< Luc 12 >

1 Cependant une grande multitude s’étant assemblée autour de lui, de sorte qu’ils marchaient les uns sur les autres, il commença à dire à ses disciples: Gardez-vous du levain des pharisiens, qui est l’hypocrisie.
Wakati watu kwa maelfu walipokuwa wamekusanyika hata wakawa wanakanyagana, Yesu aliwaambia kwanza wanafunzi wake, “Jihadharini na chachu ya Mafarisayo, yaani unafiki.
2 Car rien de caché qui ne se révèle, ni de secret qui ne se sache.
Kila kilichofunikwa kitafunuliwa, kila kilichofichika kitafichuliwa.
3 Ainsi ce que vous avez dit dans les ténèbres se dira à la lumière; et ce que vous avez dit à l’oreille, dans les chambres à coucher, sera publié sur les toits.
Kwa hiyo, kila mliyosema gizani, watu watayasikia katika mwanga, na kila mliyonong'ona faraghani milango imefungwa, yatatangazwa juu ya nyumba.
4 Or je vous dis à vous, qui êtes mes amis: Ne craignez point ceux qui tuent le corps, et après cela ne peuvent plus rien faire.
“Nawaambieni ninyi rafiki zangu: msiwaogope wale wanaoua mwili, wasiweze kufanya kitu kingine zaidi.
5 Mais je vous montrerai qui vous devez craindre: Craignez celui qui, après avoir ôté la vie, a le pouvoir d’envoyer dans la géhenne: oui, je vous le dis, craignez celui-là. (Geenna g1067)
Nitawaonyesheni yule ambaye ni lazima kumwogopa: mwogopeni yule ambaye baada ya kuua ana uwezo wa kumtupa mtu katika moto wa Jehanamu. Naam, ninawaambieni, mwogopeni huyo. (Geenna g1067)
6 Cinq passereaux ne se vendent-ils pas deux as, et cependant pas un d’eux n’est en oubli devant Dieu?
Inajulikana kwamba shomoro watano huuzwa kwa senti kumi, au sivyo? Lakini mbele ya Mungu hasahauliki hata mmoja.
7 Les cheveux mêmes de votre tête sont tous comptés. Ne craignez donc point, vous valez plus que beaucoup de passereaux.
Lakini hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote. Msiogope, basi, ninyi mna thamani zaidi kuliko shomoro wengi!
8 Or je vous le dis: Quiconque m’aura confessé devant les hommes, le Fils de l’homme aussi le confessera devant les anges de Dieu.
“Nawaambieni kweli, kila mtu anayekiri hadharani kwamba yeye ni wangu, Mwana wa Mtu naye atakiri mbele ya malaika wa Mungu kwamba mtu huyo ni wake.
9 Mais qui m’aura renié devant les hommes, sera renié devant les anges de Dieu.
Lakini, mtu yeyote anayenikana mbele ya watu, naye atakanwa mbele ya malaika wa Mungu.
10 Quiconque parle contre le Fils de l’homme, il lui sera remis; mais pour celui qui aura blasphémé contre l’Esprit-Saint, il ne lui sera pas remis.
“Yeyote anayesema neno la kumpinga Mwana wa Mtu atasamehewa; lakini anayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.
11 Lorsqu’on vous conduira dans les synagogues, devant les magistrats et les puissances, ne vous inquiétez point de quelle manière ou de ce que vous répondrez, ou bien de ce que vous direz.
“Watakapowapeleka ninyi mbele ya masunagogi na mbele ya wakuu na watawala msiwe na wasiwasi juu ya jinsi mtakavyojitetea au jinsi mtakavyosema.
12 Car l’Esprit-Saint vous enseignera à l’heure même ce qu’il vous faudra dire.
Kwa maana wakati huo Roho Mtakatifu atawafundisheni kile mnachopaswa kusema.”
13 Alors quelqu’un de la foule lui dit: Maître, dites à mon frère de partager avec moi notre héritage.
Mtu mmoja katika ule umati wa watu akamwambia, “Mwalimu, mwambie ndugu yangu tugawane urithi aliotuachia baba.”
14 Mais Jésus lui répondit: Homme, qui m’a établi juge sur vous, ou pour faire vos partages?
Yesu akamjibu, “Rafiki, ni nani aliyeniweka mimi mwamuzi au msuluhishi kati yenu?”
15 Puis il leur dit: Voyez, et gardez-vous de toute avarice; car dans l’abondance même la vie de chacun ne dépend point des choses qu’il possède.
Basi, akawaambia wote, “Jihadharini na kila aina ya tamaa; maana uzima wa mtu hautegemei wingi wa vitu alivyo navyo.”
16 Il leur dit ensuite cette parabole: il y avait un homme riche dont le champ rapportait beaucoup de fruits;
Kisha akawaambia mfano: “Kulikuwa na tajiri mmoja ambaye shamba lake lilizaa mavuno mengi.
17 Or il pensait en lui-même, disant: Que ferai-je, car je n’ai point où serrer mes fruits?
Tajiri huyo akafikiri moyoni mwake: Nitafanyaje nami sina mahali pa kuhifadhia mavuno yangu?
18 Et il dit: Voici ce que je ferai: je détruirai mes greniers, et j’en ferai de plus grands, et j’y rassemblerai tous mes produits et tous mes biens.
Nitafanya hivi: nitabomoa ghala zangu na kujenga kubwa zaidi, na humo nitahifadhi mavuno yangu yote na mali yangu.
19 Et je dirai à mon âme: Mon âme, tu as beaucoup de biens en réserve pour plusieurs années; repose-toi, mange, bois, fais grande chère.
Hapo nitaweza kuiambia roho yangu: sasa unayo akiba ya matumizi kwa miaka na miaka. Ponda mali, ule, unywe na kufurahi.
20 Mais Dieu lui dit: Insensé, cette nuit même on te redemandera ton âme; et ce que tu as amassé, à qui sera-t-il?
Lakini Mungu akamwambia: Mpumbavu wewe; leo usiku roho yako itachukuliwa. Na vitu vile vyote ulivyojilundikia vitakuwa vya nani?”
21 Ainsi est celui qui thésaurise pour lui, et qui n’est point riche devant Dieu.
Yesu akamaliza kwa kusema “Ndivyo ilivyo kwa mtu anayejilundikia mali kwa ajili yake mwenyewe, lakini si tajiri mbele ya Mungu.”
22 Et il dit à ses disciples: C’est pourquoi je vous dis: Ne vous inquiétez point pour votre vie, de ce que vous mangerez; ni pour votre corps, de quoi vous le vêtirez.
Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kwa sababu hiyo nawaambieni, msiwe na wasiwasi juu ya chakula mnachohitaji ili kuishi, wala juu ya mavazi mnayohitaji kwa ajili ya miili yenu.
23 La vie est plus que la nourriture, et le corps plus que le vêtement.
Kwa sababu uzima ni bora kuliko chakula, na mwili ni bora kuliko mavazi.
24 Considérez les corbeaux, ils ne sèment ni ne moissonnent, ils n’ont ni cellier ni grenier, et Dieu les nourrit. Combien ne valez-vous pas plus qu’eux?
Chukueni kwa mfano, kunguru: hawapandi, hawavuni wala hawana ghala yoyote. Hata hivyo, Mungu huwalisha. Ninyi mna thamani zaidi kuliko ndege!
25 Qui de vous, en s’inquiétant ainsi, peut ajouter à sa taille une seule coudée?
Ni nani kati yenu kwa kuwa na wasiwasi anaweza kuongeza urefu wa maisha yake?
26 Si donc vous ne pouvez même pas les moindres choses, pourquoi vous inquiéter des autres?
Basi, kama hamwezi kufanya jambo dogo kama hilo, kwa nini kuwa na wasiwasi juu ya yale mengine?
27 Considérez les lis comme ils croissent; ils ne travaillent ni ne filent: et cependant je vous le dis, Salomon lui-même, dans toute sa gloire, n’était pas vêtu comme l’un d’eux.
Angalieni maua jinsi yanavyomea. Hayafanyi kazi wala hayafumi. Hata hivyo, nawahakikishieni kwamba hata Solomoni mwenyewe na fahari zake zote hakupata kuvikwa vizuri kama ua mojawapo.
28 Or si l’herbe qui est aujourd’hui dans les champs, et qui demain sera jetée au four, Dieu la revêt ainsi, combien plus le fera-t-il pour vous, hommes de peu de foi?
Lakini, kama Mungu hulivika vizuri jani la shambani ambalo leo liko na kesho latupwa motoni, je, hatawafanyia ninyi zaidi? Enyi watu wenye imani haba!
29 Ne demandez donc point ce que vous aurez à manger ou à boire, et ne vous élevez pas si haut;
“Basi, msivurugike akili, mkihangaika daima juu ya mtakachokula au mtakachokunywa.
30 Car ce sont ces choses que les nations du monde recherchent; mais votre Père sait que vous en avez besoin.
Kwa maana hayo yote ndiyo yanayohangaikiwa na watu wasiomjua Mungu. Baba yenu anajua kwamba mnahitaji vitu hivyo.
31 Ainsi cherchez premièrement le royaume de Dieu et sa justice; et toutes ces choses vous seront données par surcroît.
Shughulikieni kwanza Ufalme wa Mungu, na hayo yote mtapewa kwa ziada.
32 Ne craignez point, petit troupeau, parce qu’il a plu à votre Père de vous donner son royaume.
“Msiogope, enyi kundi dogo! Maana Baba yenu amependa kuwapeni Ufalme.
33 Vendez ce que vous avez et donnez l’aumône. Faites-vous des bourses que le temps n’use point, un trésor qui ne vous fasse pas défaut dans les cieux, où le voleur n’approche point, et où les vers ne rongent point.
Uzeni mali yenu mkawape maskini misaada. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, na jiwekeeni hazina mbinguni ambako haitapungua. Huko wezi hawakaribii, wala nondo hawaharibu.
34 Car où est votre trésor, là sera aussi votre cœur.
Pale ilipo hazina yako, ndipo pia utakapokuwa moyo wako.
35 Ceignez vos reins, et ayez en vos mains les lampes allumées;
“Muwe tayari! Jifungeni mkanda kiunoni, na taa zenu ziwe zinawaka;
36 Semblables à des hommes qui attendent que leur maître revienne des noces; afin que lorsqu’il viendra et frappera à la porte, ils lui ouvrent aussitôt.
muwe kama watumishi wanaomngojea bwana wao arudi kutoka arusini, ili wamfungulie mara atakapobisha hodi.
37 Heureux ces serviteurs, que le maître, quand il viendra, trouvera veillant! En vérité, je vous le dis, il se ceindra, et les fera mettre à table, et passant de l’un à l’autre, il les servira.
Heri yao watumishi wale ambao bwana wao atakaporudi atawakuta wanakesha! Nawaambieni hakika, huyo bwana atajifunga mkanda kiunoni, atawaketisha mezani na kuwahudumia.
38 Et s’il vient à la seconde veille, et s’il vient à la troisième veille, et qu’il les trouve ainsi, heureux sont ces serviteurs.
Heri yao watumishi hao ikiwa bwana wao atawakuta wanakesha hata ikiwa atarudi usiku wa manane au alfajiri.
39 Car sachez bien que si le père de famille savait à quelle heure le voleur doit venir, il veillerait et ne laisserait point percer sa maison.
Jueni kwamba, kama mwenye nyumba angejua saa ambayo mwizi atakuja, angekesha, wala hangeiacha nyumba yake ivunjwe.
40 Et vous aussi, tenez-vous prêts; parce qu’à l’heure que vous ne pensez pas, le Fils de l’homme viendra.
Nanyi, kadhalika muwe tayari, maana Mwana wa Mtu atakuja saa msiyoitazamia.”
41 Or Pierre lui dit: Seigneur, est-ce pour nous que vous dites cette parabole, ou pour tout le monde?
Petro akamwambia, “Bwana, mfano huo ni kwa ajili yetu tu, au ni kwa ajili ya watu wote?”
42 Et le Seigneur dit: Qui, pensez-vous, est le dispensateur fidèle et prudent que le maître a établi sur tous ses serviteurs pour leur distribuer, dans le temps, leur mesure de froment?
Bwana akajibu, “Ni nani basi, mtumishi aliye mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana wake atamweka juu ya watumishi wake ili awape chakula wakati ufaao?
43 Heureux ce serviteur que le maître, lorsqu’il viendra, trouvera agissant ainsi!
Heri yake mtumishi huyo ikiwa bwana wake atakaporudi atamkuta akifanya hivyo.
44 Je vous dis, en vérité, qu’il l’établira sur tous les biens qu’il possède.
Hakika atampa madaraka juu ya mali yake yote.
45 Que si ce serviteur dit en son cœur: Mon maître tarde à venir; et qu’il commence à battre les serviteurs et les servantes, à manger, à boire et à s’enivrer;
Lakini, kama mtumishi huyo atafikiri moyoni mwake: na kusema: Bwana wangu amekawia sana kurudi halafu aanze kuwapiga watumishi wenzake, wa kiume au wa kike, na kula, kunywa na kulewa,
46 Le maître de ce serviteur viendra le jour où il ne s’y attend pas, et à l’heure qu’il ne sait pas, et il le divisera, et il lui donnera ainsi sa part avec les infidèles.
bwana wake atarudi siku asiyoitazamia na saa asiyoijua; atamkatilia mbali na kumweka fungu moja na wasioamini.
47 Mais ce serviteur, qui a connu la volonté de son maître, et ne s’est pas tenu prêt, et de cette manière n’a pas agi selon sa volonté, recevra un grand nombre de coups;
Mtumishi ambaye anajua matakwa ya bwana wake lakini hajiweki tayari kufanya anavyotakiwa, atapigwa sana.
48 Celui qui ne l’a pas connue, et qui a fait des choses dignes de châtiment, recevra peu de coups. Car à celui à qui on a donné beaucoup, on demandera beaucoup; et de celui à qui on a confié beaucoup, on exigera davantage.
Lakini yule afanyaye yanayostahili adhabu bila kujua, atapigwa kidogo. Aliyepewa vingi atatakiwa vingi; aliyekabidhiwa vingi zaidi atatakiwa kutoa vingi zaidi.
49 Je suis venu jeter un feu sur la terre; et que veux-je, sinon qu’il s’allume?
“Nimekuja kuwasha moto duniani, laiti ungekuwa umewaka tayari!
50 Je dois être baptisé d’un baptême; or combien je me sens pressé jusqu’à ce qu’il s’accomplisse?
Ninao ubatizo ambao inanipasa niupokee; jinsi gani ninavyohangaika mpaka ukamilike!
51 Pensez-vous que je sois venu apporter la paix sur la terre? Non, je vous le dis; mais la division.
Mnadhani nimekuja kuleta amani duniani? Hata kidogo; si amani bali utengano.
52 Car, désormais, dans une seule maison, cinq seront divisés, trois contre deux, et deux contre trois;
Na tangu sasa, jamaa ya watu watano itagawanyika; watatu dhidi ya wawili, na wawili dhidi ya watatu.
53 Seront divisés: le père contre le fils, et le fils contre le père; la mère contre la fille, et la fille contre la mère; la belle-mère contre sa belle-fille, et la belle-fille contre sa belle-mère.
Baba atakuwa dhidi ya mwanawe, mwana dhidi ya baba yake; mama dhidi ya bintiye, binti dhidi ya mama yake; mama mkwe dhidi ya mke wa mwanawe na huyo dhidi ya mama mkwe wake.”
54 Il disait aussi au peuple: Lorsque vous voyez un nuage se former au couchant, aussitôt vous dites: La pluie vient, et il arrive ainsi.
Yesu akayaambia tena makundi ya watu, “Mnapoona mawingu yakitokea upande wa magharibi, mara mwasema: Mvua itanyesha, na kweli hunyesha.
55 Et quand vous voyez souffler le vent du midi, vous dites: Il fera chaud, et cela arrive.
Mnapoona upepo wa kusi unavuma, mwasema Kutakuwa na hali ya joto na ndivyo inavyokuwa.
56 Hypocrites, vous savez juger d’après l’aspect du ciel et de la terre; mais ce temps-ci, comment ne le reconnaissez-vous point?
Enyi wanafiki! Mnajua kutabiri hali ya hewa kwa kuangalia dunia na anga; kwa nini basi, hamwezi kujua maana ya nyakati hizi?
57 Comment ne discernez-vous pas de vous-mêmes ce qui est juste?
“Na kwa nini hamwezi kujiamulia wenyewe jambo jema la kufanya?
58 Lorsque tu vas avec ton adversaire devant un magistrat, tâche de te dégager de lui en chemin, de peur qu’il ne te traîne devant le juge et que le juge ne te livre à l’exécuteur, et que l’exécuteur ne te jette en prison.
Maana kama mshtaki wako anakupeleka mahakamani, ingekuwa afadhali kwako kupatana naye mkiwa bado njiani, ili asije akakupeleka mbele ya hakimu, naye hakimu akakutoa kwa polisi, nao wakakutia ndani.
59 Je te le dis, tu n’en sortiras point que tu n’aies payé jusqu’à la dernière obole.
Hakika hutatoka huko nakwambia, mpaka utakapomaliza kulipa senti ya mwisho.”

< Luc 12 >