< Luc 21 >

1 Or Jésus, regardant, vit des riches qui mettaient leurs aumônes dans le tronc.
Yesu alitazama kwa makini, akawaona matajiri walivyokuwa wanatia sadaka zao katika hazina ya Hekalu,
2 Il vit aussi une pauvre veuve mettant deux petites pièces de monnaie.
akamwona pia mama mmoja mjane akitumbukiza humo sarafu mbili ndogo.
3 Et il dit: En vérité, je vous le dis, cette pauvre veuve a mis plus que tous les autres.
Basi, akasema, “Nawaambieni kweli, mama huyu mjane ametia zaidi katika hazina kuliko wote.
4 Car tous ceux-là ont mis pour offrandes à Dieu, de leur superflu; mais elle, elle a mis de son indigence même, tout le vivre qu’elle avait.
Kwa maana, wengine wote wametoa sadaka zao kutokana na ziada ya mali zao, lakini huyu mama, ingawa ni maskini, ametoa kila kitu alichohitaji kwa kuishi.”
5 Et quelques-uns disant du temple, qu’il était bâti de belles pierres, et orné de dons, il répondit:
Baadhi ya wanafunzi walikuwa wanazungumza juu ya Hekalu, jinsi lilivyopambwa kwa mawe ya thamani, pamoja na sadaka zilizotolewa kwa Mungu. Yesu akasema,
6 Viendront des jours où de ce que vous voyez, il ne restera pas pierre sur pierre, qui ne soit détruite.
“Haya yote mnayoyaona—zitakuja siku ambapo hakuna hata jiwe moja litakalosalia juu ya lingine; kila kitu kitaharibiwa.”
7 Et ils l’interrogèrent, disant: Maître, quand ces choses arriveront-elles, et quel sera le signe qu’elles commenceront de s’accomplir?
Basi, wakamwuliza, “Mwalimu, mambo hayo yatatokea lini? Na ni ishara gani zitakazoonyesha kwamba karibu mambo hayo yatokee?”
8 Jésus dit: Prenez garde d’être séduits; car beaucoup viendront en mon nom, disant: C’est moi, et le temps approche; ne les suivez donc point.
Yesu akawajibu, “Jihadharini, msije mkadanganyika. Maana wengi watatokea na kulitumia jina langu wakisema: Mimi ndiye, na, Wakati ule umekaribia. Lakini ninyi msiwafuate!
9 Et quand vous entendrez parler de guerres et de séditions, n’en soyez point effrayés; il faut auparavant que ces choses arrivent; mais ce n’est pas encore sitôt la fin.
Basi, mtakaposikia habari za vita na misukosuko, msitishike; maana ni lazima hayo yatokee kwanza, lakini mwisho wa yote, bado.”
10 Alors il leur disait: Une nation se soulèvera contre une nation, un royaume contre un royaume.
Halafu akaendelea kusema: “Taifa moja litapigana na taifa lingine, na ufalme mmoja utapigana na ufalme mwingine.
11 Il y aura de grands tremblements de terre en divers lieux, et des pestes, et des famines, et des signes effrayants dans le ciel, et de grands prodiges.
Kila mahali kutakuwa na mitetemeko mikubwa ya ardhi, kutakuwa na njaa na tauni. Kutakuwa na vituko vya kutisha na ishara kubwa angani.
12 Mais avant tout cela, on mettra la main sur vous, et on vous persécutera, vous livrant aux synagogues et aux prisons, vous traînant devant les rois et les gouverneurs à cause de mon nom.
Lakini kabla ya kutokea hayo yote, watawatieni nguvuni, watawatesa na kuwapelekeni katika masunagogi na kuwatia gerezani; mtapelekwa mbele ya wafalme na watawala kwa ajili ya jina langu.
13 Or cela vous arrivera en témoignage.
Hii itawapeni fursa ya kushuhudia Habari Njema.
14 Mettez donc bien dans vos cœurs de ne point préméditer comment vous répondrez.
Muwe na msimamo huu mioyoni mwenu: hakuna kufikiria kabla ya wakati juu ya jinsi mtakavyojitetea,
15 Car je vous donnerai moi-même une bouche et une sagesse à laquelle tous vos adversaires ne pourront résister, ni rien opposer.
kwa sababu mimi mwenyewe nitawapeni ufasaha wa maneno na hekima, hivyo kwamba zenu hawataweza kustahimili wala kupinga.
16 Vous serez livrés par vos pères et vos mères, par vos frères, vos parents et vos amis, et ils en mettront à mort d’entre vous.
Wazazi wenu, ndugu, jamaa na rafiki zenu watawasaliti ninyi; na baadhi yenu mtauawa.
17 Et vous serez en haine à tous à cause de mon nom;
Watu wote watawachukieni kwa sababu ya jina langu.
18 Mais pas un cheveu de votre tête ne périra.
Lakini, hata unywele mmoja wa vichwa vyenu hautapotea.
19 C’est par votre patience que vous posséderez vos âmes.
Kwa uvumilivu wenu, mtayaokoa maisha yenu.
20 Or, quand vous verrez Jérusalem investie par une armée, sachez que sa désolation est proche:
“Mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, ndipo mtambue ya kwamba wakati umefika ambapo mji huo utaharibiwa.
21 Alors, que ceux qui sont dans la Judée fuient vers les montagnes, que ceux qui sont au milieu d’elle s’en éloignent; et que ceux qui sont dans les contrées n’y entrent point.
Hapo walioko Yudea wakimbilie milimani; wale walio mjini watoke; na wale walio mashambani wasirudi mjini.
22 Parce que ce sont là des jours de vengeance, afin que s’accomplisse tout ce qui est écrit.
Kwa maana siku hizo ni siku za adhabu, ili yote yaliyoandikwa yatimie.
23 Mais malheur aux femmes enceintes et à celles qui nourriront en ces jours-là; car il y aura une détresse affreuse dans le pays, et une grande colère contre ce peuple.
Ole wao waja wazito na wanyonyeshao siku hizo! Kwa maana kutakuwa na dhiki kubwa katika nchi, na hasira ya Mungu itawajia watu hawa.
24 Ils tomberont sous le tranchant du glaive, et seront emmenés captifs dans toutes les nations, et Jérusalem sera foulée aux pieds par les gentils, jusqu’à ce que les temps des nations soient accomplis.
Wengine watauawa kwa upanga, wengine watachukuliwa mateka katika nchi zote; na mji wa Yerusalemu utakanyagwa na watu wa mataifa mengine, hadi nyakati zao zitakapotimia.
25 Et il y aura des signes dans le soleil, dans la lune et dans les étoiles; et, sur la terre, la détresse des nations, à cause du bruit confus de la mer et des flots;
“Kutakuwa na ishara katika jua na mwezi na nyota. Mataifa duniani yatakuwa na dhiki kwa sababu ya wasiwasi kutokana na mshindo wa mawimbi ya bahari.
26 Les hommes séchant de frayeur dans l’attente de ce qui doit arriver à tout l’univers; car les vertus des cieux seront ébranlées;
Watu watazirai kwa sababu ya uoga, wakitazamia mambo yatakayoupata ulimwengu; kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.
27 Et alors ils verront le Fils de l’homme venant dans une nuée, avec une grande puissance et une grande majesté.
Halafu, watamwona Mwana wa Mtu akija katika wingu, mwenye nguvu na utukufu mwingi.
28 Or, quand ces choses commenceront à s’accomplir, regardez et levez la tête, parce que votre rédemption approche.
Wakati mambo hayo yatakapoanza kutukia, simameni na kuinua vichwa vyenu juu, kwa maana ukombozi wenu umekaribia.”
29 Et il leur dit cette comparaison: Voyez le figuier et tous les arbres;
Kisha akawaambia mfano: “Angalieni mtini na miti mingine yote.
30 Quand ils commencent à produire du fruit, vous savez que l’été est proche.
Mnapoona kwamba imeanza kuchipua majani, mwatambua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia.
31 De même vous, quand vous verrez ces choses arriver, sachez que le royaume de Dieu est proche.
Vivyo hivyo, mtakapoona mambo hayo yanatendeka, mtatambua kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
32 En vérité, je vous le dis, cette génération ne passera point, jusqu’à ce que toutes ces choses soient accomplies.
Nawaambieni hakika, kizazi hiki cha sasa hakitapita kabla ya hayo yote kutendeka.
33 Le ciel et la terre passeront; mais mes paroles ne passeront point.
Mbingu na dunia vitapita, lakini maneno yangu hayatapita.
34 Faites donc attention à vous, de peur que vos cœurs ne s’appesantissent dans la crapule, l’ivresse et les soins de cette vie, et que ce jour ne vienne soudainement sur vous.
“Muwe macho, mioyo yenu isije ikalemewa na anasa, ulevi na shughuli za maisha haya. La sivyo, Siku ile itawajieni ghafla.
35 Car, comme un filet, il enveloppera tous ceux qui habitent sur la face de la terre.
Kwa maana itawajia kama mtego, wote wanaoishi duniani pote.
36 Veillez donc et priez en tout temps, afin que vous soyez trouvés dignes d’éviter toutes ces choses qui doivent arriver, et de paraître avec confiance devant le Fils de l’homme.
Muwe waangalifu basi, na salini daima ili muweze kupata nguvu ya kupita salama katika mambo haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele ya Mwana wa Mtu.”
37 Or, le jour il enseignait dans le temple; mais la nuit, sortant, il se retirait sur la montagne appelée des Oliviers.
Wakati wa mchana, siku hizo, Yesu alikuwa akifundisha watu Hekaluni; lakini usiku alikuwa akienda katika mlima wa Mizeituni na kukaa huko.
38 Et tout le peuple venait de grand matin vers lui au temple pour l’écouter.
Watu wote walikuwa wanakwenda Hekaluni asubuhi na mapema, wapate kumsikiliza.

< Luc 21 >