< Psaumes 63 >

1 Psaume de David lorsqu’il était dans le désert de l’Idumée. Dieu, mon Dieu, je veille et j’aspire vers vous dès la lumière.
Mungu, wewe ni Mungu wangu! Ninakutafuta wewe kwa bidii, moyo wangu unakiu yako, mwili wangu unakutamani sana wewe, katika ukame na nchi iliyochoka mahali ambapo hakuna maji.
2 Dans une terre déserte et sans chemin, et sans eau, je me suis présenté devant vous, comme dans le sanctuaire, afin de voir votre vertu et votre gloire.
Hivyo nimekutafuta wewe katika watu watakatifu kuona nguvu zako na utukufu wako.
3 Parce que votre miséricorde est meilleure que la vie; mes lèvres vous loueront.
Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakusifu wewe.
4 Ainsi je vous bénirai pendant ma vie: et en votre nom je lèverai mes mains.
Hivyo nitakutukuza wewe niwapo hai; kwa jina lako nitainua mikono yangu juu.
5 Que mon âme soit remplie comme d’une graisse abondante; et avec des lèvres d’exultation, ma bouche vous louera.
Itakuwa kana kwamba nilikula mlo wa mafuta na wenye kunona, kwa midomo ya furaha kinywa changu kitakusifu wewe,
6 Si je me suis souvenu de vous sur ma couche; je méditerai les matins sur vous,
nikufikiripo kitandani mwangu na kukutafakari wewe wakati wa saa za usiku.
7 Parce que vous avez été mon aide. Et à couvert sous vos ailes, je serai transporté de joie.
Kwa maana umekuwa msaada wangu, na katika uvuli wa mbawa zako ninafurahia.
8 Mon âme s’est attachée à vous; votre droite m’a soutenu.
Ninashikamana nawe; mkono wako wa kuume unanisaidia.
9 Pour eux, en vain ils ont cherché mon âme; ils entreront dans les parties inférieures de la terre.
Lakini wale watafutao kuuharibu uhai wangu wataenda chini kwenye sehemu ya chini kabisa ya nchi;
10 Ils seront livrés aux mains du glaive, ils seront la part des renards.
watakabidhiwa kwa wale ambao mikono yao hutumia upanga, nao watakuwa chakula cha mbweha.
11 Mais le roi se réjouira en Dieu; on louera tous ceux qui jureront par lui; parce qu’a été fermée la bouche de ceux qui disaient des choses iniques.
Bali mfalme atashangilia katika Mungu; yeyote anaye apa kupitia yeye atajivunia yeye, lakini vinywa ya wale wasemao uongo watanyamazishwa.

< Psaumes 63 >