< Matthieu 8 >

1 Or, lorsqu’il fut descendu de la montagne, une grande foule le suivit:
Yesu aliposhuka kutoka mlimani, makundi mengi ya watu yalimfuata.
2 Et voilà qu’un lépreux venant à lui l’adorait, disant: Seigneur, si vous voulez, vous pouvez me guérir.
Basi, akaja mtu mmoja mwenye ukoma, akamsujudia akisema, “Bwana, ukitaka, waweza kunitakasa!”
3 Et Jésus étendant la main le toucha, disant: Je le veux, sois guéri. Et à l’instant sa lèpre fut guérie.
Yesu akanyosha mkono wake, akamgusa na kusema, “Nataka! Takasika.” Mara huyo mtu akapona ukoma wake.
4 Alors Jésus lui dit: Prends garde, ne le dis à personne, mais va, montre-toi au prêtre, et offre le don prescrit par Moïse, en témoignage pour eux.
Kisha Yesu akamwambia, “Sikiliza, usimwambie mtu yeyote, ila nenda ukajionyeshe kwa kuhani, na ukatoe sadaka iliyoamriwa na Mose kuwathibitishia kwamba umepona.”
5 Et comme il était entré dans Capharnaüm, un centurion s’approcha de lui, le priant,
Yesu alipokuwa anaingia mjini Kafarnaumu, ofisa mmoja Mroma alimwendea, akamsihi
6 Et disant: Seigneur, mon serviteur gît paralytique dans ma maison, et il souffre violemment.
akisema, “Mheshimiwa, mtumishi wangu amelala nyumbani, mgonjwa wa kupooza na anaumwa sana.”
7 Jésus lui dit: J’irai, et le guérirai.
Yesu akamwambia, “Nitakuja kumponya.”
8 Mais le centurion répondant: Seigneur, dit-il, je ne suis pas digne que vous entriez sous mon toit; mais dites seulement une parole et mon serviteur sera guéri.
Huyo ofisa akamwambia, “Mheshimiwa, sistahili uingie nyumbani mwangu. Lakini sema tu neno, na mtumishi wangu atapona.
9 Car moi qui suis un homme soumis à la puissance d’un autre et qui ai sous moi des soldats, je dis à l’un: Va, et il va; et à un autre: Viens, et il vient, et à mon serviteur: Fais cela, et il le fait.
Maana, hata mimi niliye mtu chini ya mamlaka ya wengine, ninao askari chini yangu. Namwambia mmoja, Nenda! naye huenda; na mwingine, Njoo! naye huja; na mtumishi wangu, Fanya kitu hiki! naye hufanya.”
10 Or Jésus, l’entendant, fut dans l’admiration, et il dit à ceux qui le suivaient: En vérité, je vous le dis; je n’ai pas trouvé une si grande foi dans Israël.
Yesu aliposikia hayo, alistaajabu, akawaambia watu waliokuwa wanamfuata, “Kweli nawaambieni, sijapata kumwona mtu yeyote katika Israeli aliye na imani kama hii.
11 Aussi je vous dis que beaucoup viendront de l’Orient et de l’Occident et auront place dans le royaume des cieux avec Abraham, Isaac et Jacob;
Basi, nawaambieni kwamba watu wengi watakuja kutoka mashariki na magharibi, nao wataketi karamuni pamoja na Abrahamu, Isaka na Yakobo katika Ufalme wa mbinguni.
12 Tandis que les enfants du royaume seront jetés dans les ténèbres extérieures; là sera le pleur et le grincement de dents.
Lakini wale ambao wangalipaswa kuwa katika Ufalme huo watatupwa nje, gizani, ambako watalia na kusaga meno.”
13 Alors Jésus dit au centurion: Va, et que selon que tu as cru il te soit fait. Et son serviteur fut guéri à cette heure même.
Kisha Yesu akamwambia huyo ofisa Mroma, “Nenda nyumbani; na iwe kama ulivyoamini.” Na mtumishi wake akapona saa ileile.
14 Jésus étant venu ensuite dans la maison de Pierre vit sa belle-mère gisante et ayant la fièvre.
Yesu alifika nyumbani kwa Petro, akamkuta mama mkwe wa Petro amelala kitandani, ana homa kali.
15 Il lui toucha la main, et la fièvre la quitta; aussitôt elle se leva, et elle les servait.
Basi, Yesu akamgusa huyo mama mkono, na homa ikamwacha; akasimama, akamtumikia.
16 Le soir étant venu, on lui présenta beaucoup de démoniaques, et par sa parole il chassait les malins esprits, et il guérit tous les malades:
Ilipokuwa jioni, walimletea watu wengi waliokuwa wamepagawa na pepo; naye, kwa kusema neno tu, akawafukuza hao pepo. Aliwaponya pia watu wote waliokuwa wagonjwa.
17 Afin que s’accomplît la parole du prophète Isaïe, disant: Lui-même a pris nos infirmités et il s’est chargé de nos maladies.
Alifanya hivyo ili yale aliyosema nabii Isaya yatimie: “Yeye mwenyewe ameondoa udhaifu wetu, ameyachukua magonjwa yetu.”
18 Or Jésus voyant une grande foule autour de lui ordonna de passer à l’autre côté de la mer.
Yesu alipoona kundi la watu limemzunguka, aliwaamuru wanafunzi wake waende ng'ambo ya ziwa.
19 Alors un scribe s’approchant, lui dit: Maître, je vous suivrai partout où vous irez.
Mwalimu mmoja wa Sheria akamwendea, akamwambia, “Mwalimu, mimi nitakufuata kokote uendako.”
20 Et Jésus lui dit: Les renards ont des tanières, et les oiseaux du ciel des nids; mais le Fils de l’homme n’a pas où reposer sa tête.
Yesu akamjibu, “Mbweha wana mapango, na ndege wana viota; lakini Mwana wa Mtu hana mahali pa kupumzikia.”
21 Un autre de ses disciples lui dit: Seigneur, permettez-moi racontèrent d’aller d’abord et d’ensevelir mon père.
Kisha mtu mwingine miongoni mwa wanafunzi wake akamwambia, “Bwana, niruhusu kwanza niende nikamzike baba yangu.”
22 Mais Jésus lui dit: Suis-moi et laisse les morts ensevelir leurs morts.
Lakini Yesu akamwambia, “Nifuate! Waache wafu wazike wafu wao.”
23 Étant ensuite monté dans la barque, ses disciples le suivirent
Yesu alipanda mashua, na wanafunzi wake wakaenda pamoja naye.
24 Et voilà qu’une grande tempête se leva sur la mer; de sorte que la barque était couverte par les vagues; lui-même cependant dormait.
Ghafla, dhoruba kali ikatokea ziwani, hata mawimbi yakaanza kuifunika mashua. Yesu alikuwa amelala usingizi.
25 C’est pourquoi ses disciples s’approchèrent de lui et l’éveillèrent, disant: Seigneur, sauvez-nous, nous périssons.
Wanafunzi wakamwendea, wakamwamsha wakisema, “Bwana, tuokoe, tunaangamia!”
26 Jésus leur dit: Pourquoi craignez-vous, hommes de peu de foi? Alors, se levant, il commanda aux vents et à la mer, et il se fit un grand calme.
Yesu akawaambia, “Enyi watu wenye imani haba; mbona mnaogopa?” Basi, akainuka, akazikemea pepo na mawimbi; kukawa shwari kabisa.
27 Or, saisis d’admiration, ces hommes disaient: Quel est celui-ci, que les vents et la mer lui obéissent?
Watu wakashangaa, wakasema, “Ni mtu wa namna gani huyu? Hata pepo na mawimbi vinamtii!”
28 Lorsqu’il fut venu de l’autre côté de la mer, dans le pays des Géraséniens, coururent au-devant de lui deux démoniaques, sortant des sépulcres extrêmement furieux, au point que personne n’osait passer par ce chemin;
Yesu alifika katika nchi ya Wagerasi, ng'ambo ya ziwa, na huko watu wawili waliopagawa na pepo wakakutana naye wakitokea makaburini. Watu hawa walikuwa wenye kutisha mno, hata hakuna mtu aliyethubutu kupita katika njia hiyo.
29 Et ils se mirent à crier, disant: Qu’importe à nous et à vous, Jésus fils de Dieu? Êtes-vous venu ici avant le temps pour nous tourmenter?
Nao wakaanza kupiga kelele, “Una shauri gani nasi, wewe Mwana wa Mungu? Je, umekuja kututesa kabla ya wakati wake?”
30 Or était non loin d’eux un grand troupeau de pourceaux qui paissaient;
Karibu na mahali hapo kulikuwa na nguruwe wengi wakichungwa.
31 Et les démons le priaient, disant: Si vous nous chassez d’ici, envoyez-nous dans ce troupeau de pourceaux.
Basi, hao pepo wakamsihi, “Ikiwa utatutoa, basi uturuhusu tuwaingie nguruwe wale.”
32 Il leur répondit: Allez. Eux donc, étant sortis, entrèrent dans les pourceaux; et voilà que le troupeau tout entier se précipita impétueusement dans la mer; et ils moururent dans les eaux.
Yesu akawaambia, “Haya, nendeni.” Hapo wakawatoka watu hao, wakawaingia nguruwe. Kundi lote la nguruwe likaporomoka kwenye ule mteremko mkali, likatumbukia ziwani; nguruwe wote wakafa maji.
33 Et les gardiens s’enfuirent; et venant dans la ville, ils racontèrent tout ceci, et le sort de ceux qui avaient été démoniaques.
Wachungaji wa hao nguruwe walikimbia, wakaenda mjini. Huko walitoa habari zote na mambo yaliyowapata wale watu waliokuwa wamepagawa.
34 Aussitôt toute la ville sortit au-devant de Jésus; et l’ayant vu, ils le priaient de sortir de leurs confins.
Basi, watu wote katika mji ule walitoka, wakamwendea Yesu; na walipomwona, wakamsihi aondoke katika nchi yao.

< Matthieu 8 >