< 1 Chronik 24 >
1 Und was die Söhne Aarons betrifft, so waren ihre Abteilungen: Die Söhne Aarons: Nadab und Abihu, Eleasar und Ithamar.
Makundi vya kazi kulingana na uzao wa Aroni yalikuwa haya: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
2 Und Nadab und Abihu starben vor ihrem Vater, und sie hatten keine Söhne; und Eleasar und Ithamar übten den Priesterdienst aus.
Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao kufa. Walikuwa hawana watoto, kwahiyo Eleazari na Ithamari walitumika kama makuhani.
3 Und David, und Zadok von den Söhnen Eleasars, und Ahimelech von den Söhnen Ithamars teilten sie ab nach ihrem Amte, in ihrem Dienste.
Daudi pamoja na Zadoki, uzao wa Eleazari, na Ahimeleki, uzao wa Ithamari, waliwagawanya katika makundi yao ya kazi kama makuhani.
4 Und von den Söhnen Eleasars wurden mehr Familienhäupter [W. Häupter der Männer, d. h. der Familienväter] gefunden, als von den Söhnen Ithamars; und so teilten sie sie so ab: Von den Söhnen Eleasars sechzehn Häupter von Vaterhäusern, und von den Söhnen Ithamars acht Häupter von ihren Vaterhäusern.
Kulikuwa na wanaume viongozi zaidi kati ya uzao wa Eleazari kuliko kati ya uzao wa Ithamari, kwahiyo waligawanya uzao wa Eleazari katika makundi kumi na sita. Walifanya hivyo na viongozi wa ukoo na uzao wa Ithamari. Magawanyo haya yalikuwa nane kwa idadi, sambamba na koo zao.
5 Und zwar teilten sie sie durch Lose ab, diese wie jene; denn die Obersten des Heiligtums und die Obersten Gottes waren aus den Söhnen Eleasars und aus den Söhnen Ithamars.
Waliwagawanya bila upendeleo kwa kura, kwa kuwa walikuwa waamuzi watakatifu na waamuzi wa Mungu, kutoka pande zote uzao wa Eleazari na uzao wa Ithamari.
6 Und Schemaja, der Sohn Nethaneels, der Schreiber aus Levi, schrieb sie auf in Gegenwart des Königs und der Obersten und Zadoks, des Priesters, und Ahimelechs, des Sohnes Abjathars, und der Häupter der Väter der Priester und der Leviten. Je ein Vaterhaus wurde ausgelost für Eleasar, und je eines wurde ausgelost für Ithamar. [Eig. gezogen für Eleasar, und gezogen, gezogen für Ithamar]
Shemaia mwana wa Nethaneli mwandishi, Mlawi, aliandika majina yao mbele ya mfalme, muamuzi, kuhani Zadoki, Ahimeleki mwana wa Abiathari, na viongozi wa makuhani na familia za Walawi. Ukoo mmoja ulichaguliwa kwa kura kutoka uzao wa Eleazari, na kisha uliofata utachaguliwa kutoka uzao wa Ithhamari.
7 Und das erste Los kam heraus für Jehojarib, für Jedaja das zweite,
Kura ya kwanza ilienda kwa Yehoiaribu, ya pili kwa Yedaia,
8 für Harim das dritte, für Seorim das vierte,
ya tatu kwa Harimu, ya nne kwa Seorimu,
9 für Malkija das fünfte, für Mijamin das sechste,
ya tano kwa Malikija, ya sita kwa Mijamini,
10 für Hakkoz das siebte, für Abija das achte,
ya saba kwa Hakozi, ya nane kwa Abija,
11 für Jeschua das neunte, für Schekanja das zehnte,
ya tisa kwa Yeshua, ya kumi kwa Shekania,
12 für Eljaschib das elfte, für Jakim das zwölfte,
ya kumi na moja kwa Eliashibu, ya kumi na mbili kwa Yakimu,
13 für Huppa das dreizehnte, für Jeschebab das vierzehnte,
ya kumi na tatu kwa Hupa, ya kumi na nne kwa Yesheheabu,
14 für Bilga das fünfzehnte, für Immer das sechzehnte,
ya kumi na tano kwa Biliga, ya kumi na sita kwa Imma,
15 für Hesir das siebzehnte, für Happizez das achtzehnte,
ya kumi na saba kwa Heziri, ya kumi na nane kwa Hapizezi,
16 für Pethachja das neunzehnte, für Jecheskel das zwanzigste,
ya kumi na tisa kwa Pethaia, ya ishirini kwa Yehezikeli,
17 für Jakin das einundzwanzigste, für Gamul das zweiundzwanzigste,
ya ishirini na moja kwa Yakini, ya ishirini na mbili kwa Gamuli,
18 für Delaja das dreiundzwanzigste, für Maasja das vierundzwanzigste.
ya ishirini na tatu kwa Delaia, na ya ishirini na nne kwa Maazia.
19 Das war ihre Einteilung zu ihrem Dienst, um in das Haus Jehovas zu kommen nach ihrer Vorschrift, gegeben durch ihren Vater Aaron, so wie Jehova, der Gott Israels, ihm geboten hatte.
Hii ilikuwa taratibu ya utumishi wao, walipo kuja kwenye nyumba ya Yahweh, wakifuata utaratibu waliopewa na Aruni babu yao, kama Yahweh, Mungu wa Israeli, alivyo waagiza.
20 Und was die übrigen Söhne Levis betrifft: von den Söhnen Amrams: Schubael; von den Söhnen Schubaels: Jechdeja. -
Hawa walikuwa Walawi waliobakia: Wana wa Amiramu, Shebueli; wana wa Shebaeli, Yedeia.
21 Von Rechabja, von den Söhnen Rechabjas: das Haupt, Jischija. -
Wana wa Rehabia: wana wa Rehabia, Ishia kiongozi.
22 Von den Jizharitern: Schelomoth; von den Söhnen Schelomoths: Jachath. -
Wa Waizari, Shelomothi; mwana wa Shelomothi, Yahathi.
23 Und die Söhne Hebrons: [Vergl. Kap. 23,19] Jerija, das Haupt; Amarja, der zweite; Jachasiel, der dritte; Jekamam, der vierte. -
Wana wa Hebroni: Yeria kiongozi, Amaria wapili, Yahazieli watatu, na Yekameamu wanne.
24 die Söhne Ussiels: Micha; von den Söhnen Michas: Schamir.
Wana wa uzao wa Uzieli ulimjumuisha Mika. Uzao wa Mika ulimjumuisha Shamiri.
25 Der Bruder Michas war Jischija; von den Söhnen Jischijas: Sekarja. -
Kaka wa Mika alikuwa Ishia. Wana wa Ishia akijumuishwa Zakaria.
26 Die Söhne Meraris: Machli und Musi. Die Söhne Jaasijas, seines Sohnes:
Wana na Merari: Mahli na Mushi. Mwana wa Yaazia, Beno.
27 die Söhne Meraris von Jaasija, seinem Sohne: Schoham und Sakkur und Ibri;
Wana wa Merari: Yaazia, Beno, Shohamu, Zakuri, na Ibrri.
28 von Machli: Eleasar, der hatte aber keine Söhne;
Wana wa Mahili: eleazari, ambaye alikuwa hana wana.
29 von Kis, die Söhne Kis: Jerachmeel;
Wana wa Kishi: Yerameli
30 und die Söhne Musis: Machil und Eder und Jerimoth. Das waren die Söhne der Leviten, nach ihren Vaterhäusern.
wana wa Mushi: Mahli, Eda, na yerimothi. Walikuwa walawi, walio orodheshwa na familia zao.
31 Und auch sie warfen Lose wie ihre Brüder, die Söhne Aarons, in Gegenwart des Königs David und Zadoks und Ahimelechs und der Häupter der Väter der Priester und der Leviten, das Haupt der Väter wie sein geringster Bruder.
Wanaume hawa ambao walikuwa vichwa katika nyumba za baba zao na kila wadogo zao, walipiga kura katika uwepo wa Mfalme Daudi, na Zadoki na Ahimeleki, pamoja na viongozi wa familia wa makuhani na Walawi. Walirusha kura kama uzao wa Aroni walivyofanya.