< Tite 3 >

1 Avertis-les d’être soumis aux princes et aux puissances, d’obéir au commandement, d’être prêts à toute bonne œuvre;
Wakumbushe watu kuwastahi watawala na wenye mamlaka, kuwatii na kuwa tayari kwa kila namna kutenda mambo yote mema.
2 De ne diffamer personne, de fuir les contestations, d’être modérés, et de montrer la plus grande douceur envers tous les hommes.
Waambie wasimtukane mtu yeyote; bali waishi kwa amani na masikizano, wawe daima wapole kwa kila mtu.
3 Car nous étions nous-mêmes autrefois insensés, incrédules, égarés, esclaves de toute sorte de désirs et de voluptés, vivant dans la malignité et l’envie, haïssables, nous haïssant les uns les autres.
Maana, wakati mmoja sisi tulikuwa wapumbavu, wakaidi na wapotovu. Tulikuwa watumwa wa tamaa na anasa za kila aina. Tuliishi maisha ya uovu na wivu; watu walituchukia nasi tukawachukia.
4 Mais lorsqu’est apparue la bonté et l’humanité de notre Sauveur Dieu,
Lakini wakati wema na upendo wa Mungu, Mwokozi wetu, ulipofunuliwa,
5 Ce n’est point par les œuvres de sa justice que nous avons faites qu’il nous a sauvés, mais selon sa miséricorde, c’est par le baptême de régénération et de renouvellement de l’Esprit-Saint,
alituokoa. alituokoa si kwa sababu ya jambo lolote jema tulilotenda sisi, bali alituokoa kwa sababu ya huruma yake, kwa njia ya Roho Mtakatifu anayetujalia tuzaliwe upya na kuwa na maisha mapya kwa kutuosha kwa maji.
6 Qu’il a répandu sur nous abondamment par Jésus-Christ notre Sauveur,
Mungu alitumiminia Roho Mtakatifu bila kipimo kwa njia ya Yesu Kristo, Mwokozi wetu,
7 Afin que, justifiés par sa grâce, nous soyons héritiers selon notre espérance, de la vie éternelle. (aiōnios g166)
ili kwa neema yake tupate kukubaliwa kuwa waadilifu na kuupokea uzima wa milele tunaoutumainia. (aiōnios g166)
8 C’est une vérité certaine, et je veux que tu assures fortement ces choses, afin que ceux qui croient en Dieu aient soin de se mettre à la tête des bonnes œuvres. Voilà ce qui est bon et utile aux hommes.
Jambo hili ni kweli. Ninakutaka uyatilie mkazo mambo haya, ili wale wanaomwamini Mungu, wawe na hamu ya kuutumia wakati wao katika kutenda mema, ambayo ni mambo mazuri na ya manufaa kwa watu.
9 Quant aux questions imprudentes, aux généalogies, aux contentions, aux disputes sur la loi, évite-les; car elles sont inutiles et vaines.
Lakini jiepushe na ubishi wa kipumbavu, ugomvi na mabishano juu ya Sheria. Mambo hayo hayana faida yoyote na ni ya bure tu.
10 Evite un homme hérétique, après une première et une seconde admonition;
Mtu anayesababisha mafarakano mpe onyo la kwanza na la pili, kisha achana naye.
11 Sachant qu’un tel homme est perverti, et qu’il pèche, puisqu’il est condamné par son propre jugement.
Wajua kwamba mtu wa namna hiyo amepotoka kabisa, na dhambi zake zathibitisha kwamba amekosea.
12 Lorsque je t’aurai envoyé Artémas ou Tychique, hâte-toi de venir près de moi à Nicopolis; car j’ai résolu d’y passer l’hiver.
Baada ya kumtuma kwako Artema au Tukiko, fanya bidii kuja Nikopoli unione, maana nimeamua kukaa huko wakati wa majira ya baridi.
13 Aie soin d’envoyer devant Zénas, le docteur de la loi, et Appollo, et que rien ne leur manque.
Jitahidi kumsaidia mwana sheria Zena na Apolo ili waweze kuanza ziara zao na uhakikishe kwamba wana kila kitu wanachohitaji.
14 Et que les nôtres aussi apprennent à se mettre à la tête des bonnes œuvres, lorsque la nécessité le demande, afin qu’ils ne soient pas sans fruit.
Ni lazima watu wetu wajifunze kuutumia wakati wao katika kutenda mema ili wasaidie katika mahitaji ya kweli, na maisha yao yawe ya kufaa.
15 Tous ceux qui sont avec moi vous saluent: saluez ceux qui nous aiment dans la foi. La grâce de Dieu soit avec vous tous. Amen.
Watu wote walio pamoja nami wanakusalimu. Wasalimu rafiki zetu katika imani. Nawatakieni nyote neema ya Mungu.

< Tite 3 >