< Ruth 1 >

1 Aux jours d’un juge, lorsque les juges gouvernaient, il y eut une famine sur la terre. Or, un homme s’en alla de Bethléhem de Juda, pour voyager dans le pays de Moab, avec sa femme et ses deux enfants.
Wakati Waamuzi walipotawala Israeli, kulikuwa na njaa katika nchi. Mtu mmoja kutoka nchi ya Bethlehemu ya Yuda, pamoja na mke wake na wanawe wawili, akaenda kuishi katika nchi ya Moabu.
2 Cet homme s’appelait Elimélech, sa femme Noémi, et ses deux fils, l’un Mahalon et l’autre Chélion; ils étaient Ephrathéens de Bethléhem de Juda. Or, étant entrés dans le pays de Moab, ils y demeurèrent.
Mtu huyu aliitwa Elimeleki, mkewe aliitwa Naomi, na hao wanawe wawili waliitwa Maloni na Kilioni. Walikuwa Waefrathi kutoka Bethlehemu ya Yuda. Wakaenda katika nchi ya Moabu, wakaishi huko.
3 Et Elimélech, mari de Noémi, mourut; et elle resta avec ses fils,
Elimeleki mumewe Naomi akafa, hivyo Naomi akabaki na wanawe wawili.
4 Qui prirent des femmes moabites, dont l’une s’appelait Orpha, et l’autre Ruth. Et ils demeurèrent là pendant dix ans,
Nao wakaoa wanawake Wamoabu, jina la mmoja aliitwa Orpa, na wa pili aliitwa Ruthu. Baada ya kama miaka kumi,
5 Puis ils moururent tous deux, c’est-à-dire Mahalon et Chélion: et cette femme resta seule privée de ses deux enfants et de son mari.
Maloni na Kilioni pia wakafa. Basi Naomi akabaki hana mume wala wanawe wawili.
6 Elle se leva donc pour aller du pays de Moab dans sa patrie avec l’une et l’autre de ses belles-filles; car elle avait appris que le Seigneur avait regardé son peuple et lui avait donné de la nourriture.
Aliposikia akiwa huko Moabu kwamba Bwana amewasaidia watu wake kwa kuwapa chakula, Naomi na wakweze wakajiandaa kurudi nyumbani.
7 C’est pourquoi elle sortit du lieu de son pèlerinage avec l’une et l’autre de ses belles-filles; et s’étant déjà mise en chemin pour retourner dans la terre de Juda,
Yeye na wakweze wawili wakaondoka pale walipokuwa wakiishi na kushika njia kurudi nchi ya Yuda.
8 Elle leur dit: Allez en la maison de votre mère, que le Seigneur vous fasse miséricorde, comme vous l’avez faite à ceux qui sont morts, et à moi.
Ndipo Naomi akawaambia wale wakwe zake wawili, “Rudini, kila mmoja wenu nyumbani kwa mama yake. Bwana na awatendee fadhili kama mlivyowatendea hao waliofariki, na pia mimi.
9 Qu’il vous donne de trouver du repos dans les maisons des maris qui doivent vous échoir. Et elle les embrassa. Et elles, la voix élevée, se mirent à pleurer,
Bwana na amjalie kila mmoja wenu maisha mema nyumbani kwa mume mwingine.” Kisha akawabusu, nao wakalia kwa sauti kubwa,
10 Et à dire: Nous irons avec vous chez votre peuple.
wakamwambia, “Tutarudi pamoja na wewe nyumbani kwa watu wako.”
11 Noémi leur répondit: Retournez, mes filles, pourquoi venez-vous avec moi? Est-ce que j’ai encore des fils dans mon sein, pour que vous puissiez espérer de moi des maris?
Lakini Naomi akasema, “Rudini nyumbani, binti zangu. Kwa nini mnifuate? Je, mimi nitaweza tena kuwa na wana wengine ambao wataweza kuwaoa ninyi?
12 Retournez, mes filles, et allez-vous-en; je suis déjà usée de vieillesse, et nullement propre au lien conjugal. Quand même je pourrais concevoir cette nuit et enfanter des fils,
Rudini nyumbani, binti zangu; mimi ni mzee kiasi kwamba siwezi kumpata mume mwingine. Hata kama ningefikiria kuwa bado kuna tumaini kwangu, hata kama ningekuwa na mume usiku huu na kuwazaa wana,
13 Si vous vouliez les attendre jusqu’à ce qu’ils eussent grandi et achevé les années de puberté vous seriez vieilles avant de les épouser. Non, mes filles, je vous prie; parce que votre angoisse pèse trop sur moi, et la main du Seigneur est sortie contre moi.
je, mngesubiri mpaka wakue? Mngebakia bila kuolewa mkiwasubiri? La, hasha, binti zangu. Nimepata uchungu kuliko ninyi, kwa sababu mkono wa Bwana umekuwa kinyume nami!”
14 Ainsi, la voix élevée, elles se mirent de nouveau à pleurer. Orpha embrassa sa belle-mère, et s’en retourna; Ruth s’attacha à sa belle-mère;
Kisha wakalia tena kwa sauti. Orpa akambusu mama mkwe wake, akaenda zake, lakini Ruthu akaambatana naye.
15 Et Noémi lui dit: Voilà ta belle-sœur qui est retournée à son peuple et à ses dieux, va avec elle.
Naomi akamwambia, “Tazama, mwenzako anarejea kwa watu wake na kwa miungu yake. Rudi pamoja naye.”
16 Ruth répondit: N’insistez point auprès de moi, pour que je vous quitte et que je m’en aille, car partout où vous irez, j’irai; et là où vous demeurerez, moi aussi je demeurerai. Votre peuple est mon peuple, et votre Dieu mon Dieu.
Lakini Ruthu akajibu, “Usinisihi nikuache au niache kukufuata. Utakakokwenda nami nitakwenda, na wewe utakapoishi nitaishi. Watu wako watakuwa watu wangu, na Mungu wako atakuwa Mungu wangu.
17 Et la terre qui vous recevra mourante, j’y mourrai; et c’est là que je prendrai le lieu de ma sépulture. Que le Seigneur me fasse ceci et qu’il ajoute cela, si ce n’est pas la mort seule qui me sépare de vous.
Pale utakapofia nami nitafia hapo, na papo hapo nitazikwa. Bwana na aniadhibu vikali, kama kitu kingine chochote kitanitenga nawe isipokuwa kifo.”
18 Noémi voyant donc que Ruth avait opiniâtrement résolu d’aller avec elle, ne voulut plus s’y opposer, ni lui persuader de retourner vers les siens.
Naomi alipotambua kwamba Ruthu amenuia kufuatana naye, hakuendelea kumsihi tena.
19 Et elles partirent ensemble, et elles vinrent à Bethléhem. Entrées dans la ville, le bruit s’en répandit promptement parmi tous les habitants, et les femmes disaient: Voilà cette Noémi.
Kwa hiyo hao wanawake wawili wakaondoka, wakafika Bethlehemu. Walipofika Bethlehemu, mji mzima ulitaharuki, wanawake wakashangaa, wakasema, “Huyu aweza kuwa ni Naomi?”
20 Noémi leur dit: Ne m’appelez point Noémi (c’est-à-dire belle); mais appelez-moi Mara (c’est-à-dire amère), parce que le Tout-Puissant m’a remplie d’une grande amertume.
Akawaambia, “Msiniite tena Naomi, niiteni Mara, kwa sababu Mwenyezi amenitendea mambo machungu sana.
21 Je suis sortie pleine, et le Seigneur m’a ramenée vide. Pourquoi donc m’appelez-vous Noémi, moi que le Seigneur a humiliée et que le Tout-Puissant a affligée.
Mimi niliondoka hali nimejaa, lakini Bwana amenirudisha mtupu. Kwa nini kuniita Naomi? Bwana amenitendea mambo machungu; Mwenyezi ameniletea msiba.”
22 Noémi vint donc avec Ruth, la Moabite, sa belle-fille, de la terre de son pèlerinage; et elle revint à Bethléhem, quand on commençait à moissonner les orges.
Kwa hiyo Naomi alirudi pamoja na Ruthu Mmoabu mkwe wake, nao wakafika Bethlehemu mwanzoni mwa kuvuna shayiri.

< Ruth 1 >