< Psaumes 50 >
Zaburi ya Asafu. Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana, asema na kuiita dunia, tangu mawio ya jua hadi mahali pake liendapo kutua.
2 C’est de Sion que vient l’éclat de sa splendeur.
Kutoka Sayuni, penye uzuri mkamilifu, Mungu anaangaza.
3 Dieu viendra manifestement: notre Dieu viendra, et il ne gardera pas le silence.
Mungu wetu anakuja na hatakaa kimya, moto uteketezao unamtangulia, akiwa amezungukwa na tufani kali.
4 D’en haut il appellera le ciel et la terre pour juger son peuple.
Anaziita mbingu zilizo juu, na nchi, ili aweze kuwahukumu watu wake:
5 Rassemblez-lui ses saints, qui exécutent son alliance sur les sacrifices.
“Nikusanyieni watu wangu waliowekwa wakfu, waliofanya agano nami kwa dhabihu.”
6 Et les cieux annonceront sa justice, parce que c’est Dieu lui-même qui est juge.
Nazo mbingu zinatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ni hakimu.
7 Écoute, mon peuple, et je parlerai; Israël, écoute; car je te prendrai à témoin: Dieu, ton Dieu, c’est moi qui le suis.
“Sikieni, enyi watu wangu, nami nitasema, ee Israeli, nami nitashuhudia dhidi yenu: Mimi ndimi Mungu, Mungu wenu.
8 Je ne te reprendrai pas pour tes sacrifices; car tes holocaustes sont toujours en ma présence.
Sikukemei kwa sababu ya dhabihu zako, au sadaka zako za kuteketezwa, ambazo daima ziko mbele zangu.
9 Je ne prendrai pas des veaux de ta maison, ni des boucs de tes troupeaux.
Sina haja ya fahali wa banda lako, au mbuzi wa zizi lako.
10 Parce qu’à moi sont toutes les bêtes des forêts, les animaux qui paissent sur les montagnes et les bœufs.
Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, na pia makundi ya mifugo juu ya vilima elfu.
11 Je connais tous les volatiles du ciel, et la beauté des champs est en mon pouvoir.
Ninamjua kila ndege mlimani, nao viumbe wa kondeni ni wangu.
12 Si j’ai faim, je ne te le dirai pas: car à moi est le globe de la terre, et sa plénitude.
Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi, kwa maana ulimwengu ni wangu, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake.
13 Est-ce que je mangerai des chairs de taureaux? ou boirai-je du sang des boucs?
Je, mimi hula nyama ya mafahali au kunywa damu ya mbuzi?
14 Immole à Dieu un sacrifice de louange, et rends au Très-Haut tes vœux.
Toa sadaka za shukrani kwa Mungu, timiza nadhiri zako kwake Yeye Aliye Juu Sana,
15 Et invoque-moi, au jour de la tribulation: je te délivrerai, et tu m’honoreras.
na uniite siku ya taabu; nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”
16 Mais au pécheur Dieu a dit: Pourquoi racontes-tu mes justices, et pourquoi ta bouche annonce-t-elle mon alliance?
Lakini kwake mtu mwovu, Mungu asema: “Una haki gani kunena sheria zangu au kuchukua agano langu midomoni mwako?
17 Pour toi, tu hais la discipline, et tu as rejeté ma parole derrière toi.
Unachukia mafundisho yangu na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.
18 Si tu voyais un voleur, tu courais avec lui, et c’est avec les adultères que tu mettais ta part.
Unapomwona mwizi, unaungana naye, unapiga kura yako pamoja na wazinzi.
19 Ta bouche a abondé en malice, et ta langue ajustait des fourberies.
Unakitumia kinywa chako kwa mabaya na kuuongoza ulimi wako kwa hila.
20 Assis, tu parlais contre ton frère et contre le fils de ta mère, tu posais une pierre d’achoppement.
Wanena daima dhidi ya ndugu yako na kumsingizia mwana wa mama yako.
21 Tu as fait ces choses, et je me suis tu.
Mambo haya unayafanya, nami nimekaa kimya, ukafikiri Mimi nami ni kama wewe. Lakini nitakukemea na kuweka mashtaka mbele yako.
22 Comprenez ces choses, vous qui oubliez Dieu; de peur qu’un jour il ne vous enlève, et qu’il n’y ait personne qui vous délivre.
“Yatafakarini haya, ninyi mnaomsahau Mungu, ama sivyo nitawararua vipande vipande, wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwaokoa:
23 C’est un sacrifice de louange qui m’honorera; et c’est là le chemin par lequel je lui montrerai le salut de Dieu.
Atoaye dhabihu za shukrani ananiheshimu mimi, naye aiandaa njia yake ili nimwonyeshe wokovu wa Mungu.”