< Nombres 3 >

1 Voici les générations d’Aaron et de Moïse, au jour que le Seigneur parla à Moïse sur la montagne de Sinaï.
Hii ni hesabu ya jamaa ya Aroni na Mose kwa wakati ambao Bwana alizungumza na Mose katika Mlima Sinai.
2 Et voici les noms des fils d’Aaron: Son premier-né Nadab, ensuite Abiu, Eléazar et Ithamar.
Majina ya wana wa Aroni yalikuwa: Nadabu mzaliwa wa kwanza na Abihu, Eleazari na Ithamari.
3 Tels sont les noms des fils d’Aaron, prêtres qui furent oints, et dont les mains furent remplies et consacrées pour qu’ils exerçassent les fonctions du sacerdoce.
Hayo yalikuwa majina ya wana wa Aroni, makuhani wapakwa mafuta, waliokuwa wamesimikwa kuhudumu kama makuhani.
4 Or Nadab et Abiu moururent sans enfants lorsqu’ils offraient un feu étranger en la présence du Seigneur dans le désert de Sinaï; et Eléazar et Ithamar exercèrent les fonctions du sacerdoce devant Aaron leur père.
Hata hivyo Nadabu na Abihu walikufa mbele za Bwana walipotoa sadaka kwa moto usioruhusiwa mbele zake katika Jangwa la Sinai. Hawakuwa na wana; kwa hiyo Eleazari na Ithamari walihudumu peke yao kama makuhani wakati wote wa maisha ya Aroni baba yao.
5 Et le Seigneur parla à Moïse, disant:
Bwana akamwambia Mose,
6 Fais approcher la tribu de Lévi, et fais-les tenir en la présence d’Aaron, le prêtre, afin qu’ils le servent, et qu’ils veillent;
“Walete watu wa kabila la Lawi mbele ya Aroni kuhani ili wamsaidie.
7 Qu’ils observent aussi tout ce qui appartient au culte de la multitude devant le tabernacle de témoignage;
Watafanya huduma kwa ajili yake na kwa jumuiya yote katika Hema la Kukutania kwa kufanya kazi za Maskani.
8 Qu’ils gardent les vases du tabernacle, servant pour son ministère.
Watatunza samani zote za Hema la Kukutania, wakitimiza wajibu wa kuhudumia Waisraeli kwa kufanya kazi ya Maskani.
9 Et tu donneras en dons les Lévites
Wakabidhi Walawi kwa Aroni na wanawe; hao ndio Waisraeli ambao wanakabidhiwa kwake kabisa.
10 À Aaron et à ses fils auxquels ils ont été accordés par les enfants d’Israël. Mais tu établiras Aaron et ses fils dans les fonctions du sacerdoce. L’étranger qui approchera pour exercer le ministère, mourra.
Waweke Aroni na wanawe kuhudumu kama makuhani; mtu mwingine yeyote atakayesogea mahali patakatifu ni lazima auawe.”
11 Le Seigneur parla encore à Moïse, disant:
Bwana akamwambia Mose,
12 J’ai pris les Lévites d’entre les enfants d’Israël, à la place de tout premier-né qui ouvre un sein parmi les enfants d’Israël, et les Lévites seront à moi.
“Nimewatwaa Walawi kutoka miongoni mwa Waisraeli badala ya mzaliwa wa kwanza wa kiume wa kila mwanamke wa Mwisraeli. Walawi ni wangu,
13 Car tout premier-né est à moi, depuis que j’ai frappé les premiers-nés dans la terre d’Egypte, j’ai consacré pour moi tout ce qui naît le premier en Israël, depuis l’homme jusqu’à la bête: Je suis le Seigneur.
kwa kuwa wazaliwa wote wa kwanza ni wangu. Nilipowaua wazaliwa wa kwanza huko Misri, nilimtenga kila mzaliwa wa kwanza katika Israeli awe wangu, akiwa mwanadamu au mnyama. Watakuwa wangu. Mimi ndimi Bwana.”
14 Le Seigneur parla de nouveau à Moïse dans le désert de Sinaï, disant:
Bwana akamwambia Mose katika Jangwa la Sinai,
15 Dénombre les enfants de Lévi, selon les maisons de leurs pères et leurs familles, tout mâle d’un mois et au-dessus.
“Wahesabu Walawi kwa jamaa zao na koo zao. Mhesabu kila mwanaume mwenye umri wa mwezi mmoja au zaidi.”
16 Moïse les dénombra, comme avait ordonné le Seigneur,
Kwa hiyo Mose akawahesabu, kama alivyoamriwa na neno la Bwana.
17 Et furent trouvés les enfants de Lévi, selon leurs noms, Gerson, Caath et Mérari.
Haya yalikuwa majina ya wana wa Lawi: Gershoni, Kohathi na Merari.
18 Les fils de Gerson: Lebni et Séméi.
Haya ndiyo yaliyokuwa majina ya koo za Wagershoni: Libni na Shimei.
19 Les fils de Caath: Amram, Jésaar, Hébron et Oziel.
Koo za Wakohathi zilikuwa ni: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
20 Les fils de Mérari: Moholi et Musi.
Koo za Wamerari zilikuwa ni: Mahli na Mushi. Hizi ndizo zilizokuwa koo za Walawi, kufuatana na jamaa zao.
21 De Gerson sont sorties deux familles, la Lebnitique et la Séméitique,
Kulikuwa na koo za Walibni na Washimei kwa Gershoni; hizi ndizo zilizokuwa koo za Wagershoni.
22 Dont la population du sexe masculin depuis un mois et au-dessus dénombrée, fut de sept mille cinq cents.
Idadi ya waume wote waliokuwa na mwezi mmoja au zaidi waliohesabiwa walikuwa 7,500.
23 Ceux-ci camperont derrière le tabernacle, vers l’occident,
Ukoo wa Wagershoni walitakiwa kuweka kambi zao upande wa magharibi, nyuma ya Maskani.
24 Sous le prince Eliasaph, fils de Laël.
Kiongozi wa jamaa za Wagershoni alikuwa Eliasafu mwana wa Laeli.
25 Et ils auront la garde dans le tabernacle d’alliance,
Katika Hema la Kukutania, Wagershoni walikuwa na wajibu wa kutunza Maskani na hema, vifuniko vyake, pazia katika mlango wa kuingilia ndani ya Hema la Kukutania,
26 Du tabernacle lui-même et de sa couverture, du voile qu’on tire devant la porte du toit d’alliance, et des rideaux du parvis, ainsi que du voile qui est suspendu à l’entrée du parvis du tabernacle, et de tout ce qui appartient au ministère de l’autel, les cordages du tabernacle et tous ses ustensiles.
mapazia ya ua, pazia katika ingilio la ua unaozunguka Maskani na madhabahu, pamoja na kamba, na kila kinachohusika kwa matumizi yake.
27 La parenté de Caath aura les peuples Amramites, Jésaarites, Hébronites et Oziélites. Ce sont là les familles des Caathites recensées selon leurs noms.
Kwa Kohathi kulikuwepo koo za Waamramu, Waishari, Wahebroni na Wauzieli; hizi ndizo zilizokuwa koo za Wakohathi.
28 Tous ceux du genre masculin depuis un mois et au-dessus, huit mille six cents auront la garde du sanctuaire,
Hesabu ya waume wote wenye mwezi mmoja au zaidi ilikuwa watu 8,600. Wakohathi waliwajibika kutunza mahali patakatifu.
29 Et ils camperont vers le côté méridional;
Koo za Wakohathi zilitakiwa kuweka kambi zao upande wa kusini wa Maskani.
30 Et leur prince sera Elisaphan, fils d’Oziel.
Kiongozi wa jamaa za koo za Wakohathi alikuwa Elisafani mwana wa Uzieli.
31 Ainsi ils garderont l’arche, la table, le chandelier, les autels, les vases du sanctuaire avec lesquels se fait le service, le voile et tous les objets semblables:
Waliwajibika kutunza Sanduku la Agano, meza, kinara cha taa, madhabahu, na vile vyombo vya mahali patakatifu vinavyotumika kuhudumu, pazia, na kila kitu kinachohusika na matumizi yake.
32 Mais le prince des princes des Lévites, Eléazar fils d’Aaron le prêtre, sera au-dessus de ceux qui veilleront à la garde du sanctuaire.
Kiongozi mkuu wa Walawi alikuwa Eleazari mwana wa kuhani, Aroni. Aliwekwa juu ya wale waliowajibika kutunza mahali patakatifu.
33 Mais de Mérari sortiront les familles Moholites et Musites, recensées selon leurs noms.
Kwa Merari kulikuwa na koo za Wamahli na Wamushi; hizi zilikuwa koo za Merari.
34 Tous les mâles depuis un mois et au-dessus sont au nombre de six mille deux cents.
Hesabu ya waume wote wenye umri wa mwaka mmoja au zaidi waliohesabiwa walikuwa 6,200.
35 Leur prince est Suriel, fils d’Abihaïel: c’est au côté septentrional qu’ils camperont.
Kiongozi wa jamaa za koo za Wamerari alikuwa Surieli mwana wa Abihaili; hawa walitakiwa kuweka kambi zao upande wa kaskazini mwa Maskani.
36 Seront sous leur garde: les ais du tabernacle, les leviers, les colonnes et leurs soubassements, et tout ce qui appartient à un tel service;
Wamerari waliwekwa kutunza miimo ya Maskani, mataruma yake, nguzo, vitako na vifaa vyake vyote na kila kitu kilichohusika na matumizi yake,
37 Et les colonnes autour du parvis avec leurs soubassements, et les pieux avec leurs cordages.
na pia nguzo za ua unaozunguka pamoja na vitako vyake, vigingi vya hema na kamba zake.
38 Devant le tabernacle d’alliance, c’est-à-dire vers le côté oriental, camperont Moïse et Aaron avec ses fils, ayant la garde du sanctuaire, au milieu des enfants d’Israël; tout étranger qui s’en approchera, mourra.
Mose, na Aroni na wanawe walitakiwa kuweka kambi zao mashariki mwa Maskani, kuelekea mawio ya jua, mbele ya Hema la Kukutania. Wao walihusika na utunzaji wa mahali patakatifu kwa niaba ya Waisraeli. Mtu mwingine yeyote aliyepasogelea mahali patakatifu angeuawa.
39 Tous les Lévites que dénombrèrent Moïse et Aaron d’après le commandement du Seigneur, selon leurs familles, parmi les mâles d’un mois et au-dessus, furent vingt-deux mille.
Jumla ya hesabu ya Walawi waliohesabiwa na Mose na Aroni kwa amri ya Bwana, kufuatana na koo, pamoja na kila mume mwenye umri wa mwezi mmoja au zaidi, walikuwa 22,000.
40 Le Seigneur dit encore à Moïse: Dénombre les premiers-nés mâles d’entre les enfants d’Israël, depuis un mois et au-dessus, et tu en tiendras compte.
Bwana akamwambia Mose, “Wahesabu wazaliwa wa kwanza wa kiume wote wa Waisraeli wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi na uorodheshe majina yao.
41 Et tu prendras pour moi les Lévites à la place de tout premier-né des enfants d’Israël; je suis le Seigneur; et leurs bestiaux à la place de tous les premiers-nés des bestiaux des enfants d’Israël.
Nitwalie Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli, nayo mifugo ya Walawi badala ya wazaliwa wa mifugo ya Waisraeli. Mimi ndimi Bwana.”
42 Moïse recensa, comme avait ordonné le Seigneur, les premiers-nés des enfants d’Israël;
Hivyo Mose akawahesabu wazaliwa wa kwanza wote wa Waisraeli, kama Bwana alivyomwamuru.
43 Et les mâles, selon leurs noms, depuis un mois et au-dessus, furent vingt-deux mille deux cent soixante-treize.
Jumla ya hesabu ya wazaliwa wa kwanza waume wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi, walioorodheshwa kwa majina, walikuwa 22,273.
44 Le Seigneur parla encore à Moïse, disant:
Bwana akamwambia Mose,
45 Prends les Lévites à la place des premiers-nés des enfants d’Israël, et les bestiaux des Lévites à la place de leurs bestiaux, et les Lévites seront à moi. Je suis le Seigneur.
“Watwae Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wote wa Israeli, nayo mifugo ya Walawi badala ya mifugo yao. Walawi watakuwa wangu. Mimi ndimi Bwana.
46 Et pour le prix des deux cent soixante-treize d’entre les premiers-nés des enfants d’Israël qui dépassent le nombre des Lévites,
Ili kukomboa wazao wa kwanza 273 wa Waisraeli ambao wamezidi hesabu ya Walawi,
47 Tu prendras cinq sicles pour chaque tête, selon la mesure du sanctuaire. Le sicle a vingt oboles.
kusanya shekeli tano kwa kila mmoja, kufuatana na shekeli ya mahali patakatifu, ambayo ina uzito wa gera ishirini.
48 Et tu donneras l’argent à Aaron pour le prix de ceux qui sont de plus.
Mpe Aroni na wanawe hizo fedha kwa ajili ya ukombozi wa idadi ya Waisraeli waliozidi.”
49 Moïse prit donc l’argent de ceux qui étaient de plus, et qu’ils avaient rachetés des Lévites,
Kwa hiyo Mose akakusanya fedha za ukombozi kutoka kwa wale ambao hesabu yao ilizidi wale waliokombolewa na Walawi.
50 Pour les premiers-nés des enfants d’Israël, mille trois cent soixante-cinq sicles selon le poids du sanctuaire;
Kutokana na wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli alikusanya fedha yenye uzito wa shekeli 1,365 kufuatana na shekeli ya mahali patakatifu.
51 Et il le donna à Aaron et à ses fils, selon la parole que lui avait ordonnée le Seigneur.
Mose akampa Aroni na wanawe ile fedha ya ukombozi, kama alivyoamriwa na neno la Bwana.

< Nombres 3 >