< Psaumes 106 >

1 Louez le Seigneur, parce qu’il est bon, parce que pour jamais est sa miséricorde.
Msifuni Bwana. Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
2 Qui dira les puissances du Seigneur, et fera entendre toutes ses louanges?
Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana au kutangaza kikamilifu sifa zake?
3 Bienheureux ceux qui gardent l’équité, et qui pratiquent la justice en tout temps.
Heri wale wanaodumisha haki, ambao daima wanafanya yaliyo mema.
4 Souvenez-vous de nous, Seigneur, dans votre bienveillance pour votre peuple; visitez-nous pour nous sauver;
Ee Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako, uwe msaada wangu unapowaokoa,
5 Pour que nous voyions avec joie les biens de vos élus, que nous nous réjouissions dans la joie de votre nation, afin que vous soyez loué avec votre héritage.
ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako, niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako, na kuungana na urithi wako katika kukusifu.
6 Nous avons péché avec nos pères; nous avons injustement agi, nous avons commis l’iniquité.
Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda, tumekosa na tumetenda uovu.
7 Nos pères en Égypte ne comprirent point vos merveilles, ils ne se souvinrent pas de la grandeur de votre miséricorde. Et ils vous irritèrent, lorsqu’ils montaient vers la mer, la mer Rouge.
Wakati baba zetu walipokuwa Misri, hawakuzingatia maajabu yako, wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako, bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu.
8 Mais il les sauva à cause de son nom, afin de faire connaître sa puissance.
Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake, ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.
9 Il réprimanda la mer Rouge, et elle fut desséchée, et il les conduisit dans des abîmes, comme dans un désert.
Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka, akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani.
10 Il les sauva de la main de ceux qui les haïssaient, et il les racheta de la main d’un ennemi.
Aliwaokoa mikononi mwa adui; kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.
11 Et l’eau couvrit ceux qui les tourmentaient, et il ne resta pas un seul d’entre eux.
Maji yaliwafunika adui zao, hakunusurika hata mmoja.
12 Alors ils crurent à ses paroles, et chantèrent ses louanges.
Ndipo walipoamini ahadi zake, nao wakaimba sifa zake.
13 Bientôt ils oublièrent ses œuvres, et n’attendirent pas l’accomplissement de ses desseins.
Lakini mara walisahau aliyowatendea, wala hawakungojea shauri lake.
14 Mais ils conçurent un désir violent dans le désert, et ils tentèrent Dieu dans un lieu sans eau.
Jangwani walitawaliwa na tamaa zao, walimjaribu Mungu nyikani.
15 Il leur accorda leur demande, il leur envoya le rassasiement de leurs âmes.
Kwa hiyo aliwapa kile walichoomba, lakini akatuma juu yao ugonjwa wa kudhoofisha.
16 Et ils irritèrent, dans le camp, Moïse et Aaron, le saint du Seigneur.
Kambini walimwonea wivu Mose, na pia Aroni aliyekuwa amewekwa wakfu kwa Bwana.
17 La terre s’ouvrit et engloutit Dathan; et elle couvrit la troupe d’Abiron.
Ardhi ilifunguka ikawameza Dathani, ikawazika Abiramu na kundi lake.
18 Un feu s’alluma au milieu de leur assemblée: une flamme brûla entièrement ces pécheurs.
Moto uliwaka katikati ya wafuasi wao, mwali wa moto uliwateketeza waovu.
19 Et ils firent un veau à Horeb, et adorèrent une image taillée au ciseau.
Huko Horebu walitengeneza ndama, na kuabudu sanamu ya kusubu kwa chuma.
20 Ils changèrent ainsi leur gloire contre la ressemblance d’un veau qui mange de l’herbe.
Waliubadilisha Utukufu wao kwa sanamu ya fahali, ambaye hula majani.
21 Ils oublièrent le Dieu qui les avait sauvés, qui avait fait de grandes choses en Égypte,
Walimsahau Mungu aliyewaokoa, aliyekuwa ametenda mambo makuu huko Misri,
22 Des choses merveilleuses dans la terre de Cham; des choses terribles dans la mer Rouge.
miujiza katika nchi ya Hamu na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu.
23 Et il avait dit qu’il les perdrait entièrement, si Moïse son élu ne se fût tenu sur la brèche en sa présence. Afin de détourner sa colère, pour qu’il ne les perdît pas entièrement;
Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza: kama Mose mteule wake, asingesimama kati yao na Mungu kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza.
24 Et ils comptèrent pour rien une terre si désirable; Ils ne crurent point à sa parole,
Kisha waliidharau ile nchi nzuri, hawakuiamini ahadi yake.
25 Mais ils murmurèrent dans leurs tabernacles; ils n’écoutèrent point la voix du Seigneur.
Walinungʼunika ndani ya mahema yao, wala hawakumtii Bwana.
26 Alors il leva sa main sur eux, afin de les terrasser dans le désert,
Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba atawafanya waanguke jangwani,
27 Et afin d’abaisser leur race au milieu des nations, pour les disperser dans diverses contrées.
kuwatawanya wazao wao waanguke miongoni mwa mataifa, na kuwatawanya katika nchi zote.
28 Ils se consacrèrent à Béelphégor, et ils mangèrent des sacrifices des morts.
Walijifunga nira na Baali wa Peori, wakala dhabihu zilizotolewa kwa miungu isiyo na uhai.
29 Ils irritèrent le Seigneur par leurs inventions, et la ruine se multiplia parmi eux.
Waliichochea hasira ya Bwana, wakamkasirisha kwa matendo yao maovu, nayo tauni ikazuka katikati yao.
30 Mais Phinéès se présenta et apaisa le Seigneur, et le désastre cessa.
Lakini Finehasi alisimama na kuingilia kati, nayo tauni ikazuiliwa.
31 Et ce lui fut imputé à justice, dans toutes les générations à jamais.
Hili likahesabiwa kwake haki, kwa vizazi visivyo na mwisho vijavyo.
32 Ils irritèrent encore le Seigneur aux eaux de contradiction, et Moïse fut puni à cause d’eux,
Kwenye maji ya Meriba, walimkasirisha Bwana, janga likampata Mose kwa sababu yao;
33 Parce qu’ils contristèrent son esprit. Et que la défiance fut sur ses lèvres;
kwa maana walimwasi Roho wa Mungu, na maneno yasiyofaa yakatoka midomoni kwa Mose.
34 Ils ne détruisirent point les nations que Dieu leur avait désignées.
Hawakuyaangamiza yale mataifa kama Bwana alivyowaagiza,
35 Mais ils se mêlèrent parmi les nations, ils apprirent leurs œuvres;
bali walijichanganya na mataifa na wakazikubali desturi zao.
36 Et ils servirent leurs images taillées au ciseau, et ce devint pour eux une occasion de scandale.
Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.
37 Ils immolèrent leurs fils et leurs filles au démon.
Wakawatoa wana wao na binti zao dhabihu kwa mashetani.
38 Ils répandirent un sang innocent, le sang de leurs fils et de leurs filles qu’ils sacrifièrent aux images taillées au ciseau de Chanaan.
Walimwaga damu isiyo na hatia, damu za wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.
39 Et elle fut souillée par leurs œuvres: et ils forniquèrent avec leurs inventions.
Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.
40 Aussi le Seigneur fut irrité de fureur contre son peuple, et il eut en abomination son héritage.
Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake na akauchukia sana urithi wake.
41 Et il les livra entre les mains des nations, et ceux qui les haïssaient les dominèrent.
Akawakabidhi kwa mataifa na adui zao wakawatawala.
42 Et leurs ennemis les tourmentèrent, et ils furent humiliés sous leurs mains;
Adui zao wakawaonea na kuwatia chini ya mamlaka yao.
43 Souvent il les délivra. Mais eux l’aigrirent par leurs sentiments, et ils furent humiliés à cause de leurs iniquités.
Mara nyingi aliwaokoa lakini walikuwa wamezama kwenye uasi, nao wakajiharibu katika dhambi zao.
44 Et il vit qu’ils étaient tourmentés, et il écouta leur prière.
Lakini akaangalia mateso yao wakati aliposikia kilio chao;
45 Il se souvint de son alliance, et il se repentit selon la grandeur de sa miséricorde.
kwa ajili yao akakumbuka agano lake, na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.
46 Il les livra donc à ses miséricordes, en présence de tous ceux qui les avaient menés en captivité.
Akawafanya wahurumiwe na wote waliowashikilia mateka.
47 Sauvez-nous, Seigneur notre Dieu, et rassemblez-nous, et délivrez-nous des nations,
Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe. Tukusanye tena kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.
48 Béni le Seigneur Dieu d’Israël d’un siècle jusqu’à un autre siècle! et tout le peuple dira: Ainsi soit, ainsi soit.
Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Watu wote na waseme, “Amen!” Msifuni Bwana.

< Psaumes 106 >