je mtu anaweza kubeba moto katika kifua chake bila kuuguza mavazi yake?
28 Oder sollte jemand über glühende Kohlen gehen, ohne daß seine Füße versengt würden?
Je mtu anaweza kutembea juu ya makaa bila kuchomwa miguu yake?
29 So der, welcher zu dem Weibe seines Nächsten eingeht: keiner, der sie berührt, wird für schuldlos gehalten werden. - [O. ungestraft bleiben]
Ndivyo alivyo mtu alalaye na mke wa jirani yake; yule alalaye na huyo mke hatakosa adhabu.
30 Man verachtet den Dieb nicht, wenn er stiehlt, um seine Gier zu stillen, weil ihn hungert;
Watu hawawezi kumdharau mwizi kama anaiba ili kukidhi hitaji lake la njaa.
31 und wenn er gefunden wird, kann er siebenfach erstatten, kann alles Gut seines Hauses hingeben.
Walakini akimatwa, atalipa mara saba ya kile alichoiba; lazima atoe kila kitu cha thamani katika nyumba yake.
32 Wer mit einem Weibe Ehebruch begeht, ist unsinnig; wer seine Seele verderben will, der tut solches.
Mtu anayefanya uzinzi hana akili; hufanya hiyo kwa uharibifu wake mwenyewe.
33 Plage und Schande wird er finden, und seine Schmach wird nicht ausgelöscht werden.
Anasitahili aibu na majeraha na fedheha yake haiwezi kuondolewa.
34 Denn Eifersucht ist eines Mannes Grimm, und am Tage der Rache schont er nicht.
Maana vivu humghadhibisha mtu; hatakuwa na huruma wakati wa kulipa kisasi chake.
35 Er nimmt keine Rücksicht auf irgendwelche Sühne und willigt nicht ein, magst du auch das Geschenk vergrößern.
Ujapompa zawadi nyingi, hatakubali mbadala wa kusuruhishwa wala kulipwa.

< Sprueche 6 >