< Malachie 1 >
1 Malheur accablant de la parole du Seigneur, adressée à Israël, par l’entremise de Malachie.
Ujumbe: Neno la Bwana kwa Israeli kupitia kwa Malaki.
2 Je vous ai aimés, dit le Seigneur, et vous avez dit: En quoi nous avez-vous aimés? Est-ce qu’Esaü n’était pas frère de Jacob? dit le Seigneur, et j’ai aimé Jacob;
Bwana asema, “Nimewapenda ninyi.” “Lakini ninyi mnauliza, ‘Wewe umetupendaje?’” Bwana asema, “Je, Esau hakuwa ndugu yake Yakobo? Hata hivyo nimempenda Yakobo,
3 Mais j’ai haï Esaü; et j’ai fait de ses montagnes une solitude, et j’ai abandonné son héritage aux dragons du désert.
lakini nikamchukia Esau, nami nimeifanya milima yake kuwa ukiwa, na urithi wake nimewapa mbweha wa jangwani.”
4 Que si l’Idumée dit: Nous avons été détruits, mais revenant nous bâtirons ce qui a été détruit: voici ce que dit le Seigneur des armées: Ceux-ci bâtiront, et moi je détruirai; et ils seront appelés bornes d’impiété et peuple contre qui le Seigneur s’est irrité jusqu’à jamais.
Edomu anaweza kusema, “Ingawa tumepondapondwa, tutajenga upya magofu.” Lakini hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Wanaweza kujenga, lakini nitabomoa. Wataitwa Nchi Ovu, watu ambao siku zote wapo chini ya ghadhabu ya Bwana.
5 Et vos yeux verront, et vous direz: Que le Seigneur soit magnifié par delà les limites d’Israël.
Mtayaona kwa macho yenu wenyewe na kusema, ‘Bwana ni mkuu, hata nje ya mipaka ya Israeli!’
6 Un fils honore son père et un serviteur son maître; si donc moi, je suis votre père, où est mon honneur? et si moi, je suis votre Seigneur, où est la crainte de moi? dit le Seigneur des armées, à vous, ô prêtres, qui méprisez mon nom, et qui dites: En quoi avons-nous méprisé votre nom?
“Mwana humheshimu baba yake, naye mtumishi humheshimu bwana wake. Kama mimi ni baba, iko wapi heshima ninayostahili? Kama mimi ni bwana, iko wapi heshima ninayostahili?” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Ni ninyi, enyi makuhani, mnaolidharau Jina langu. “Lakini mnauliza, ‘Tumelidharau Jina lako kwa namna gani?’
7 Vous offrez sur mon autel un pain souillé, et vous dites: En quoi vous avons-nous souillé? En ce que vous dites: La table du Seigneur est méprisée.
“Mnatoa sadaka chakula kilichotiwa unajisi juu ya madhabahu yangu. “Lakini ninyi mnauliza, ‘Tumekutia unajisi kwa namna gani?’ “Kwa kusema kuwa meza ya Bwana ni ya kudharauliwa.
8 Si vous offrez un animal aveugle pour être immolé, n’est-ce pas un mal? et si vous en offrez un boiteux ou malade, n’est-ce pas un mal? offre-le à ton gouverneur pour voir s’il lui plaira, ou s’il accueillera ta face, dit le Seigneur des armées.
Wakati mletapo dhabihu za wanyama walio vipofu, je, hilo si kosa? Mnapoleta dhabihu zilizo vilema au wanyama wagonjwa, je, hilo si kosa? Jaribuni kuvitoa kwa mtawala wenu! Je, angefurahishwa nanyi? Je, atawakubalia?” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
9 Et maintenant implorez la face du Seigneur, afin qu’il ait pitié de vous (car c’est par votre main que cela a été fait), pour voir si de quelque manière il accueillera vos faces, dit le Seigneur des armées.
“Basi mwombeni Mungu awe na neema kwetu. Je, kwa sadaka kama hizo kutoka mikononi mwenu, atawapokea?” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
10 Qui est celui parmi vous qui ferme les portes de mon temple, et qui allume le feu sur mon autel gratuitement? mon affection n’est pas en vous, dit le Seigneur des armées, et je ne recevrai pas de présent de votre main.
“Laiti mmoja wenu angalifunga milango ya Hekalu, ili msije mkawasha moto usiokuwa na faida juu ya madhabahu yangu! Sina furaha nanyi,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, “nami sitaikubali sadaka toka mikononi mwenu.
11 Car, depuis le lever du soleil jusqu’à son coucher, grand est mon nom parmi les nations; et en tout lieu l’on sacrifie, et une oblation pure est offerte à mon nom, parce que grand est mon nom parmi les nations, dit le Seigneur des armées.
Jina langu litakuwa kuu miongoni mwa mataifa, kuanzia mawio ya jua hata machweo yake. Kila mahali uvumba na sadaka safi zitaletwa kwa Jina langu, kwa sababu Jina langu litakuwa kuu miongoni mwa mataifa,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
12 Et vous l’avez souillé en ce que vous dites: La table du Seigneur est souillée; et ce qu’on pose dessus est méprisable, aussi bien que le feu qui le dévore.
“Lakini mnalinajisi Jina langu kwa kusema kuhusu meza ya Bwana, ‘Imetiwa unajisi pamoja na chakula chake. Ni ya kudharauliwa.’
13 Et vous avez dit: Voilà de notre travail, et vous avez soufflé dessus, dit le Seigneur des armées; et vous avez amené un animal boiteux et malade, fruit de vos rapines, et vous l’offrez en présent; est-ce que je le recevrai de votre main? dit le Seigneur.
Nanyi mnasema, ‘Mzigo gani huu!’ Nanyi mnaidharau kwa kiburi,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Wakati mnapowaleta wanyama mliopokonya kwa nguvu, walio vilema au walio wagonjwa na kuwatoa kama dhabihu, je, niwakubali kutoka mikononi mwenu?” asema Bwana.
14 Maudit le fourbe qui a dans son troupeau un mâle, et qui faisant un vœu, immole un animal débile au Seigneur; parce que je suis le grand roi, dit le Seigneur des armées, et mon nom est terrible parmi les nations.
“Amelaaniwa yeye adanganyaye, aliye na mnyama wa kiume anayekubalika katika kundi lake na kuweka nadhiri ya kumtoa, lakini akatoa dhabihu ya mnyama aliye na dosari kwa Bwana. Kwa kuwa mimi ni Mfalme Mkuu, nalo Jina langu linapaswa kuogopwa miongoni mwa mataifa,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.