< Romains 11 >
1 Je dis donc: Est-ce que Dieu a rejeté son peuple? Non, sans doute; car moi-même je suis Israélite, de la race d’Abraham, de la tribu du Benjamin;
Basi nauliza: Je, Mungu amewakataa watu wake? La, hasha! Mimi mwenyewe ni Mwisraeli, tena uzao wa Abrahamu kutoka kabila la Benyamini.
2 Dieu n’a point rejeté son peuple qu’il a connu dans sa prescience. Ne savez-vous pas ce que l’Ecriture dit d’Elie, comment il interpelle Dieu contre Israël, disant:
Mungu hajawakataa watu wake, ambao yeye aliwajua tangu mwanzo. Je, hamjui yale Maandiko yasemayo kuhusu Eliya, jinsi alivyomlalamikia Mungu kuhusu Israeli?
3 Seigneur, ils ont tué vos prophètes, démoli vos autels; et moi, je suis resté seul, et ils recherchent mon âme?
Alisema, “Bwana, wamewaua manabii wako na kuzibomoa madhabahu zako, nimebaki mimi peke yangu, nao wanataka kuniua?”
4 Mais que lui dit la réponse divine? Je me suis réservé sept mille hommes qui n’ont point fléchi le genou devant Baal.
Je, Mungu alimjibuje? “Nimejibakizia watu elfu saba ambao hawajapiga magoti kumwabudu Baali.”
5 De même donc, en ce temps aussi, un reste a été sauvé, selon l’élection de la grâce.
Vivyo hivyo pia, sasa wapo mabaki waliochaguliwa kwa neema ya Mungu.
6 Mais si c’est par la grâce, ce n’est donc point par les œuvres; autrement la grâce ne serait plus grâce.
Lakini ikiwa wamechaguliwa kwa neema, si tena kwa msingi wa matendo. Kama ingekuwa kwa matendo, neema isingekuwa neema tena.
7 Qu’est-il donc arrivé? Ce que cherchait Israël, il ne l’a pas trouvé; mais ceux qui ont été choisis l’ont trouvé; les autres ont été aveuglés,
Tuseme nini basi? Kile kitu ambacho Israeli alikitafuta kwa bidii hakukipata. Lakini waliochaguliwa walikipata. Waliobaki walifanywa wagumu,
8 Selon qu’il est écrit: Dieu leur a donné jusqu’à ce jour un esprit de torpeur; des yeux pour ne point voir, et des oreilles pour ne point entendre.
kama ilivyoandikwa: “Mungu aliwapa bumbuazi la mioyo, macho ili wasiweze kuona, na masikio ili wasiweze kusikia, hadi leo.”
9 David dit encore: Que leur table devienne pour eux lacet, piège, scandale et rétribution.
Naye Daudi anasema: “Karamu zao na ziwe tanzi na mtego wa kuwanasa, kitu cha kuwakwaza waanguke, na adhabu kwao.
10 Que leurs yeux s’obscurcissent pour qu’ils ne voient point, et faites que leur dos soit toujours courbé.
Macho yao yatiwe giza ili wasiweze kuona, nayo migongo yao iinamishwe daima.”
11 Je dis donc: Ont-ils trébuché de telle sorte qu’ils soient tombés? Point du tout. Mais par leur péché, le salut est venu aux gentils qui devaient ainsi leur donner de l’émulation.
Hivyo nauliza tena: Je, Waisraeli walijikwaa ili waanguke na kuangamia kabisa? La, hasha! Lakini kwa sababu ya makosa yao, wokovu umewafikia watu wa Mataifa, ili kuwafanya Waisraeli waone wivu.
12 Que si leur péché est la richesse du monde, et leur diminution, la richesse des gentils; combien plus encore leur plénitude?
Basi ikiwa kukosa kwao kumekuwa utajiri mkubwa kwa ulimwengu, tena kama kuangamia kwao kumeleta utajiri kwa watu wa Mataifa, kurudishwa kwao kutaleta utajiri mkuu zaidi.
13 Car je le dis à vous, gentils: Tant que je serai apôtre des gentils, j’honorerai mon ministère,
Sasa ninasema nanyi watu wa Mataifa. Maadamu mimi ni mtume kwa watu wa Mataifa, naitukuza huduma yangu
14 M’efforçant d’exciter l’émulation de ceux de mon sang, et d’en sauver quelques-uns.
ili kuwafanya watu wangu waone wivu na hivyo kuwaokoa baadhi yao.
15 Car si leur perte est la réconciliation du monde, que sera leur rappel, sinon une résurrection?
Kwa kuwa ikiwa kukataliwa kwao ni kupatanishwa kwa ulimwengu, kukubaliwa kwao si kutakuwa ni uhai baada ya kufa?
16 Que si les prémices sont saintes, la masse l’est aussi; et si la racine est sainte, les rameaux aussi.
Kama sehemu ya donge la unga uliotolewa kuwa limbuko ni mtakatifu, basi unga wote ni mtakatifu, nalo shina kama ni takatifu, vivyo hivyo na matawi nayo.
17 Si donc quelques-uns des rameaux ont été rompus, et si toi, qui n’étais qu’un olivier sauvage, tu as été enté en eux et fait participant de la racine et de la graisse de l’olivier,
Lakini kama baadhi ya matawi yalikatwa, nawe chipukizi la mzeituni mwitu ukapandikizwa mahali pao ili kushiriki unono pamoja na matawi mengine kutoka shina la mzeituni,
18 Ne te glorifie point aux dépens des rameaux. Que si tu te glorifies, sache que tu ne portes point la racine, mais que c’est la racine qui te porte.
basi usijivune juu ya hayo matawi. Kama ukijivuna, kumbuka jambo hili: si wewe unayelishikilia shina, bali ni shina linalokushikilia wewe.
19 Tu diras, sans doute: Les rameaux ont été brisés pour que je fusse enté.
Basi utasema, “Matawi yale yalikatwa ili nipate kupandikizwa katika hilo shina.”
20 Fort bien. C’est à cause de leur incrédulité qu’ils ont été rompus. Pour toi, tu demeures ferme par ta foi, ne cherche pas à t’élever, mais crains.
Hii ni kweli. Matawi hayo yalikatwa kwa sababu ya kutokuamini kwake, lakini wewe umesimama tu kwa sababu ya imani. Kwa hiyo usijivune, bali simama kwa kuogopa.
21 Car si Dieu n’a pas épargné les rameaux naturels, il pourra bien ne pas t’épargner toi-même.
Kwa maana kama Mungu hakuyahurumia matawi ya asili, wala hatakuhurumia wewe.
22 Vois donc la bonté et la sévérité de Dieu: sa sévérité envers ceux qui sont tombés, et sa bonté envers toi, si toutefois tu demeures ferme dans cette bonté; autrement tu seras aussi retranché.
Angalia basi wema na ukali wa Mungu: Kwa wale walioanguka, ukali, bali kwako wewe wema wa Mungu, kama utadumu katika wema wake. La sivyo, nawe utakatiliwa mbali.
23 Mais eux-mêmes, s’ils ne demeurent point dans l’incrédulité, seront entés; car Dieu est puissant pour les enter de nouveau.
Wao nao wasipodumu katika kutokuamini kwao, watapandikizwa tena kwenye shina, kwa maana Mungu anao uwezo wa kuwapandikiza tena kwenye hilo shina.
24 En effet, si tu as été coupé de l’olivier sauvage, ta tige naturelle, et enté contre nature sur l’olivier franc, à combien plus forte raison, ceux qui sont les rameaux naturels seront-ils entés sur leur propre olivier?
Ikiwa wewe ulikatwa kutoka kile ambacho kwa asili ni mzeituni mwitu na kupandikizwa kinyume cha asili kwenye mzeituni uliopandwa, si rahisi zaidi matawi haya ya asili kupandikizwa tena kwenye shina lake la mzeituni!
25 Car je ne veux pas, mes frères, que vous ignoriez ce mystère ( afin que vous ne soyez pas sages à vos propres yeux), qu’une partie d’Israël est tombée dans l’aveuglement, jusqu’à ce que la plénitude des gentils soit entrée;
Ndugu zangu, ili msije mkajidai kuwa wenye hekima kuliko mlivyo, nataka mfahamu siri hii: Ugumu umewapata Israeli kwa sehemu hadi idadi ya watu wa Mataifa watakaoingia itimie.
26 Et qu’ainsi tout Israël soit sauvé, selon qu’il est écrit: Il viendra de Sion celui qui doit délivrer, et qui doit bannir l’impiété de Jacob.
Hivyo Israeli wote wataokolewa. Kama ilivyoandikwa: “Mkombozi atakuja kutoka Sayuni; ataondoa kutokumcha Mungu katika Yakobo.
27 Et ce sera là mon alliance avec eux quand j’aurai effacé leurs péchés.
Hili ndilo agano langu nao nitakapoziondoa dhambi zao.”
28 Il est vrai que, selon l’Evangile, ils sont ennemis à cause de vous; mais, selon l’élection, ils sont très aimés à cause de leurs pères.
Kwa habari ya Injili, wao ni adui wa Mungu kwa ajili yenu, lakini kuhusu kule kuteuliwa kwao ni wapendwa, kwa ajili ya mababa zao wa zamani,
29 Parce que les dons et la vocation de Dieu sont sans repentir.
kwa maana akishawapa watu karama, Mungu haziondoi, wala wito wake.
30 Comme donc autrefois vous-mêmes n’avez pas cru à Dieu, et que maintenant vous avez obtenu miséricorde à cause de leur incrédulité
Kama vile ninyi wakati fulani mlivyokuwa waasi kwa Mungu lakini sasa mmepata rehema kwa sababu ya kutokutii kwao,
31 Ainsi eux maintenant n’ont pas cru, pour que miséricorde vous fût faite, et qu’à leur tour ils obtiennent miséricorde.
hivyo nao Waisraeli wamekuwa waasi ili kwamba wao nao sasa waweze kupata rehema kwa ajili ya rehema za Mungu kwenu.
32 Car Dieu a renfermé tout dans l’incrédulité, pour faire miséricorde à tous. (eleēsē )
Kwa maana Mungu amewafunga wanadamu wote kwenye kuasi ili apate kuwarehemu wote. (eleēsē )
33 Ô profondeur des trésors de la sagesse et de la science de Dieu! Que ses jugements sont incompréhensibles et ses voies impénétrables!
Tazama jinsi kilivyo kina cha utajiri wa hekima na maarifa ya Mungu! Tazama jinsi ambavyo hukumu zake hazichunguziki, na ambavyo njia zake zisivyotafutikana!
34 Car qui a connu la pensée du Seigneur? ou qui a été son conseiller?
“Ni nani aliyeyafahamu mawazo ya Bwana? Au ni nani ambaye amekuwa mshauri wake?”
35 Ou qui, le premier, lui a donné, et sera rétribué?
“Au ni nani aliyempa chochote ili arudishiwe?”
36 Puisque c’est de lui, et par lui, et en lui, que sont toutes choses; à lui la gloire dans les siècles. Amen. (aiōn )
Kwa maana vitu vyote vyatoka kwake, viko kwake na kwa ajili yake. Utukufu ni wake milele! Amen. (aiōn )