< Lévitique 7 >

1 Voici aussi la loi de l’hostie pour le délit, elle est très sainte:
Hii ndiyo sheria ya sadaka ya hatia. Kwa sababu hiyo ni sadaka takatifu sana.
2 C’est pourquoi là où sera immolé l’holocauste, sera aussi tuée la victime pour le délit; son sang sera répandu autour de l’autel.
Ni lazima waichinje sadaka ya hatia mahali panapostali kuchinjwa, na ni lazima watainyunyiza damu yake pande zote za madhabahu.
3 On en offrira la queue et la graisse qui couvre les entrailles:
Mafuta yote yaliyomo ndani yake yataondolewa: mafuta ya mkiani, mafuta yaliyo sehamu za ndani,
4 Les deux reins, la graisse qui est près des flancs et la membrane réticulaire du foie avec les reins;
zile figo mbili pamoja na mafuta yaliyo juu yake, yaliyo karibu na kiuno, na yanayofunika ini—nyama hii yote lazima iondolewe pamoja na hizo figo.
5 Et le prêtre les brûlera sur l’autel: c’est l’holocauste du Seigneur pour le délit.
Kuhani ataviteketeza vipande hivi juu ya madhabahu viwe dhabihu iliyofanywa kwa Yahweh kwa moto. Hii ni sadaka ya hatia
6 Tout mâle de la race sacerdotale mangera de ces chairs dans un lieu saint, parce que c’est une chose très sainte.
Kila mwanaume miongoni mwa familia ya kuhani anaweza kula sehemu ya sadaka hii. Lakini ni lazima iliwe ndani ya mahali patakatifu kwa sababu ni takatifu sana.
7 Comme pour le péché est offerte l’hostie, de même aussi l’hostie pour le délit: une seule loi sera pour les deux hosties: c’est au prêtre qui les a offertes qu’elles appartiendront.
Nayo sadaka ya dhambi ni kama ilivyo sadaka ya hatia. Ni sheria ileile hutumika kwa zote mbili. Zote ni mali ya kuhani azitumiaye kufanya upatanisho.
8 Le prêtre qui offre la victime de l’holocauste, en aura la peau.
Kuhani atoaye sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya mtu yeyote anaweza kuchuku ngozi ya sadaka hiyo kwa ajili yake mwenyewe.
9 Et toute offrande de fleur de farine qui se cuit dans le four ou qui s’apprête sur un gril ou dans la poêle, sera au prêtre par lequel elle est offerte:
Kila sadaka ya nafaka inayookwa mekoni, na kila sadaka kama hiyo ipikwayo kaangoni au kwenye sufuria itakuwa ya kuhani aitoaye.
10 Qu’elle soit arrosée d’huile ou qu’elle soit sèche, elle sera partagée entre tous les fils d’Aaron en une égale mesure.
Kila sadaka ya nafaka, ama iwe unga mkavu au uliochanganywa na mafuta ya zeitu itakuwa ya ukoo wa Aroni kwa usawa.
11 Voici la loi de l’hostie des sacrifices pacifiques qui est offerte au Seigneur.
Hii ndiyo sheria ya dhabihu ya sadaka za amani, ambazo watu watazitoa kwa Yahweh.
12 Si c’est une oblation pour action de grâces, on offrira des pains sans levain, arrosés d’huile, des beignets azymes, oints d’huile, de la fleur de farine cuite, des galettes mêlées et arrosées d’huile;
Iwapo mtu yeyote anaitoa ili kuonyesha shukrani kwa Yahweh, basi ataitoa pamoja na dhabih uya mikate iliyotengenezwa bila hamira, bali kwa mafuta ya zeituni yaliyochanganywa na unga lakini bila hamira, na maandazi yaliyotengenezwa bila hamira, bali yaliyopakwa mafuta juu yake, na mikate miembamba iliyofanywa kwa unga laini uliochanganywa na mafuta.
13 Et aussi des pains fermentés, avec l’hostie d’action de grâces, qui est immolée pour les sacrifices pacifiques.
Kwa kusudi la kutoa shukrani, pia anapaswa kutoa pamoja na sadaka yake ya amani, vipande vya mikate iliyotiwa hamira.
14 Un de ces pains sera offert pour prémices au Seigneur, et il sera au prêtre qui répandra le sang de l’hostie,
Ni lazima atatoa moja kila aina ya sadaka hizi kama sadaka iliyoletwa kwa Yahweh. Nayo itakuwa ya makuhani wanaonyunyizia damu ya sadaka ya amani kwenye madhabahu.
15 Dont la chair sera mangée le même jour, et il n’en restera rien jusqu’au matin.
Mtu anayeleta sadaka ya amani kwa kusudi la kutoa shukrani ni lazima ataila nyama ya sadaka yake siku ya kutoa dhabihu. Hatakiwi kusaza chochote kilicho cha sadaka hiyo hata asubuhi ya pili.
16 Si quelqu’un par vœu ou spontanément offre une hostie, elle sera également mangée le même jour, et si quelque chose en reste pour le lendemain, il sera permis d’en manger;
Lakini iwapo dhabihu ya matoleo yake kusudi lake ni nadhiri, au kwa kusudi la sadaka ya hiari, nyama yake italiwa siku iyo hiyo aitoapo dhabihu yake, lakini chochote kinachosalia cha sadaka hiyo kinaweza kuliwa siku inayofuata.
17 Mais tout ce que le troisième jour en trouvera, le feu le consumera.
Hata hivyo, nyama yoyote ya dhabihu inayobaki siku ya tatu ni lazima ichomwe moto.
18 Si quelqu’un mange le troisième jour de la chair de la victime des sacrifices pacifiques, l’oblation deviendra nulle, et elle ne sera pas utile à celui qui l’aura offerte; bien plus, quiconque se sera souillé par un tel aliment, sera coupable de prévarication.
Iwapo kipande chochote cha nyama hiyo ya dhabihu kinachobaki kinaliwa katika siku ya tatu, hakitakubalika, wala hakitatolewa kwa aliyeitoa. Kitakuwa ni kitu cha kuchukiza, na mtu akilaye atabeba hatia ya dhambi mwenyewe yake.
19 La chair qui aura touché quelque chose d’impur, ne sera point mangée, mais elle sera brûlée au feu; celui qui sera pur mangera de la victime des sacrifices pacifiques.
Nyama yoyote inayogusa kitu kilicho najisi haitaliwa. Ni lazima ichomwe moto. Na kwa ajili ya nyama inayobaki, yeyote aliye safi anaweza kuila.
20 L’homme souillé qui mangera de la chair de l’hostie des sacrifices pacifiques, laquelle aura été offerte au Seigneur, périra du milieu de ses peuples.
Hata hivyo, mtu najisi anayekula nyama kutoka kwenye dhabihu ya matoleo ya amani ambayo ni ya Yahweh yapasa mtu huyu akatiliwe mbali kutoka kwa watu wake.
21 Et celui qui aura touché quelque chose d’impur d’un homme, ou d’une bête, ou bien de toute chose qui peut souiller, et qui mangera de la chair de cette sorte, périra du milieu de ses peuples.
Iwapo mtu yeyote anagusa kitu chochote kilichonajisi—iwe ni unajisi wa binadamu, au wa mnyama aliyenajisi, au wa kitu fulani kilichonajisi na chenye kuchukiza, na kisha akala baadhi ya nyama ya dhabihu ya sadaka ya amani iliyotolewa kwa Yahweh, lazima mtu huyo akatiliwe mbali kutoka kwa watu wake.
22 Le Seigneur parla encore à Moïse, disant:
Kisha Yahweh akazungumza na Musa, akisema,
23 Dis aux enfants d’Israël: Vous ne mangerez point de la graisse de brebis, de bœuf et de chèvre.
“Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, 'hamruhusiwi kula mafuta ya fahali au kondoo au mbuzi.
24 Quant à la graisse d’un animal crevé, et de celui qui a été pris par une bête sauvage, vous l’emploierez à divers usages.
Mafuta ya mnyama yoyote afaye peke yake bila ya kuwa dhabihu, au mafuta ya mnyama yeyote aliyeraruliwa na wanyama pori, yanaweza kutumika kwa makusudi mengine, lakini hakika hamtayala.
25 Si quelqu’un mange de la graisse qui doit être consumée par le feu comme une oblation au Seigneur, il périra du milieu de son peuple.
Yeyote atakayekula mafuta ya mnyama ambayo watu wanaweza kuyatoa kuwa dhabihu ya iliyofanywa kwa Yahweh kwa moto, mtu huyo lazima atakatiliwa mbali kutoka kwa watu wake.
26 Vous ne prendrez pas non plus pour nourriture du sang d’aucun animal, tant des oiseaux que des troupeaux.
Hamtakula damu yoyote katika mojawapo ya nyumba zenu, ama iwe kutoka kwa ndege au mnyama.
27 Tout homme qui aura mangé du sang, périra du milieu de ses peuples.
Yeyote alaye damu yoyote, mtu huyo lazima akatiliwe mbali kutoka kwa watu wake.'”
28 Le Seigneur parla encore à Moïse, disant:
Kwa hiyo Yahweh akazungumza na Musa na akasema,
29 Parle aux enfants d’Israël, disant: Que celui qui offre la victime des sacrifices pacifiques au Seigneur, lui offre aussi en même temps son sacrifice, c’est-à-dire, ses libations.
“Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, 'Yeye atoaye dhabidhu ya sadaka ya amani kwa Yahweh lazima alete sehemu ya dhabihu yake kwa Yahweh.
30 Il tiendra dans ses mains la graisse de l’hostie et la poitrine; et lorsqu’en les offrant l’une et l’autre au Seigneur, il les aura consacrées, il les remettra au prêtre,
Mikono yake mwenyewe lazima iilete hiyo sadaka ifanywayo kwa Yahweh kwa moto. Naye atayaleta hayo mafuta pamoja na kidari, ili kwamba kidari kiweze kutikiswa kuwa sadaka ya kutikiswa mbele za Yahweh.
31 Qui brûlera la graisse sur l’autel; mais la poitrine sera pour Aaron et pour ses fils.
Kuhani atayachoma mafuta hayo juu ya madhabahu, lakini kile kidari kitakuwa mali ya Aroni na uzao wake.
32 L’épaule droite des hosties des sacrifices pacifiques deviendra les prémices du prêtre.
Ni lazima utatoa paja la kulia kwa kuhani kama sadaka iliyotokana na dhabihu ya sadaka yako ya amani.
33 Celui des fils d’Aaron qui aura offert le sang et la graisse, celui-là même aura aussi l’épaule droite pour sa portion.
Yule kuhani, mmoja wa wazao wa Aroni, atoaye damu na mafuta ya sadaka ya amani—ni lazima atapata paja la kulia kama mgao wake wa sadaka.
34 Car la poitrine de l’élévation et l’épaule de la séparation, je les ai prises aux enfants d’Israël sur leurs hosties pacifiques, et je les ai données à Aaron, le prêtre, et à ses fils, par une loi perpétuelle pour tout le peuple d’Israël.
Kwa kuwa nimetwaa kidari, na paja la sadaka ya kutikiswa kutoka kwa watu wa Israeli uwe mchango wao, na amepewa Aroni kuhani na wanawe kuwa mgao wao wa kawaida.
35 C’est là l’onction d’Aaron et de ses fils dans les cérémonies du Seigneur, au jour que Moïse les présenta pour exercer les fonctions du sacerdoce;
Huu ndiyo mgao wa Aroni na uzao wake utokanao na matoleo yaliyofanywa kwa Yahweh kwa moto, siku ile Musa alipowaweka wakfu ili kumtumikia Yahweh katika kazi ya kuhani.
36 Et c’est ce que le Seigneur a commandé de donner aux enfants d’Israël, comme culte perpétuel dans leurs générations.
Huu ndio mgao ambao Yahweh aliamru waweze kupewa kutoka kwa watu wa Israeli, katika siku hiyo aliyowatia mafuta ya upako wawe makuhani. Nao utakuwa mgao wao wa kila siku katika vizazi vyote.
37 Telle est la loi de l’holocauste et du sacrifice pour le péché et pour le délit, et pour la consécration et les victimes des sacrifices pacifiques;
Hii ndiyo sheria ya sadaka ya kuteketezwa, ya sadaka ya nafaka, ya sadaka ya dhambi, ya sadaka ya hatia, ya sadaka ya kuweka wakfu, na ya dhabihu, ya sadaka za amani,
38 Loi que le Seigneur donna à Moïse sur la montagne de Sinaï, quand il commanda aux enfants d’Israël d’offrir leurs oblations au Seigneur dans le désert de Sinaï,
ni sheria ambazo Yahweh alizitoa kwa Musa kwenye Mlima Sinai siku aliyowaamru watu wa Israeli kutoa dhabihu zao kwa Yahweh katika jangwa la Sinai.'”

< Lévitique 7 >