< Psaumes 75 >
1 Pour la fin. Ne corrompez pas. Psaume d’un cantique d’Asaph. Nous vous louerons, ô Dieu, nous louerons, et nous invoquerons votre nom. Nous raconterons vos merveilles.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Zaburi ya Asafu. Wimbo. Ee Mungu, tunakushukuru, tunakushukuru wewe, kwa kuwa jina lako li karibu; watu husimulia matendo yako ya ajabu.
2 Lorsque j’aurai pris mon temps, c’est moi qui jugerai les justices.
Unasema, “Ninachagua wakati maalum; ni mimi nihukumuye kwa haki.
3 La terre s’est fondue, et tous ceux qui y habitent. C’est moi qui ai affermi ses colonnes.
Wakati dunia na watu wake wote inapotetemeka, ni mimi ninayezishikilia nguzo zake imara.
4 J’ai dit aux hommes iniques: N’agissez pas iniquement; et à ceux qui pèchent: N’élevez pas votre corne.
Kwa wale wenye majivuno ninasema, ‘Msijisifu tena,’ kwa wale waovu, ‘Msiinue pembe zenu.
5 N’élevez pas en haut votre corne: ne dites pas contre Dieu d’iniquité;
Msiinue pembe zenu dhidi ya mbingu; msiseme kwa shingo zilizonyooshwa.’”
6 Parce que ni de l’Orient, ni de l’Occident, ni des montagnes désertes, il ne vous viendra des secours,
Hakuna yeyote atokaye mashariki wala magharibi au kutoka jangwani awezaye kumkweza mwanadamu.
7 Car c’est Dieu qui est juge. Il humilie celui-ci et il exalte celui-là;
Bali Mungu ndiye ahukumuye: Humshusha huyu na kumkweza mwingine.
8 Parce qu’un calice de vin pur est dans la main du Seigneur, calice plein d’un mélange.
Mkononi mwa Bwana kuna kikombe kilichojaa mvinyo unaotoka povu uliochanganywa na vikolezo; huumimina, nao waovu wote wa dunia hunywa mpaka tone la mwisho.
9 Pour moi, j’annoncerai à jamais, je chanterai le Dieu de Jacob.
Bali mimi, nitatangaza hili milele; nitaimba sifa kwa Mungu wa Yakobo.
10 Et je briserai les cornes des pécheurs; et les cornes des justes seront élevées.
Nitazikatilia mbali pembe za waovu wote, bali pembe za wenye haki zitainuliwa juu.