< Psaumes 56 >

1 Pour le peuple qui a été éloigné des saints (ou des choses saintes); par David, pour une inscription de titre, lorsque les Allophylles (étrangers) le retinrent dans Geth. Ayez pitié de moi, ô Dieu, parce qu’un homme m’a foulé aux pieds: tout le jour m’attaquant, il m’a tourmenté.
Uwe na huruma nami, Mungu, kwa maana watu wananishambulia! Muda wote wale wanao pigana nami hunikaribia zaidi ili wanishambulie.
2 Mes ennemis m’ont foulé aux pieds tout le jour; parce qu’ils sont nombreux, ceux qui combattent contre moi.
Adui zangu hunikanyaga muda wote; maana ni wengi ambao kwa kiburi hupigana dhidi yangu.
3 Dès la hauteur du jour, je viendrai; mais j’espérerai en vous.
Wakati nina woga, nitaweka imani yangu katika wewe.
4 En Dieu je louerai mes discours, en Dieu j’ai espéré; je ne craindrai pas ce que pourra me faire la chair.
Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu - nimeweka imani yangu katika Mungu; sitaogopa; mtu wa kawaida atanifanya nini?
5 Tout le jour ils exécraient mes paroles: c’est contre moi que toutes leurs pensées s’exerçaient au mal.
Muda wote wanayageuza maneno yangu; mawazo yao yote yako kinyume na mimi kwa ajili ya uovu.
6 Ils habiteront près de moi et ils se cacheront; en même temps, ils observeront mes pas. Comme ils ont attendu avec constance mon âme pour la perdre,
Wanajikusanya kwa pamoja, wanajificha wenyewe, na kuzifuatilia hatua zangu, wakisubiri kuniua.
7 Vous ne les sauverez à aucun prix: dans votre colère, vous briserez des peuples. Ô Dieu!
Usiwaache waikimbie adhabu yako kwa ajili ya uovu wao. Uwaangushe watu chini katika hasira yako, Mungu.
8 Je vous ai exposé ma vie; vous avez mis mes larmes en votre présence, Comme aussi dans votre promesse.
Wewe unahesabu kutangatanga kwangu na kuweka machozi yangu kwenye chupa yako; je, hayako kitabuni mwako?
9 Alors mes ennemis seront rejetés en arrière. En quelque jour que je vous aie invoqué, j’ai connu que vous êtes mon Dieu.
Ndipo maadui zangu watakimbia katika siku ile nikuitapo wewe; hili najua, kwamba Mungu yupo kwa ajili yangu.
10 En Dieu, je louerai une parole; dans le Seigneur, je louerai un discours:
Katika Mungu ambaye neno lake ninalisifu, katika Yahwe ambaye neno lake ninalisifu,
11 en Dieu j’ai espéré, je ne craindrai pas ce que pourra me faire un homme.
katika Mungu ninaamini, sitaogopa. Yeyote atanifanya nini?
12 Je vous dois, ô Dieu, des vœux que j’acquitterai, et des louanges en votre honneur.
Wajibu wa kutimiza viapo vyangu kwako uko juu yangu, Mungu; nitatoa sadaka ya shukurani.
13 Parce que vous avez arraché mon âme à la mort, et mes pieds à la chute, afin que je me rende agréable devant Dieu, dans la lumière des vivants.
Kwa kuwa umeokoa uhai wangu na mauti; umezuia miguu yangu isianguke, ili kwamba niweze kutembea mbele ya Mungu katika nuru ya uhai.

< Psaumes 56 >