< Psaumes 69 >
1 Pour la fin, pour ceux qui seront changés, par David. Sauvez-moi, ô Dieu, parce que des eaux sont entrées dans mon âme.
Uniokoe, Mungu; maana maji yameweka uhai wangu hatarini.
2 Je suis enfoncé dans une boue profonde et sans consistance. Je suis venu dans la profondeur de la mer, et une tempête m’a submergé.
Ninazama kwenye kina cha matope, pasipo na hahari pa kusimama; nimekuja kwenye kina kirefu cha maji, ambako mafuriko yananifunika.
3 Je me suis fatigué en criant, ma gorge est devenue enrouée: mes yeux défaillent, pendant que j’espère en mon Dieu.
Nimechoka sana kwa kulia kwangu; koo langu ni kavu; macho yangu yanafifia wakati namngoja Mungu wangu.
4 Ils se sont multipliés plus que les cheveux de ma tête, ceux qui me haïssent sans sujet. Ils se sont fortifiés, ceux qui me persécutent injustement; ce que je n’avais pas pris, je l’ai pourtant payé.
Wale wanichukiao bila sababu wako zaidi ya nywele za kichwa changu; wale ambao wangeweza kuniua, wakiwa adui zangu kwa sababu zisizo sahihi, ni wengi mno; wanalazimisha nirudishe kile ambacho sijaiba.
5 Ô Dieu, c’est vous qui savez ma folie; et mes péchés ne vous sont point cachés.
Mungu, wewe unaujua ujinga wangu, na dhambi zangu hazifichiki kwako.
6 Qu’ils ne rougissent pas à cause de moi, ceux qui vous attendent, Seigneur, Seigneur des armées. Qu’ils ne soient pas confondus à mon sujet, ceux qui vous cherchent, ô Dieu d’Israël.
Usiwaache wale wanao kungoja wewe waaibishwe kwa sababu yangu, Bwana Yahwe wa majeshi; usiwaache wale wanaokutafuta wewe wadharauliwe kwa sababu yangu, Mungu wa Israeli.
7 Puisque c’est à cause de vous que j’ai souffert l’opprobre, et que la confusion a couvert ma face.
Kwa ajili yako nimestahimili lawama; aibu imeufunika uso wangu.
8 Je suis devenu étranger à mes frères, un inconnu aux fils de ma mère.
Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu, nisiye fahamika wala kuaminika kwa watoto wa mama yangu.
9 Parce que le zèle de votre maison m’a dévoré, et que les outrages de ceux qui vous insultaient sont tombés sur moi.
Kwa maana bidii ya nyumba yako imenila, na laumu zao wanao kulaumu wewe zimeniangukia mimi.
10 J’ai couvert mon âme dans le jeûne, et on m’en a fait un sujet d’opprobre.
Wakati nilipolia na kutokula chakula, walinitukana.
11 Et j’ai pris pour mon vêtement un cilice, et je suis devenu pour eux un proverbe.
Nilipoteneneza mavazi ya gunia, nikawa kituko kwao.
12 Ceux qui étaient assis à la porte de la ville parlaient contre moi, et ceux qui buvaient du vin me chantaient en dérision.
Wale wakaao katika lango la mji huniseng'enya; mimi ni wimbo wa walevi.
13 Pour moi, je vous adresse ma prière, Seigneur; c’est le temps de votre bienveillance, ô Dieu.
Lakini kwangu mimi, maombi yangu ni kwako, Yahwe, wakati ambao wewe utayapokea; unijibu katika uaminifu wa wokovu wako.
14 Retirez-moi de la fange, afin que je n’y demeure pas enfoncé; délivrez-moi de ceux qui me haïssent, et du fond des eaux.
Unitoe matopeni, na usiniache nizame; uniondoe mbali na wale wanaonichukia na uniokoe katika kina cha maji.
15 Qu’une tempête d’eau ne me submerge pas, qu’un abîme ne m’engloutisse pas; qu’un puits ne referme pas sa bouche sur moi.
Usiache mafuliko ya maji yanielemee, wala kina kisinimeze. Usiache mdomo wa shimo unimeze.
16 Exaucez-moi, Seigneur, parce que votre miséricorde est bienfaisante; selon la multitude de vos bontés, jetez un regard sur moi.
Unijibu, Yahwe, maana uaminifu wa agano lako ni mwema; kwa maana rehema zako kwangu ni nyingi, unigeukie.
17 Et ne détournez pas votre face de votre serviteur; parce que je suis tourmenté, exaucez-moi promptement,
Usiufiche uso wako mbali na mtumishi wako, maana niko katika dhiki; unijibu haraka.
18 Soyez attentif à mon âme et délivrez-la à cause de mes ennemis: sauvez-moi.
Uje kwangu na unikomboe. Kwa sababu ya adui zangu, uwe fidia yangu.
19 C’est vous qui connaissez mon opprobre, ma confusion et ma retenue.
Wewe wajua kulaumiwa kwangu, kuaibishwa kwangu, na kudharauliwa kwangu; wapinzani wangu wote wako mbele yako.
20 Ils sont en votre présence, tous ceux qui me tourmentent: mon cœur a attendu l’opprobre et la misère.
Lawama imevunja moyo wangu; nimejawa na huzuni kubwa; nilitafuta mtu wa kunihurumia, lakini hakuwepo; nilitafuta wafariji, lakini sikupata.
21 Ils m’ont donné pour nourriture du fiel, et dans ma soif ils m’ont abreuvé de vinaigre.
Walinipa sumu kwa ajili ya chakula changu; katika kiu yangu walinipa siki ninywe.
22 Que leur table devienne devant eux un filet, et la punition qu’ils méritent, une pierre d’achoppement.
Meza yao mbele yao na iwe mtego; wafikiripo wako kwenye usalama, iwe kitanzi.
23 Que leur yeux s’obscurcissent, afin qu’ils ne voient point: et tenez leur dos toujours courbé.
Macho yao na yatiwe giza ili kwamba wasiweze kuona; uvifanye viuno vyao kutetemeka daima.
24 Répandez sur eux votre colère, et que la fureur de votre colère les saisisse.
Wamwagie gadhabu yako, ukali wa hasira yako uwafikie wao.
25 Que leur habitation devienne déserte, et que dans leurs tabernacles il n’y ait personne qui habite.
Sehemu yao na iwe ukiwa; mtu yeyote asiishi katika hema yao.
26 Parce qu’ils ont persécuté celui que vous-même vous avez frappé, et qu’ils ont ajouté à la douleur de mes plaies.
Kwa kuwa walimtesa yule uliyempa adhabu. Mara kwa mara walihesabu maumivu ya wale walioumizwa.
27 Mettez iniquité sur leur iniquité, et qu’ils n’entrent point dans votre justice.
Wakiwashtaki kuwa wamefanya uovu juu ya uovu; usiwaache waje kwenye ushindi wa haki yako.
28 Qu’ils soient effacés du livre des vivants, et qu’avec les justes ils ne soient point écrits.
Uwafute kwenye Kitabu cha Uzima na wasiandikwe pamoja na wenyehaki.
29 Pour moi, je suis pauvre et souffrant; votre secours, ô mon Dieu, m’a soutenu.
Lakini mimi ni maskini na mwenye huzuni; uruhusu wokovu wako, Mungu, uniweke juu sana.
30 Je louerai le nom du Seigneur par un cantique, je le glorifierai par ma louange.
Nitalisifu jina la Mungu kwa wimbo na nitamtukuza yeye kwa shukrani.
31 Et cela sera plus agréable à Dieu qu’un jeune veau qui pousse ses cornes et ses ongles.
Nitamsifu Yahwe zaidi kuliko ng'ombe au ndama aliye na mapembe na kwato.
32 Que les pauvres voient et se réjouissent: cherchez Dieu et votre âme vivra;
Wanyenyekevu wameona na kufurahi; ninyi mnao matafuta Mungu, mioyo yenu itiwe nguvu.
33 Parce que le Seigneur a exaucé les pauvres, il n’a pas méprisé ceux qui sont dans les liens.
Maana Yahwe husikia wenye uhitaji naye hawadharau wafungwa wake.
34 Que les cieux le louent, ainsi que la terre, la mer et tous les reptiles qu’ils contiennent.
Mbingu na nchi zimsifu yeye, bahari na vyote vitembeavyo majini.
35 Parce que Dieu sauvera Sion, et que les cités de Juda seront rebâties.
Kwa maana Mungu ataiokoa Sayuni na ataujenga tena mji wa Yuda; watu wataishi huko na kupata umiliki wao.
36 Et la race des serviteurs de Dieu la possédera; et ceux qui aiment son nom y habiteront.
Ukoo wa watumishi wake watairithi; nao walipendao jina lake wataishi humo.