< Philippiens 2 >

1 Si donc il est quelque consolation dans le Christ, quelque douceur dans la charité, quelque communion d’esprit; s’il est des entrailles de commisération,
Ikiwa kuna kutiwa moyo katika Kristo. Ikiwa kuna faraja kutoka katika pendo lake. Ikiwa kuna ushirika wa Roho. Ikiwa kuna rehema na huruma.
2 Comblez ma joie, étant dans les mêmes sentiments, ayant la même charité, la même âme, la même pensée;
Ikamilisheni furaha yangu kwa kunia mamoja mkiwa na upendo mmoja, mkiwa wamoja katika roho, na kuwa na kusudi moja.
3 Rien par esprit de contention, ni par vaine gloire, mais par humilité, croyant les autres au-dessus de soi,
Msifanye kwa ubinafsi na majivuno. Isipokuwa kwa unyenyekevu mkiwaona wengine kuwa bora zaidi yenu.
4 Chacun ayant égard, non à ses propres intérêts, mais à ceux d’autrui.
Kila mmoja wenu asiangalie tu mahitaji yake binafsi, bali pia ajali mahitaji ya wengine.
5 Ayez en vous les sentiments qu’avait en lui le Christ Jésus,
Muwe na nia kama aliyonayo Kristo Yesu.
6 Qui, étant dans la forme de Dieu, n’a pas cru que ce fût une usurpation de se faire égal à Dieu;
Ingawaje yeye ni sawa na Mungu. Lakini hakujali kuwa sawa na Mungu ni kitu cha kushikamana nacho.
7 Mais il s’est anéanti lui-même, prenant la forme d’esclave, ayant été fait semblable aux hommes, et reconnu pour homme par les dehors.
Badala yake, alijishusha mwenyewe. Alichukua umbo la mtumishi. Akajitokeza katika mfano wa wanadamu. Alionekana mwanadamu.
8 Il s’est humilié lui-même, s’étant fait obéissant jusqu’à la mort de la croix.
Yeye alijinyeyekeza na kuwa mtii hadi kifo, kifo cha msalaba.
9 C’est pourquoi Dieu l’a exalté et lui a donné un nom qui est au-dessus de tout nom;
Hivyo basi Mungu alimtukuza sana. Alimpa jina kuu lipitalo kila jina.
10 Afin qu’au nom de Jésus, tout genou fléchisse dans le ciel, sur la terre et dans les enfers,
Alifanya hivyo ili kwamba katika jina la Yesu kila goti sharti liiname. Magoti ya walio mbinguni na walio juu ya ardhi na chini ya ardhi.
11 Et que toute langue confesse que le Seigneur Jésus-Christ est dans la gloire de Dieu le Père.
Na alifanya hivyo ili kwamba kila ulimi sharti ukiri kwamba Yesu kristo ni Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba.
12 Ainsi, mes bien-aimés (comme vous avez été toujours obéissants), non-seulement en ma présence, mais bien plus encore en mon absence, comme en ce moment, opérez votre salut avec crainte et tremblement.
Kwa hiyo basi, wapendwa wangu kama mnavyotii siku zote, Si tu katika uwepo wangu lakini sasa ni zaidi sana hata pasipo uwepo wangu, uwajibikeni wokovu wenu wenyewe kwa hofu na kutetemeka.
13 Car c’est Dieu qui opère en vous et le vouloir et le faire, selon sa bonne volonté.
Kwa kuwa ni Mungu anayetenda kazi ndani yenu ili kuwawezesha kunia na kutenda mambo yale yampendezayo yeye.
14 Faites tout sans murmure et sans hésitations;
Fanyeni mambo yote bila malalamiko na mabishano.
15 Afin que vous soyez sans reproche et sincères, comme des enfants de Dieu, sans répréhension au milieu d’une nation dépravée et perverse, parmi laquelle vous brillez comme des astres dans le monde,
Fanyeni hivyo ili kwamba msilaumike na kuwa watoto wa Mungu waaminifu wasiyo na lawama. Fanyeni hivyo ili kwamba muwe nuru ya dunia, katika kizazi cha uasi na uovu.
16 Gardant la parole de vie pour ma gloire au jour du Christ, parce que ce n’est pas en vain que j’ai couru, ni en vain que j’ai travaillé.
Shikani sana neno la uzima ili kwamba niwe na sababu ya kutukuza siku ya Kristo. Kisha nitafahamu kwamba sikupiga mbio bure wala sikutaabika bure.
17 Et si je suis immolé sur le sacrifice et l’oblation de votre foi, je m’en réjouis et m’en félicite avec vous tous;
Lakini hata kama ninamiminwa kama sadaka juu ya dhabidhu na huduma ya imani yenu, ninafurahi, na ninafurahi pamoja nanyi nyote.
18 Mais vous-mêmes, réjouissezvous-en et vous en félicitez avec moi.
Vilevile na ninyi pia mnafurahi, na mnafurahi pamoja nami.
19 J’espère dans le Seigneur Jésus vous envoyer bientôt Timothée, afin que moi aussi, je sois consolé, ce qui vous regarde m’étant connu.
Lakini natumaini katika Bwana Yesu kumtuma Timotheo kwenu hivi karibuni, ili kwamba niweze kutiwa moyo nitakapojua mambo yenu.
20 Car je n’ai personne qui me soit aussi intimement uni et qui s’inquiète autant de vous par une affection sincère.
Kwa kuwa sina mwingine aliye na mtazamo kama wake, mwenye nia ya kweli kwa ajili yenu.
21 En effet, tous cherchent leurs intérêts et non les intérêts de Jésus-Christ.
Wengine wote ambao ningewatuma kwenu wanatafuta mambo yao binafsi tu, na siyo mambo ya Yesu Kristo.
22 Or jugez-le par l’épreuve qui en a été faite, puisque, comme un fils aide son père, il m’a aidé dans la prédication de l’Evangile.
Lakini mnaijua thamani yake, kwa sababu kama mtoto anavyomhudumia baba yake, ndivyo alivyotumika pamoja nami katika injili.
23 J’ai donc dessein de vous l’envoyer dès que j’aurai pourvu à ce qui me regarde.
Kwa hiyo ninatumaini kumtuma haraka pindi tu nitakapofahamu nini kitatokea kwangu.
24 Et j’ai cette confiance dans le Seigneur, que moi-même je viendrai bientôt vers vous.
Lakini nina hakika katika Bwana kwamba mimi mwenyewe pia nitakuja hivi karibuni.
25 Cependant j’ai jugé nécessaire de vous envoyer Epaphrodite, mon frère, compagnon de mes travaux et de mes combats, votre apôtre et mon aide dans mes nécessités;
Lakini nafikiri ni muhimu kumrejesha kwenu Epafradito. Yeye ni ndugu yangu na mtenda kazi mwenzangu na askari mwenzangu, mjumbe na mtumishi wenu kwa ajili ya mahitaji yangu.
26 Parce qu’il désirait vous voir tous, et qu’il était affligé que vous l’aviez su malade.
Kwa sababu alikuwa na hofu na alitamani kuwa pamoja nanyi nyote, kwa kuwa mlisikia kwamba alikuwa mgonjwa.
27 Car il a été malade jusqu’à la mort, mais Dieu a eu pitié de lui, et non-seulement de lui, mais de moi aussi, afin que je n’eusse point tristesse sur tristesse.
Maana hakika alikuwa mgonjwa sana kiasi cha kufa. Lakini Mungu alimhurumia, na wema huo haukuwa juu yake tu, lakini pia ulikuwa juu yangu, ili kwamba nisiwe na huzuni juu ya huzuni.
28 Je vous l’ai donc envoyé en grande hâte, pour que le revoyant, vous vous réjouissiez, et que je ne sois plus moi-même dans l’affliction.
Kwa hiyo ninamrejesha kweny haraka iwezekanavyo, Ili kwamba mtakapomwona tena mpate kufurahi na mimi nitakuwa nimeondolewa wasi wasi.
29 C’est pourquoi recevez-le en toute joie dans le Seigneur, et honorez ceux qui sont tels.
Mkaribisheni Epafradito katika Bwana kwa furaha zote. Waheshimuni watu kama yeye.
30 Car c’est à cause de l’œuvre du Christ qu’il a été tout près de la mort, livrant son âme pour accomplir envers moi le service que vous ne me pouviez rendre vous-mêmes.
Kwa kuwa ilikuwa kwa ajili ya kazi ya Kristo kwamba alikaribia kufa. Alihatarisha maisha yake ili kuniokoa mimi na akafanya kile ambacho hamkuweza kufanya katika kunihudumia mimi kwa mko mbali nami.

< Philippiens 2 >