< Hebraeer 13 >

1 Die Bruderliebe dauere fort!
Endeleeni kupendana kidugu.
2 Gastfreundschaft zu üben vergeßt nicht! Denn dadurch haben einige ohne ihr Wissen Engel beherbergt.
Msisahau kuwakaribisha wageni; maana kwa kufanya hivyo watu wengine walipata kuwakaribisha malaika bila kujua.
3 Gedenkt der Gefangenen, als wäret ihr auch im Gefängnis! Nehmt euch der Bedrängten an; ihr seid ja auch im (sterblichen) Leib!
Wakumbukeni wale waliofungwa kana kwamba mmefungwa pamoja nao. Wakumbukeni wale wanaoteseka kana kwamba nanyi mnateseka kama wao.
4 Haltet die Ehe in jeder Hinsicht in Ehren; befleckt nicht das Ehebett! Denn Unzüchtige und Ehebrecher wird Gott richten.
Ndoa inapaswa kuheshimiwa na watu wote, na haki zake zitekelezwe kwa uaminifu. Mungu atawahukumu waasherati na wazinzi.
5 Euer Sinn sei frei von Geldgier! Seid zufrieden mit dem, was euch beschieden ist! Er selbst hat ja gesagt: Nie will ich von dir abtun meine Hand, nie dich verlassen.
Msiwe watu wa kupenda fedha; toshekeni na vile vitu mlivyo navyo. Mungu mwenyewe amesema: “Sitakuacha kamwe, wala sitakutupa.”
6 Darum können wir auch getrosten Mutes sprechen: Der Herr ist mein Helfer, ich werde mich nicht fürchten. Was können mir Menschen tun?
Ndiyo maana tunathubutu kusema: “Bwana ndiye msaada wangu, sitaogopa. Binadamu atanifanya nini?”
7 Gedenkt eurer Führer, die euch Gottes Wort verkündigt haben! Schaut auf den Ausgang ihrer Erdenwallfahrt und folgt ihrem Glauben nach!
wakumbukeni viongozi wenu waliowatangazieni ujumbe wa Mungu. Fikirieni juu ya mwenendo wao, mkaige imani yao.
8 Jesus Christus ist gestern, heute und in Ewigkeit derselbe! (aiōn g165)
Yesu Kristo ni yuleyule, jana, leo na milele. (aiōn g165)
9 Laßt euch nicht durch allerlei fremdartige Lehren irreführen! Denn gut und heilsam ist's, daß das Herz durch Gnade fest werde. Durch Speisen kann das nicht geschehen. Die sich damit befassen, sind ohne den erwarteten Gewinn geblieben.
Msipeperushwe huku na huku kwa mafundisho tofauti ya kigeni. Neema ya Mungu ndiyo inayoimarisha roho zetu na wala si masharti juu ya chakula; masharti hayo hayakumsaidia kamwe mtu yeyote aliyeyafuata.
10 Wir haben einen Altar, von dessen Opfer die nicht essen dürfen, die (Gott nach den Vorschriften) der Stiftshütte dienen.
Sisi tunayo madhabahu ambayo wale wanaotumikia bado katika hema la Wayahudi, hawana haki ya kula vitu vyake.
11 Denn die Leiber jener Tiere, deren Blut zur Sühnung für die Sünde durch den Hohenpriester in das Allerheiligste getragen wird, die pflegt man außerhalb des Lagers zu verbrennen.
Kuhani Mkuu wa Kiyahudi huleta damu ya wanyama katika Mahali Patakatifu na kuitoa dhabihu kwa ajili ya dhambi; lakini nyama za hao wanyama huteketezwa nje ya kambi.
12 Darum hat auch Jesus, um durch sein eigen Blut das Volk zu weihen, außerhalb des Tores gelitten.
Ndiyo maana Yesu pia, kusudi apate kuwatakasa watu kwa damu yake mwenyewe, aliteswa na kufa nje ya mji.
13 So laßt uns denn zu ihm hinausgehen außerhalb des Lagers und seine Schmach auf uns nehmen!
Basi, tumwendee huko nje ya kambi tukajitwike laana yake.
14 Denn hier haben wir keine bleibende Stadt, sondern unsere Sehnsucht steht nach der zukünftigen.
Maana hapa duniani hatuna mji wa kudumu; lakini tunautafuta ule unaokuja.
15 Durch ihn laßt uns nun fort und fort Gott Lobopfer bringen: "die Frucht der Lippen", die seinen Namen preisen!
Basi, kwa njia ya Yesu, tumtolee Mungu dhabihu ya sifa daima, yaani sifa zinazotolewa na midomo inayoliungama jina lake.
16 Vergeßt auch nicht wohlzutun und mitzuteilen, denn an solchen Opfern hat Gott Wohlgefallen!
Msisahau kutenda mema na kusaidiana, maana hizi ndizo dhabihu zinazompendeza Mungu.
17 Gehorcht euern Vorstehern und folgt ihnen! Denn sie sind Wächter zum Heil eurer Seelen, und sie sollen einst Rechenschaft (von ihrer Arbeit) ablegen. Das möchten sie mit Freuden tun und nicht mit Seufzen; denn dies wäre euch zum Schaden.
Watiini viongozi wenu na kushika amri zao; wao huchunga roho zenu usiku na mchana, na watatoa ripoti ya utumishi wao mbele ya Mungu. Kama mkiwatii watafanya kazi zao kwa furaha, la sivyo, watazifanya kwa huzuni, na hiyo haitakuwa na faida kwenu.
18 Betet für uns! Denn wir meinen, daß wir ein gutes Gewissen haben, da wir in jeder Hinsicht recht zu wandeln trachten.
Tuombeeni na sisi. Tuna hakika kwamba tunayo dhamiri safi, maana twataka kufanya lililo sawa daima.
19 Und besonders deshalb fordere ich euch zu dieser Fürbitte auf, damit ich euch desto eher zurückgegeben werde.
Nawasihi sana mniombee ili Mungu anirudishe kwenu upesi iwezekanavyo.
20 Gott, der Friedenspender, der Jesus, unseren Herrn, aus den Toten heraufgeführt, weil er durch sein Blut eine ewige Gottesstiftung begründet hat, und ihn nun eingesetzt zum Oberhirten seiner Schafe, (aiōnios g166)
Mungu amemfufua Bwana wetu Yesu Kristo ambaye ni Mchungaji Mkuu wa kondoo kwa sababu ya kumwaga damu yake iliyothibitisha agano la milele. (aiōnios g166)
21 der vollende euch in allem Guten, damit ihr seinen Willen tut, und wirke selbst in euch, was vor ihm wohlgefällig ist durch Jesus Christus! Ihm sei Ehre in alle Ewigkeit! Amen. (aiōn g165)
Mungu wa amani awakamilishe katika kila tendo jema ili mtekeleze mapenzi yake; yeye na afanye ndani yetu kwa njia ya Kristo yale yanayompendeza mwenyewe. Utukufu uwe kwake, milele na milele! Amina. (aiōn g165)
22 Ich bitte euch, Brüder, nehmt mein Ermahnungswort freundlich auf! Ich habe euch ja auch nur einen kurzen Brief geschrieben.
Basi, ndugu, nawasihi mpokee kwa utulivu ujumbe huu wa kuwatieni moyo. Hii ni barua fupi tu ambayo nimewaandikieni.
23 Die Abreise des Bruders Timotheus ist euch bekannt. Sobald er zu mir zurückkehrt, will ich euch mit ihm besuchen.
Napenda kuwajulisheni kwamba ndugu yetu Timotheo amekwisha funguliwa gerezani. Kama akifika hapa mapema, nitakuja naye nitakapokuja kwenu.
24 Grüßt alle eure Vorsteher und alle Heiligen! Es grüßen euch die Brüder in Italien.
Wasalimieni viongozi wenu wote pamoja na watu wa Mungu! Ndugu wa Italia wanawasalimuni.
25 Die Gnade sei mit euch allen! Amen.
Tunawatakieni nyote neema ya Mungu.

< Hebraeer 13 >