< Luqaassa 3 >

1 Xiibaros geetettiza qeesarey kawottida tammanne ichachchantho laythan Phanxoossa Philaxosa gizays Yuda biitta haariza wode, Herdossay Galila biitta haariza wode, iza ishay piliphoossay, Ixuriyasanne Xirakkondose biitta haariza wode, Lisannyossay Sabilane biitta haariza wode,
Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberio, Pontio Pilato akiwa mtawala wa Uyahudi, Herode akiwa mfalme wa Galilaya, Filipo ndugu yake akiwa mfalme wa Iturea na nchi ya Trakoniti, na Lisania akiwa mfalme wa Abilene,
2 Haanaynne Qayafay waana qeeseta gidida wode Xoossa qaalay baazo biittan diza Zakarassa na Yanisakko yides.
nao Anasi na Kayafa wakiwa makuhani wakuu, neno la Mungu likamjia Yohana, mwana wa Zekaria huko jangwani.
3 Yaanisay Yordanose shoore achchan diza dereta wurson “inte nagara atto gaanas nagarappe simmidi xamaqqetite” gidi yoottides.
Akaenda katika nchi yote kandokando ya Mto Yordani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi.
4 Hessika qasse nabe Isayaasay bazon hizgidi wassiza asa koshinch “Godas oge giigissite baassidikka lo7ethite.
Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Sauti ya mtu aliaye nyikani, ‘Itengenezeni njia ya Bwana, yanyoosheni mapito yake.
5 Shoobba biittay wuri kumana guutha zumayne gita zumay wuri ziq gaana geella ogey sitta moorettida ogey lo7o gidana.
Kila bonde litajazwa, kila mlima na kilima vitashushwa. Njia zilizopinda zitanyooshwa, na zilizoparuza zitasawazishwa.
6 Asa zerethi wuri ashshizza Xoossa woliqqa beyana giidi bazon wassiza asa qaala giireth” giidi ba maxaafan xaafida mala.
Nao watu wote watauona wokovu wa Mungu.’”
7 Yanisaykka iza kushen xamaqqistana yiza asas “inteno ha shoosha nayto yaana diza Xoossa hanqqofe haakkana mala ooni intena zoridee?
Yohana akauambia ule umati wa watu uliokuwa unakuja ili kubatizwa naye, “Ninyi watoto wa nyoka! Ni nani aliyewaonya kuikimbia ghadhabu inayokuja?
8 Inte naggara oothoppe simmidayssa erisiza ootho oothite (Abramey nu aaway nuus dees) gusi aggitte gides. Xoossi bees giikko ha shuchchatappe Abrames na oothi denthaanas dandda7izayssa erite”
Basi zaeni matunda yastahiliyo toba. Wala msianze kusema mioyoni mwenu kuwa, ‘Sisi tunaye Abrahamu, baba yetu.’ Kwa maana nawaambia kuwa Mungu anaweza kumwinulia Abrahamu watoto kutoka mawe haya.
9 Beyxxey mith qanxanas miththa xaphon dees. Lo7o ayfe ayfontta iita mithi wuri qanxettidi taman yegistana.
Hata sasa shoka limeshawekwa tayari kwenye shina la kila mti. Basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.”
10 Asaykka “histtini ay oothooni” giidi oychchides.
Ule umati wa watu ukamuuliza, “Inatupasa tufanyeje basi?”
11 Yanisaykka asas “nam77u mayoy diza issi mayoy bayndda asas imo qassekka qumay dizaykka shaakkidi immo” gides.
Yohana akawaambia, “Aliye na kanzu mbili amgawie asiye nayo, naye aliye na chakula na afanye vivyo hivyo.”
12 Qaraxa shiishizayttikka xamaqqistanaas yiidi “tamarisizayso nu ay oothino?” gida.
Watoza ushuru nao wakaja ili wabatizwe, wakamuuliza, “Bwana na sisi inatupasa tufanyeje?”
13 Izikka “inte azazettidayssafe bollara qaraxa shiishoppite” gides.
Akawaambia, “Msichukue zaidi ya kiwango mlichopangiwa.”
14 Wotadarattikka “nuni qasse ay oothino” giidi oychchida. izikka “oona miishshakka gidin dafi ekkofite qassekka oonane wordon mootopite inte damozay intes giddana” gides.
Askari nao wakamuuliza, “Je, nasi inatupasa tufanye nini?” Akawaambia, “Msimdhulumu mtu wala msimshtaki mtu kwa uongo, bali mridhike na mishahara yenu.”
15 Asay Yanisa beyidi haysi kirstossa? giidi ba wozinan sidhides.
Watu walikuwa na matazamio makubwa. Wakawa wanajiuliza mioyoni mwao iwapo Yohana angeweza kuwa ndiye Kristo.
16 Yanisaykka wursos “tani intena haathan xamaqays gido attin ta iza caamma birshaanas besoontta tappe aadhdhizaddey yaana. izi intena Xillo Ayaananne taman xamaqqana.
Yohana akawajibu akawaambia, “Mimi nawabatiza kwa maji. Lakini atakuja aliye na nguvu kuniliko mimi, ambaye sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake. Yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
17 Kath suragiza layiday iza kushen dees. Balezza kumetha geeshshanna gistteza qasse di7en qollana gafezakka to7onta taman xuugana” gides.
Pepeto lake liko mkononi, tayari kusafisha sakafu yake ya kupuria na kuikusanya ngano ghalani, lakini makapi atayateketeza kwa moto usiozimika.”
18 Yanissay asa hara dumma dumma zore qaalara minnithethi zorishe mishrachcho qaala yoottides.
Basi, kwa maonyo mengine mengi Yohana aliwasihi na kuwahubiria watu Habari Njema.
19 Gido attin Galila biitta haariza Herdoosay ba isha machcho Herooddiyaado ekkida gishine hara daro iita oothida gish Yanisay iza hanqqida gish
Lakini Yohana alipomkemea Mfalme Herode kuhusu uhusiano wake na Herodia, mke wa ndugu yake, na maovu mengine aliyokuwa amefanya,
20 kase mooro bolla hara gujjidi Herdossay Yaanisa woyne keeththan yegides.
Herode aliongezea jambo hili kwa hayo mengine yote: alimfunga Yohana gerezani.
21 Asay xamaqqettidappe guyyen Yesussaykka xamaqqetides, izi woosishin saloy doyettides.
Baada ya watu wote kubatizwa, Yesu naye akabatizwa. Naye alipokuwa akiomba, mbingu zilifunguka.
22 Xillo Ayyaanaykka wole milattida iza bolla wodhides. “saloppe ta dosiza nay nena nenan tani ufa7istays” giza qaalay yides.
Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa umbo kama la hua, nayo sauti kutoka mbinguni ikasema: “Wewe ni Mwanangu mpendwa; nami nimependezwa nawe sana.”
23 Yesussay Xoossa ootho oykkishn laythay izas heezu tamu laytha mala gidana. Asaykka izi Yosefo na, Eelle na,
Yesu alikuwa na umri wa miaka thelathini alipoanza huduma yake. Alikuwa akidhaniwa kuwa mwana wa Yosefu, Yosefu alikuwa mwana wa Eli,
24 Maati na, Lewe na, Milki na, Yuda na, Yosefo na,
Eli alikuwa mwana wa Mathati, Mathati alikuwa mwana wa Lawi, Lawi alikuwa mwana wa Melki, Melki alikuwa mwana wa Yanai, Yanai alikuwa mwana wa Yosefu,
25 Matattiyu na, Amoxxe na, Nahome na, Isilime na, Naage na,
Yosefu alikuwa mwana wa Matathia, Matathia alikuwa mwana wa Amosi, Amosi alikuwa mwana wa Nahumu, Nahumu alikuwa mwana wa Esli, Esli alikuwa mwana wa Nagai,
26 Maate na, Matatiyo na, Semeye na, Yosefo na, Yuda na,
Nagai alikuwa mwana wa Maathi, Maathi alikuwa mwana wa Matathia, Matathia alikuwa mwana wa Semeini, Semeini alikuwa mwana wa Yoseki, Yoseki alikuwa mwana wa Yoda,
27 Yoonane na, Reese na, zerubbaabeele na, Selatiyale na, Nere na,
Yoda alikuwa mwana wa Yoanani, Yoanani alikuwa mwana wa Resa, Resa alikuwa mwana wa Zerubabeli, Zerubabeli alikuwa mwana wa Shealtieli, Shealtieli alikuwa mwana wa Neri,
28 Milki na, hadi na, Yosa na, Qoosame na, Elimodamme na,
Neri alikuwa mwana wa Melki, Melki alikuwa mwana wa Adi, Adi alikuwa mwana wa Kosamu, Kosamu alikuwa mwana wa Elmadamu, Elmadamu alikuwa mwana wa Eri,
29 Yose na, Elazare na, Yorame na, Maaxate na, Eelle na,
Eri alikuwa mwana wa Yoshua, Yoshua alikuwa mwana wa Eliezeri, Eliezeri alikuwa mwana wa Yorimu, Yorimu alikuwa mwana wa Mathati, Mathati alikuwa mwana wa Lawi,
30 Simoona na, Yuda na, Yosefo na, Yooname na, Eliyaqqeeme na,
Lawi alikuwa mwana wa Simeoni, Simeoni alikuwa mwana wa Yuda, Yuda alikuwa mwana wa Yosefu, Yosefu alikuwa mwana wa Yonamu, Yonamu alikuwa mwana wa Eliakimu, Eliakimu alikuwa mwana wa Melea,
31 Meliya na, Maaxate na, Naatane na, Daawute na,
Melea alikuwa mwana wa Mena, Mena alikuwa mwana wa Matatha, Matatha alikuwa mwana wa Nathani, Nathani alikuwa mwana wa Daudi,
32 Iseeye na, Iyobede na, Bo7eeze na, Selimoona na, Ne7asoone na,
Daudi alikuwa mwana wa Yese, Yese alikuwa mwana wa Obedi, Obedi alikuwa mwana wa Boazi, Boazi alikuwa mwana wa Salmoni, Salmoni alikuwa mwana wa Nashoni,
33 Amnaddabe na, Aarame na, Aaronne na, Esrome na, Faareesse na, Yuda na,
Nashoni alikuwa mwana wa Aminadabu, Aminadabu alikuwa mwana wa Aramu, Aramu alikuwa mwana wa Hesroni, Hesroni alikuwa mwana wa Peresi, Peresi alikuwa mwana wa Yuda,
34 Yaqoobe na, Yisaqqa na, Abrame na, tara na, Nakore na,
Yuda alikuwa mwana wa Yakobo, Yakobo alikuwa mwana wa Isaki, Isaki alikuwa mwana wa Abrahamu, Abrahamu alikuwa mwana wa Tera, Tera alikuwa mwana wa Nahori,
35 Seerohe na, Raggawe na, Faaleeqqe na, Aabere na, Saala na,
Nahori alikuwa mwana wa Serugi, Serugi alikuwa mwana wa Reu, Reu alikuwa mwana wa Pelegi, Pelegi alikuwa mwana wa Eberi, Eberi alikuwa mwana wa Sala,
36 Qayneme na, Aarfakkisidde na, Seeme na, Nohe na, Lamehe na,
Sala alikuwa mwana wa Kenani, Kenani alikuwa mwana wa Arfaksadi, Arfaksadi alikuwa mwana wa Shemu, Shemu alikuwa mwana wa Noa, Noa alikuwa mwana wa Lameki,
37 Matosala na, Henokke na, Yarede na, Malali7eele na, Qaynane na,
Lameki alikuwa mwana wa Methusela, Methusela alikuwa mwana wa Enoki, Enoki alikuwa mwana wa Yaredi, Yaredi alikuwa mwana wa Mahalaleli, Mahalaleli alikuwa mwana wa Kenani,
38 Henosse na Seete na Addamme na, Xoossa na, milatides.
Kenani alikuwa mwana wa Enoshi, Enoshi alikuwa mwana wa Sethi, Sethi alikuwa mwana wa Adamu, Adamu alikuwa mwana wa Mungu.

< Luqaassa 3 >