< Luc 21 >
1 Or Jésus, regardant, vit des riches qui mettaient leurs aumônes dans le tronc.
Yesu alipoinua macho yake, aliwaona matajiri wakiweka sadaka zao kwenye sanduku la hazina ya Hekalu.
2 Il vit aussi une pauvre veuve mettant deux petites pièces de monnaie.
Akamwona pia mjane mmoja maskini akiweka humo sarafu mbili ndogo za shaba.
3 Et il dit: En vérité, je vous le dis, cette pauvre veuve a mis plus que tous les autres.
Yesu akasema, “Amin, nawaambia, huyu mjane maskini ameweka humo zaidi ya watu wengine wote.
4 Car tous ceux-là ont mis pour offrandes à Dieu, de leur superflu; mais elle, elle a mis de son indigence même, tout le vivre qu’elle avait.
Hawa watu wengine wote wametoa sadaka kutokana na wingi wa mali zao. Lakini huyu mjane ametoa kutokana na umaskini wake vyote alivyokuwa navyo, hata kile alichohitaji ili kuishi.”
5 Et quelques-uns disant du temple, qu’il était bâti de belles pierres, et orné de dons, il répondit:
Baadhi ya wanafunzi wake wakawa wanamwonyesha jinsi Hekalu lilivyopambwa kwa mawe mazuri na kwa vitu vilivyotolewa kuwa sadaka kwa Mungu. Lakini Yesu akawaambia,
6 Viendront des jours où de ce que vous voyez, il ne restera pas pierre sur pierre, qui ne soit détruite.
“Kuhusu haya mnayoyaona hapa, wakati utafika ambapo hakuna jiwe moja litakalobaki juu ya jingine, bali kila moja litabomolewa.”
7 Et ils l’interrogèrent, disant: Maître, quand ces choses arriveront-elles, et quel sera le signe qu’elles commenceront de s’accomplir?
Wakamuuliza, “Mwalimu, mambo haya yatatukia lini? Ni dalili gani itaonyesha kwamba yanakaribia kutendeka?”
8 Jésus dit: Prenez garde d’être séduits; car beaucoup viendront en mon nom, disant: C’est moi, et le temps approche; ne les suivez donc point.
Yesu akawajibu, “Jihadharini msije mkadanganywa. Maana wengi watakuja kwa Jina langu, wakidai, ‘Mimi ndiye,’ na, ‘Wakati umekaribia.’ Msiwafuate.
9 Et quand vous entendrez parler de guerres et de séditions, n’en soyez point effrayés; il faut auparavant que ces choses arrivent; mais ce n’est pas encore sitôt la fin.
Lakini msikiapo habari za vita na machafuko, msiogope. Kwa maana hayo ni lazima yatokee kwanza, ila ule mwisho hautakuja wakati huo.”
10 Alors il leur disait: Une nation se soulèvera contre une nation, un royaume contre un royaume.
Kisha akawaambia: “Taifa litainuka dhidi ya taifa jingine, na ufalme mmoja dhidi ya ufalme mwingine.
11 Il y aura de grands tremblements de terre en divers lieux, et des pestes, et des famines, et des signes effrayants dans le ciel, et de grands prodiges.
Kutakuwa na mitetemeko mikubwa ya ardhi, na njaa kali, na magonjwa ya kuambukiza katika sehemu mbalimbali. Pia kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara kuu kutoka mbinguni.
12 Mais avant tout cela, on mettra la main sur vous, et on vous persécutera, vous livrant aux synagogues et aux prisons, vous traînant devant les rois et les gouverneurs à cause de mon nom.
“Lakini kabla yote hayajatokea, watawakamata ninyi na kuwatesa. Watawatia mikononi mwa wakuu wa masinagogi na kuwafunga magerezani. Nanyi mtapelekwa mbele ya wafalme na watawala kwa ajili ya Jina langu.
13 Or cela vous arrivera en témoignage.
Hii itawapa nafasi ya kushuhudia.
14 Mettez donc bien dans vos cœurs de ne point préméditer comment vous répondrez.
Lakini kusudieni mioyoni mwenu msisumbuke awali kuhusu mtakalosema mbele ya mashtaka.
15 Car je vous donnerai moi-même une bouche et une sagesse à laquelle tous vos adversaires ne pourront résister, ni rien opposer.
Kwa maana nitawapa maneno na hekima ambayo hakuna hata adui yenu mmoja atakayeweza kushindana nayo wala kuipinga.
16 Vous serez livrés par vos pères et vos mères, par vos frères, vos parents et vos amis, et ils en mettront à mort d’entre vous.
Mtasalitiwa hata na wazazi, ndugu, jamaa na marafiki, na baadhi yenu watawaua.
17 Et vous serez en haine à tous à cause de mon nom;
Mtachukiwa na watu wote kwa ajili ya Jina langu.
18 Mais pas un cheveu de votre tête ne périra.
Lakini hapatakuwa na unywele mmoja wa kichwa chenu utakaoangamia.
19 C’est par votre patience que vous posséderez vos âmes.
Kwa kuvumilia mtaokoa roho zenu.
20 Or, quand vous verrez Jérusalem investie par une armée, sachez que sa désolation est proche:
“Mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, basi fahamuni kwamba kuharibiwa kwake kumekaribia.
21 Alors, que ceux qui sont dans la Judée fuient vers les montagnes, que ceux qui sont au milieu d’elle s’en éloignent; et que ceux qui sont dans les contrées n’y entrent point.
Wakati huo, wale walio Uyahudi wakimbilie milimani, walio mjini Yerusalemu watoke humo, nao wale walioko mashambani wasiingie mjini.
22 Parce que ce sont là des jours de vengeance, afin que s’accomplisse tout ce qui est écrit.
Kwa sababu huu utakuwa ni wakati wa adhabu ili kutimiza yote yaliyoandikwa.
23 Mais malheur aux femmes enceintes et à celles qui nourriront en ces jours-là; car il y aura une détresse affreuse dans le pays, et une grande colère contre ce peuple.
Ole wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo! Kutakuwa na dhiki kuu katika nchi na ghadhabu juu ya hawa watu.
24 Ils tomberont sous le tranchant du glaive, et seront emmenés captifs dans toutes les nations, et Jérusalem sera foulée aux pieds par les gentils, jusqu’à ce que les temps des nations soient accomplis.
Wataanguka kwa makali ya upanga, na wengine watachukuliwa kuwa mateka katika mataifa yote. Nao mji wa Yerusalemu utakanyagwa na watu wa Mataifa hadi muda wa hao watu wa Mataifa utimie.
25 Et il y aura des signes dans le soleil, dans la lune et dans les étoiles; et, sur la terre, la détresse des nations, à cause du bruit confus de la mer et des flots;
“Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Hapa duniani, mataifa yatakuwa katika dhiki na fadhaa kutokana na ngurumo na misukosuko ya bahari.
26 Les hommes séchant de frayeur dans l’attente de ce qui doit arriver à tout l’univers; car les vertus des cieux seront ébranlées;
Watu watazimia roho kutokana na hofu kuu na kuyaona yale mambo yanayotokea duniani, kwa maana nguvu za angani zitatikisika.
27 Et alors ils verront le Fils de l’homme venant dans une nuée, avec une grande puissance et une grande majesté.
Wakati huo ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni pamoja na uweza na utukufu mkuu.
28 Or, quand ces choses commenceront à s’accomplir, regardez et levez la tête, parce que votre rédemption approche.
Mambo haya yatakapoanza kutendeka, simameni na mkaviinue vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umekaribia.”
29 Et il leur dit cette comparaison: Voyez le figuier et tous les arbres;
Akawaambia mfano huu: “Uangalieni mtini na miti mingine yote.
30 Quand ils commencent à produire du fruit, vous savez que l’été est proche.
Inapochipua majani, ninyi wenyewe mnaweza kuona na kutambua wenyewe ya kuwa wakati wa kiangazi umekaribia.
31 De même vous, quand vous verrez ces choses arriver, sachez que le royaume de Dieu est proche.
Vivyo hivyo, myaonapo mambo haya yakitukia, mnatambua kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
32 En vérité, je vous le dis, cette génération ne passera point, jusqu’à ce que toutes ces choses soient accomplies.
“Amin, nawaambia, kizazi hiki hakitapita hadi mambo haya yote yawe yametimia.
33 Le ciel et la terre passeront; mais mes paroles ne passeront point.
Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.”
34 Faites donc attention à vous, de peur que vos cœurs ne s’appesantissent dans la crapule, l’ivresse et les soins de cette vie, et que ce jour ne vienne soudainement sur vous.
“Jihadharini mioyo yenu isije ikalemewa na anasa, ulevi na fadhaa za maisha haya, nayo siku ile ikawakuta ninyi bila kutazamia kama vile mtego unasavyo.
35 Car, comme un filet, il enveloppera tous ceux qui habitent sur la face de la terre.
Kwa maana kama vile mtego unasavyo, ndivyo siku hiyo itakavyowapata wanadamu wote waishio katika uso wa dunia yote.
36 Veillez donc et priez en tout temps, afin que vous soyez trouvés dignes d’éviter toutes ces choses qui doivent arriver, et de paraître avec confiance devant le Fils de l’homme.
Kesheni daima na mwombe ili mweze kuokoka na yale yote yatakayotokea na kusimama mbele ya Mwana wa Adamu.”
37 Or, le jour il enseignait dans le temple; mais la nuit, sortant, il se retirait sur la montagne appelée des Oliviers.
Kila siku Yesu alikuwa akifundisha Hekaluni, na jioni ilipofika, alikwenda zake kwenye Mlima wa Mizeituni na kukaa huko usiku kucha.
38 Et tout le peuple venait de grand matin vers lui au temple pour l’écouter.
Nao watu wote walikuja asubuhi na mapema Hekaluni ili kumsikiliza.