< Néhémie 2 >
1 Or il arriva au mois de Nisan, en la vingtième année du roi Artaxerxès, que le vin était devant lui; et je pris le vin, et je le donnai au roi, et jetais comme languissant devant sa face.
Katika mwezi wa Nisani mwaka wa ishirini wa utawala wa Mfalme Artashasta, wakati divai ilipoletwa kwake, niliichukua na kumpa mfalme. Sikuwahi kuonekana mwenye huzuni mbele yake kabla ya hapo.
2 Et le roi me dit: Pourquoi ton visage est-il triste, quoique je ne te voie point malade? Ce n’est pas en vain, mais je ne sais le mal qui est en ton cœur. Et je craignis beaucoup et extrêmement.
Basi mfalme akaniuliza, “Kwa nini uso wako unaonekana una huzuni wakati wewe si mgonjwa? Jambo hili si kitu kingine bali ni huzuni ya moyo.” Niliogopa sana,
3 Et je dis au roi: Roi, vivez éternellement. Pourquoi mon visage ne serait-il pas triste, puisque la ville, maison des tombeaux de mes pères, est déserte, et que ses portes ont été brûlées au feu.
lakini nikamwambia mfalme, “Mfalme na aishi milele! Kwa nini uso wangu usiwe na huzuni wakati mji walipozikwa baba zangu umebaki magofu, na malango yake yameteketezwa kwa moto?”
4 Et le roi me dit: Que demandes-tu? Alors je priai le Dieu du ciel,
Mfalme akaniambia, “Je, haja yako ni gani?” Ndipo nikaomba kwa Mungu wa mbinguni,
5 Et je répondis au roi: S’il semble bon au roi, et si votre serviteur est agréable devant votre face, que le roi m’envoie en Judée, dans la ville du sépulcre de mon père, et je la rebâtirai.
na nikamjibu mfalme, “Kama ikimpendeza mfalme, na kama mtumishi wako amepata kibali machoni pake, anitume kule mji wa Yuda, mahali baba zangu walipozikwa, ili niweze kuujenga upya.”
6 Alors le roi me demanda, et la reine qui était assise auprès de lui: Jusqu’à quel temps durera ton voyage, et quand reviendras-tu? Et il fut agréable devant la face du roi de m’envoyer; et je lui marquai le temps.
Kisha mfalme, na malkia akiwa ameketi karibu naye, akaniuliza, “Safari yako itachukua muda gani, nawe utarudi lini?” Ilimpendeza mfalme kunituma, kwa hiyo nikapanga muda.
7 Puis je dis au roi: S’il semble bon au roi, qu’il me donne des lettres pour les chefs de la contrée au-delà du fleuve, afin qu’ils me fassent conduire jusqu’à ce que je sois arrivé en Judée;
Pia nikamwambia, “Kama ikimpendeza mfalme, naomba nipewe barua kwa watawala wa Ngʼambo ya Frati, ili wanipe ulinzi mpaka nifike Yuda.
8 Et une lettre pour Asaph, gardien de la forêt du roi, afin qu’il me donne des bois, et que je puisse couvrir les portes de la tour de la maison, et les murs de la ville, et la maison dans laquelle j’entrerai. Et le roi me les donna, à cause que la main favorable de mon Dieu était avec moi.
Naomba nipewe barua nipeleke kwa Asafu, mtunzaji wa msitu wa mfalme, ili anipe miti ya kutengeneza boriti kwa ajili ya malango ya ngome ya Hekalu, na ukuta wa mji, na makao yangu nitakapoishi.” Kwa kuwa mkono wenye neema wa Mungu wangu ulikuwa juu yangu, mfalme akanijalia ombi langu.
9 Et je vins vers les chefs de la contrée au-delà du fleuve, et je leur donnai les lettres du roi. Or le roi avait envoyé avec moi des princes de la milice, et des cavaliers.
Basi nilienda kwa watawala wa Ngʼambo ya Frati na kuwapa barua za mfalme. Pia mfalme alikuwa ametuma maafisa wa jeshi na askari wapanda farasi pamoja nami.
10 Et Sanaballat, l’Horonite, et Tobie, le serviteur Ammanite, l’apprirent, et ils furent saisis d’une grande affliction, parce qu’il était venu un homme qui cherchait la prospérité des enfants d’Israël.
Sanbalati Mhoroni na Tobia afisa Mwamoni waliposikia juu ya jambo hili, waliudhika sana kwamba amekuja mtu kuinua ustawi wa Waisraeli.
11 Et je vins à Jérusalem, et je fus là trois jours.
Nilienda Yerusalemu, na baada ya kukaa huko siku tatu,
12 Et je me levai pendant la nuit, et un petit nombre d’hommes avec moi, et je ne dis à personne ce que Dieu avait mis en mon cœur de faire à Jérusalem; et je n’avais pas de bête avec moi, si ce n’est l’animal sur lequel j’étais assis.
nikaondoka wakati wa usiku pamoja na watu wachache. Sikuwa nimemwambia mtu yeyote kile ambacho Mungu wangu alikuwa ameweka moyoni mwangu kufanya kwa ajili ya Yerusalemu. Hapakuwepo na mnyama yeyote pamoja nami isipokuwa yule niliyekuwa nimempanda.
13 Or je sortis par la porte de la vallée pendant la nuit, et devant la fontaine du dragon, et à la porte du fumier; et je considérais le mur de Jérusalem abattu, et ses portes consumées par le feu.
Nikatoka nje usiku kupitia Lango la Bondeni, kuelekea Kisima cha Joka na Lango la Samadi, nikikagua kuta za Yerusalemu zilizokuwa zimebomolewa, na malango yake yaliyokuwa yameteketezwa kwa moto.
14 Je passai donc à la porte de la fontaine, et à l’aqueduc du roi, et il n’y avait pas d’endroit pour que la bête sur laquelle j’étais assis passât.
Kisha nikaelekea mpaka Lango la Chemchemi na Bwawa la Mfalme, lakini hapakuwepo nafasi ya kutosha kwa ajili ya mnyama wangu kupita,
15 Et je montai par le torrent pendant la nuit, et je considérais le mur; et, revenant, j’arrivai à la porte de la vallée, et je retournai.
kwa hiyo nikapandia bondeni usiku nikikagua ukuta. Mwishoni nikarudi na kuingia tena kupitia Lango la Bondeni.
16 Or les magistrats ne savaient où j’étais allé, ni ce que je faisais; bien plus, aux Juifs mêmes, aux prêtres, aux grands, aux magistrats, et à ceux qui faisaient l’ouvrage, je n’avais rien révélé jusque là.
Maafisa hawakujua nilikokwenda wala nilichokuwa nikifanya, kwa sababu mpaka sasa nilikuwa bado sijasema lolote kwa Wayahudi, wala makuhani, wala wakuu, wala maafisa, wala mtu yeyote ambaye angefanya kazi.
17 Je leur dis alors: Vous connaissez l’affliction dans laquelle nous sommes, puisque Jérusalem est déserte, et que ses portes ont été consumées par le feu: venez, et bâtissons les murs de Jérusalem, et ne soyons plus désormais un opprobre.
Ndipo nilipowaambia, “Mnaona taabu tuliyo nayo: Yerusalemu imebaki magofu na malango yake yameteketezwa kwa moto. Njooni tujenge upya ukuta wa Yerusalemu, nasi hatutakuwa tena katika aibu hii.”
18 Et je leur montrai que la main de mon Dieu était bonne pour moi, et les paroles du roi, qu’il m’avait adressées; et je dis: Levons-nous, et bâtissons. Et leurs mains furent affermies dans le bien.
Pia niliwaambia kuhusu mkono wenye neema wa Mungu wangu uliokuwa juu yangu, na kile mfalme alichokuwa ameniambia. Wakajibu, “Haya! Tuanze kujenga tena.” Kwa hiyo wakaanza kazi hii njema.
19 Or Sanaballat, l’Horonite, et Tobie, le serviteur Ammanite, et Gossem, l’Arabe, l’apprirent, et ils nous raillèrent, nous méprisèrent, et dirent: Qu’est-ce que vous faites? Ne vous révoltez-vous point contre le roi?
Lakini Sanbalati Mhoroni, Tobia afisa Mwamoni, na Geshemu Mwarabu waliposikia kuhusu jambo hili, walitudhihaki na kutucheka. Wakauliza, “Ni nini hiki mnachokifanya? Je, mnaasi dhidi ya mfalme?”
20 Et je leur rendis réponse et leur dis: Le Dieu du ciel lui-même nous aide, et nous, nous sommes ses serviteurs: levons-nous et bâtissons; mais pour vous il n’y a ni part, ni droit, ni souvenir en Jérusalem.
Nikawajibu kwa kusema, “Mungu wa mbinguni atatufanikisha. Sisi watumishi wake tutaanza kujenga upya, lakini kwenu ninyi, hamna sehemu wala dai lolote wala kumbukumbu la haki katika Yerusalemu.”