< Marqqossa 15 >

1 Malado wontara qessista halaqti dere cimatinne Muse woga tamarsizayti kummetha shango alafistara issippe zoretidi Yesusa qachi ekki efidi Philaxosas athi immida.
Asubuhi na mapema, viongozi wa makuhani, pamoja na wazee, walimu wa sheria na Baraza lote, wakafikia uamuzi. Wakamfunga Yesu, wakamchukua na kumkabidhi kwa Pilato.
2 Philaxosaykka Yesusa “Ne Ayhudata kawo?” gi ooychidees. Yesusakka “Ee ne gida mala” gidi izas zaridees.
Pilato akamuuliza, “Je, wewe ndiye Mfalme wa Wayahudi?” Yesu akajibu, “Wewe umesema.”
3 Qessista halaqatikka daro yoho iza bolla shisi motida.
Viongozi wa makuhani wakamshtaki kwa mambo mengi.
4 Philaxosay qass “Ne aazas malthe immikki? Hekko nena daro yon motetes” giidi qassekka oychidees.
Pilato akamuuliza tena, “Je, huna la kujibu? Tazama ni mashtaka mangapi wanayaleta juu yako.”
5 Gido atin Yesusay ha7ikka izas aykkoka malthe imonta gish Pilaxosaykka malaletides.
Lakini Yesu hakujibu lolote, hivyo Pilato akashangaa.
6 Paziga ba7ale galas Pilaxosay derey birshana mala oychidade birshi yediza wogay kasse dees.
Ilikuwa desturi wakati wa Sikukuu ya Pasaka kumfungulia mfungwa yeyote ambaye watu wangemtaka.
7 Itta oothon dere bolla dendidi shemppo wodhida asatara issippe qashetida barbane getetiza issadey dees.
Wakati huo, mtu aliyeitwa Baraba alikuwa amefungwa gerezani pamoja na waasi wengine waliokuwa wametekeleza uuaji wakati wa maasi.
8 Dereykka yidi kasse dosse gididaysa izi oothana mala Philaxosa wosidees.
Ule umati wa watu ukamjia Pilato na kumwomba awafanyie kama ilivyokuwa desturi yake.
9 Pilaxosaykka istas “Ta intes Ayhude kawo birshana mala koyetii? gi ooychidees.
Pilato akawauliza, “Mnataka niwafungulie huyu Mfalme wa Wayahudi?”
10 Philaxosay hessaththo ooychiday kasse qessista halaqati Yesusa qanaten athi immidaysa eriza gishasa.
Kwa maana yeye alitambua kuwa viongozi wa makuhani walikuwa wamemtia Yesu mikononi mwake kwa ajili ya wivu.
11 Qessista halaqati qass iza olla Barbaney birsheto gi oychana mala dereza denthethida.
Lakini viongozi wa makuhani wakauchochea ule umati wa watu wamwombe awafungulie Baraba badala yake.
12 Philaxosay “Histikko inte Ayhuda kawo giza adeza wostana mala koyeti” gides.
Pilato akawauliza tena, “Basi mnataka nifanye nini na huyu mtu mnayemwita Mfalme wa Wayahudi?”
13 Issti qassekka “Kaqa kaqa” gi wasida.
Wakapiga kelele wakisema, “Msulubishe!”
14 Philaxosaykka “Ay iita oothide?” gi istta oychidees. Istti qass “Kaqa kaqa” gidi kasseppe athi wasida.
Pilato akawauliza, “Kwa nini? Amefanya kosa gani?” Lakini wao wakapiga kelele kwa nguvu zaidi, wakisema, “Msulubishe!”
15 Philaxosaykka dereza ufaysana gidi Barbane istas birshides. Yesusa garafidi kaqanas athi immidees.
Pilato, akitaka kuuridhisha ule umati wa watu, akawafungulia Baraba. Naye baada ya kuamuru Yesu achapwe mijeledi, akamtoa ili asulubishwe.
16 Wotadarati Yesusa dere harizaysa gibe ekki bidi atida wotadarata wursi shishida.
Askari wakampeleka Yesu hadi kwenye ukumbi wa ndani wa jumba la kifalme, ndio Praitorio, wakakusanya kikosi kizima cha askari.
17 Yesusa waga la7o gidida zo7o mayo mayzida; aguntha akilile xaxidi iza hu7en wothida.
Wakamvalisha Yesu joho la zambarau, wakasokota taji ya miiba, wakamvika kichwani.
18 Hessappekka “Aayhuda kawo saroy ness gido!” gishe iza sarothida.
Wakaanza kumsalimu kwa dhihaka, “Salamu, mfalme wa Wayahudi!”
19 Iza hu7e gufera shocida; iza bollakka cutida gulbatidi izas goynida.
Wakampiga kwa fimbo ya mwanzi tena na tena kichwani na kumtemea mate. Wakapiga magoti mbele yake, wakamsujudia kwa kumdhihaki.
20 Iza bolla qidhi ka7idappe guye kasse mayzida zo7o mayoza qari ekidi kase iza mayoza zari mayzidi kaqanaso eki bida.
Walipokwisha kumdhihaki, wakamvua lile joho la zambarau, wakamvika tena nguo zake. Kisha wakamtoa nje ili wakamsulubishe.
21 Alakisandrosanne Rufosa aawa Simmona getetiza issi qarena dere assi dereppe katama yizaysa Yesusa masqale wolqara ooyki tosida.
Mtu mmoja kutoka Kirene, jina lake Simoni, baba yao Aleksanda na Rufo, alikuwa anapita zake kuingia mjini kutoka shamba, nao wakamlazimisha kuubeba ule msalaba.
22 Hessafe Yesusa izas birshechay “asa hu7e guge” Golgothu getetizaso efida.
Kisha wakampeleka Yesu mpaka mahali palipoitwa Golgotha (maana yake ni Mahali pa Fuvu la Kichwa).
23 Karbe getetiza dhalera walaketida woynne caje uuyana mala izas immin izi ekonta ixidees.
Nao wakampa divai iliyochanganywa na manemane, lakini hakuinywa.
24 Hessafe guye iza kaqida, iza mayo issade issade awaysa gakanakone gidi sama yegidi gishetida.
Basi wakamsulubisha, nazo nguo zake wakagawana miongoni mwao kwa kuzipigia kura ili kuamua ni gani kila mtu ataichukua.
25 Issti iza kaqishin wonappe hezu saatte gididees.
Ilikuwa yapata saa tatu asubuhi walipomsulubisha.
26 Isstti masqale bolla xafi shishida moto qalay “Aayhude kawo” giza qaala.
Tangazo likaandikwa la mashtaka dhidi yake lenye maneno haya: “Mfalme wa Wayahudi.”
27 Izara issippe namm7u pangata issa izappe ushachara issa hadirsara kaqida.
Pamoja naye walisulubiwa wanyangʼanyi wawili, mmoja upande wake wa kuume na mwingine upande wa kushoto. [
28 Heesankka kasse maxafay “Ittatara issippe taybetidees” gida tinbite qalay poletidees.
Nayo maandiko yakatimizwa, yale yasemayo, “Alihesabiwa pamoja na watenda dhambi.]”
29 Ooggera adhi bizaytikka ba hu7e qathishe “Oy! oy! maqidasse lalada hezu galasan kexanay nene?” gidi pala cashe cayishe;
Watu waliokuwa wakipita njiani wakamtukana huku wakitikisa vichwa vyao na kusema, “Aha! Wewe ambaye utalivunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu,
30 “Anne ha7i masqale bollappe wodhada nena asha” gida.
basi shuka kutoka msalabani na ujiokoe mwenyewe!”
31 Hesathokka Qessista halaqatinne Muse woga tamarsizayti ba garsan issay issas “harata ashidees shin bena ashana danda7ibeyna” gidi iza qidhida.
Vivyo hivyo, viongozi wa makuhani pamoja na walimu wa sheria wakamdhihaki miongoni mwao wakisema, “Aliwaokoa wengine, lakini hawezi kujiokoa mwenyewe!
32 “Nu iza beydi amanana mala anne haysi kirsotosay Isra7elista kawoy ha7i masqaleppe wodho” gida. Izara kaqetidaytikka iza bolla cashe korida.
Basi huyu Kristo, huyu Mfalme wa Israeli, ashuke sasa kutoka msalabani, ili tupate kuona na kuamini.” Wale waliosulubiwa pamoja naye pia wakamtukana.
33 Usuppun satteppe oykidi uudufun sate gakaans biittay wuri dhumidees.
Ilipofika saa sita, giza liliifunika nchi yote hadi saa tisa.
34 Uddufun satte bolla Yesusay “Eelohe eelohe lama sabaqitani?” gidi qaala dhoqu histidi wasidees. Hessas birshechay “Ta Xoosso Xoosso ne tana aazas agadi” gussa.
Mnamo saa tisa, Yesu akapaza sauti, akalia, “Eloi, Eloi, lama sabakthani?” (maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”)
35 Hen gadan eqida asappe issi issi asati hessa siyidi “Eelasa xeygesikko” gida.
Baadhi ya watu waliokuwa wamesimama karibu waliposikia hayo, wakasema, “Msikieni, anamwita Eliya.”
36 Hesappe issi uray eleli bidi calida woynne caje isponje mala mishan gelithi kessidi miththa xeran qaphidi uuyana mala Yesusas shishidees. Hessafe qasse “Anne agagitte Elasay yidi iza kaqoppe wothishin nu beynna” gidees.
Mtu mmoja akaenda mbio, akachovya sifongo kwenye siki, akaiweka kwenye mwanzi na akampa Yesu ili anywe, akisema, “Basi mwacheni. Hebu tuone kama Eliya atakuja kumshusha kutoka hapo msalabani.”
37 Hessafe Yesusay qaala dhoqu histi wasidi shempo kezides.
Kisha Yesu akatoa sauti kuu, akakata roho.
38 Meqidase magalasha pude hu7era duge namm7u kezi daketidees.
Pazia la Hekalu likachanika vipande viwili kuanzia juu hadi chini.
39 Yesusa ginara eqida issi xeetu wotadara halaqay Yesusay hessaththo gita qalara wasidi shemppo kezishi beydi “Haysadey tummu Xoossa nakoshin” gidees.
Basi yule jemadari aliyekuwa amesimama hapo mbele ya msalaba wa Yesu aliposikia ile sauti yake na kuona jinsi alivyokata roho, akasema, “Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu!”
40 Hessa wode macashati hanizaysa hahon didi xeleida. Issta gidoppe Magidaleppe yida Maramane natiza Yaqobene Yossa aayo Maramira qassekka Solomira issippe deetes.
Walikuwepo pia wanawake waliokuwa wakiangalia kwa mbali. Miongoni mwao walikuwepo Maria Magdalene, na Maria mama yao Yakobo mdogo na Yose, pia na Salome.
41 Heyti macashati Galilan Yesusa kalishene izas othishe gamm7idayta. Istarakka issippe hara daro macashati Yerusalame bida.
Hawa walifuatana na Yesu na kushughulikia mahitaji yake alipokuwa Galilaya. Pia walikuwepo wanawake wengine wengi waliokuwa wamekuja pamoja naye Yerusalemu.
42 Wodey qami qami bishin Sanbatas gigetiza galasi gakidees.
Ilipofika jioni, kwa kuwa ilikuwa Siku ya Maandalizi, yaani siku moja kabla ya Sabato,
43 Dere cimata garsan bonchetida issi Armata ass Yosefo getetizaysi Xoossa kawoteth nagishe dizadey babonta Philaxossakko bidi Yesusa anha wosidees.
Yosefu wa Arimathaya, mtu aliyeheshimiwa katika Baraza, na ambaye alikuwa anautarajia Ufalme wa Mungu, akamwendea Pilato kwa ujasiri na kumwomba mwili wa Yesu.
44 Philaxosaykka izi hini wode elera hayqidaysa siyidi malaletidees. Xeetu wotadarata halaqa xeygidi izi hayqin woqa wodekkonne ooychidees.
Pilato alikuwa akijiuliza kama Yesu alikuwa amekwisha kufa. Hivyo akamwita yule jemadari, akamuuliza iwapo Yesu alikuwa amekwisha kufa.
45 Izi hayqidaysa xeetu wotadarata halaqay geshi eridappe guye Yesusa anha Yosefos immidees.
Baada ya kupata habari kutoka kwa yule jemadari kwamba kweli amekwisha kufa, Pilato akampa Yosefu ruhusa ya kuuchukua huo mwili.
46 Yosefoykka mogo mayo shamidi anha masqaleppe wothidi mogo mayon xaxidi shuchappe wocetida dufon wothidees. Duhaaththaa dunna shuchara tucidees.
Hivyo Yosefu akanunua kitambaa cha kitani safi, akaushusha mwili kutoka msalabani, akaufunga katika kile kitambaa cha kitani, na kuuweka ndani ya kaburi lililochongwa kwenye mwamba. Kisha akavingirisha jiwe kwenye ingilio la kaburi.
47 Magidaleppe yida Maramirane Yossa ayo Maramra Yesusa anha awan mogidakkon beyida.
Maria Magdalene na Maria mamaye Yose walipaona mahali pale alipolazwa.

< Marqqossa 15 >