< Nahum 3 >

1 Malheur, cité de sang, tout entière au mensonge, pleine de brigandages; la rapine ne te quittera pas.
Ole kwa mji uliojaa damu! Wote umejaa uongo na mali za wizi; wahanga wapo kwake daima.
2 Voix du fouet et voix de l’impétuosité de la roue, et du cheval qui frémit, du quadrige brûlant, et du cavalier qui monte;
Lakini sasa kunasauti ya mijeledi na sauti za kugongesha matairi, farasi wakicheza, na magari ya vita yanaruka ruka.
3 Et du glaive brillant, et de la lance étincelante, et de la multitude tuée, et de la ruine cruelle; et les cadavres sont sans fin, et ils tomberont sur leurs corps morts.
Kuna wapanda farasi wanashambulia, Upanga unang'ara, mikuki inametameta, marundo ya maiti, mafungu makubwa ya miili; hakuna ukomo wa miili, washambuliaji wanajikwaa juu yake.
4 À cause de la multitude des fornications de la courtisane, belle et gracieuse, et possédant l’art des maléfices, laquelle a vendu des peuples par ses fornications, et des nations par ses maléfices;
Hii inatokea kwa sababu ya matendo ya tamaa ya kahaba mzuri, mzoefu wa uchawi, mwenye kuuza taifa kwa umalaya wake, na watu kwa njia ya matendo yake ya kichawi.
5 Voici que moi je viens vers toi, dit le Seigneur des armées, et je découvrirai ta honte à ta face, et je montrerai à des nations ta nudité, et à des royaumes ton ignominie.
“Tazama, mimi nipo kinyume na wewe- hili ni neno la Yehova wa majeshi- sketi yako nitaiinua juu ya uso wako na kuzionyesha sehemu zako za siri kwa mataifa, aibu yako kwa falme.
6 Et je jetterai sur toi tes abominations, et je te couvrirai d’infamie, et je ferai de toi un exemple.
Nitarusha uchafu wa kuchukiza na kukufanya uwe mbaya sana; nitakufanya uwe mtu wa kutazamwa na kila mmoja.
7 Et il arrivera que quiconque te verra se retirera de toi, et dira: Elle a été dévastée, Ninive; qui secouera la tête sur toi? où chercherai-je un consolateur pour toi?
Itakuwa kwamba kila mmoja anayekutazama atakukimbia na kusema, “Ninawi ameharibika; ni nani ataomboleza kwa ajili yake?' Ni wapi nitampata mtu anayeweza kukufariji?”
8 Est-ce que tu es meilleure qu’Alexandrie des peuples, qui habite au milieu des fleuves, environnée d’eaux; dont les richesses sont la mer et les eaux les murs?
Ninawi, je wewe ni bora kuliko Noamoni, uliojengwa juu ya Mto Naili, uliokuwa umezungukwa na maji, ambao ulinzi wake ilikuwa bahari, ambao ukuta wake ilikuwa bahari yenyewe?
9 L’Éthiopie était sa force, ainsi que l’Égypte, et il n’y a pas de fin; l’Afrique et la Libye sont venues à ton secours, ô Alexandrie.
Ethiopia na Misri zilikuwa nguvu zake, na mwisho wake haukuwepo; Putu na Libya walikuwa rafiki zake.
10 Et cependant elle-même a été emmenée en exil et en captivité; ses petits enfants ont été écrasés à l’entrée de toutes les rues; et sur ses hommes illustres on a jeté le sort, et tous ses grands ont été chargés d’entraves.
Lakini Noamoni alichukuliwa; alikwenda kwenye mateka; watoto wake wadogo walivunjwa vipande vipande katika kila makao makuu ya mtaa; adui zake walipiga kura kwa watu wake wenye heshima na wakuu wake wote walifungwa minyororo.
11 Et toi aussi, Ninive, tu seras donc enivrée, et tu seras méprisée; et tu demanderas du secours à un ennemi.
Wewe pia utalewa; utajaribu kujificha, na utatafuta makimbilio kutoka kwa adui yako.
12 Toutes tes fortifications seront comme des figuiers avec des figues précoces; s’ils sont secoués, elles tomberont dans la bouche de celui qui les mangera.
Ngome zako zote zitakuwa kama mitini yenye tini zilizoiva mapema: kama zikitikiswa, zitaangukia kwenye kimywa cha mlaji.
13 Voilà ton peuple, ce sont des femmes au milieu de toi; les portes de ta terre seront tout ouvertes à tes ennemis; un feu dévorera tes verroux.
Tazama, watu miongoni mwenu ni wanawake; malango ya nchi yako yamefunguliwa sana kwa ajili ya adui zako; moto umeharibu bawaba zake.
14 Puise de l’eau, à cause du siège; construis tes fortifications; entre dans l’argile, et foule-la aux pieds; en la mettant en œuvre, fais de la brique.
Nenda ukachote maji kwenye boma iliyozingirwa; ziimarishe ngome zako; nenda kwenye udongo na kandamiza matope; finyanga kwa ajili ya matofali.
15 Là, un feu te consumera; tu périras par le glaive, il te dévorera comme le bruchus; rassemble-toi comme le bruchus; multiplie-toi comme la sauterelle.
Moto utakuteketeza pale, na upanga utakuangamiza. Utateketezwa kama nzige wachanga wanavyoteketeza kila kitu. Ninyi wenyewe mjitengeneze kuwa wengi kama nzige wachanga, na wengi kama nzinge waliopevuka.
16 Tu as fait plus de trafics qu’il n’y a d’étoiles au ciel; le bruchus s’est répandu et envolé.
Umezidisha wafanyabiashara wako zaidi kuliko nyota mbinguni; lakini wapo kama tunutu: wanapora nchi na kisha kuruka kwenda mbali.
17 Tes gardes sont comme des sauterelles, et tes petits enfants comme les sauterelles des sauterelles qui se posent dans les haies dans un jour de froid; le soleil s’est levé, et elles se sont envolées et on ne connaît pas la place où elles ont été,
Wafalme wenu wapo wengi kama zinge, na wakuu wenu wa majeshi ni kama kundi la wadudu wenye kuweka kambi katika ukuta wakati wa baridi. Lakini jua linapowaka wanaruka kwenda mbali ambako hakuna anayepajua.
18 Ils se sont endormis, tes pasteurs, ô roi d’Assur, tes princes seront ensevelis dans le sommeil; ton peuple s’est caché dans les montagnes et il n’y a personne qui le rassemble.
Mfalme wa Ashuru, wachungaji wako wamelala; watawala wako wamejilaza chini kupumzika. Watu wako wametawanyika juu ya milima, na hakuna hata mmoja wa kuwakusanya.
19 Ta blessure n’est pas cachée, sa plaie est très maligne; tous ceux qui ont appris des nouvelles de toi ont frappé des mains à ton sujet; car sur qui ta malice ne s’est-elle pas toujours portée?
Hakuna uponyaji unaowezekana kwa ajili ya vidonda vyako. Vidonda vyako ni vikubwa. Wanaosikia habari juu yako watapiga makofi kwa furaha juu yako. Ni nani aliyejiepusha kwa uovu wako wa daima?

< Nahum 3 >