< Lévitique 15 >

1 Le Seigneur parla encore à Moïse et à Aaron, disant:
Yahwe alizungumza na Musa na Haruni, akisema,
2 Parlez aux enfants d’Israël et dites-leur: Un homme qui a la gonorrhée sera impur.
“Waambie watu wa Israeli, na sema kwao, 'Wakati mtu yeyote kisonono kimemwathiri mwili wake unatoa ugiligili, anakuwa najisi.
3 Or, on jugera qu’il est atteint de cette maladie, lorsqu’à chaque moment s’attachera à sa chair et s’accroîtra une humeur sale.
Unajisi wake unatokana na athari ya kisonono. Iwe mwili wake unatoa ugiligili au umekoma, huo ni unajisi.”
4 Tout lit sur lequel il aura dormi, sera impur, et tout endroit où il se sera assis.
Kitanda chochote anachokilalia kitakuwa najisi, na kila kitu ambacho anakaa juu yake kitakuwa najisi.
5 Si quelque homme touche son lit, il lavera ses vêtements, et lui-même, s’étant lavé dans l’eau, sera impur jusqu’au soir.
Yeyote anayegusa kitanda chake lazima afue nguo zake na aoge kwenye maji, na awe amenajisika mpaka jioni.
6 S’il s’assied où cet homme s’est assis, il lavera lui aussi ses vêtements; et s’étant lavé dans l’eau, il sera impur jusqu’au soir.
Yeyote anayekaa katika kitu chochote ambacho mtu ambaye ameathiriwa na kisonono alikaa, mtu huyo lazima afue nguo zake na aoge katika maji, na atakuwa najisi mpaka jioni.
7 Celui qui aura touché sa chair, lavera ses vêtements; et lui-même s’étant lavé dans l’eau, il sera impur jusqu’au soir.
Na yeyote anayegusa mwili wa ambaye ameathirika na kisonono lazima afue nguo zake na aoge katika maji, na awe najisi hadi jioni.
8 Si un homme, en cet état, jette de sa salive sur celui qui est pur, celui-ci lavera ses vêtements; et s’étant lavé dans l’eau, il sera impur jusqu’au soir.
Kama mtu ambaye anaona majimaji kama hayo kwa mtu fulani ambaye ametakasika, ndipo mtu huyo lazima afue nguo zake na aoge kwenye maji, na atakuwa najisi hata jioni.
9 Le bât sur lequel il se sera assis, sera impur;
Tandiko lolote ambalo ambaye anamajimaji ya kisonono atalikalia litakuwa najisi.
10 Et tout ce qui aura été sous celui qui a la gonorrhée sera souillé jusqu’au soir. Celui qui portera quelqu’une de ces choses, lavera ses vêtements; et lui-même, s’étant lavé dans l’eau, sera impur jusqu’au soir.
Yeyote anayegusa kitu chochote kilichokuwa chini ya mtu huyo atakuwa najisi mpaka jioni, na yeyote anayebeba vitu hivyo lazima afue nguo zake na aoge katika maji; atanajisika mpaka jioni.
11 Tout homme qu’aura touché celui qui est en cet état, avant d’avoir lavé ses mains, lavera ses vêtements; et s’étant lavé dans l’eau, il sera impur jusqu’au soir.
Ambaye anamajimaji kama hayo akimgusa kabla kwanza ya kuosha kwa maji safi mikono yake, mtu aliyeguswa lazima afue nguo zake na aoge katika maji, na atakuwa najisi mpaka jioni.
12 Un vase de terre qu’il aura touché, sera brisé; mais un vase de bois sera lavé dans l’eau;
Chungu chochote cha udongo ambacho ambaye anamajimaji kama hayo akigusa lazima kivunjwe, na kila chombo cha mti lazima kioshwe na maji safi.
13 Mais si celui qui endure une pareille maladie guérit, il comptera sept jours après sa purification, et, ses vêtements et tout son corps lavés dans des eaux vives, il sera pur.
Wakati mwenye kisonono anapotakaswa katika kisonono chake, ndipo lazima ahesabu kwaajili yake siku saba kwaajili ya kutakasika kwake; ndipo afue nguo na aoshe mwili wake kwenye maji yatiririkayo. Ndipo atakuwa safi.
14 Mais au huitième jour, il prendra deux tourterelles, ou deux petits de colombe, et il viendra en la présence du Seigneur à la porte du tabernacle de témoignage, et les donnera au prêtre,
Katika siku ya nane lazima achukue njiwa wawili au kinda mbili za njiwa na aje mbele za Yahwe pakuingilia kwenye hema ya mkutano; pale lazima atoe hao ndege kwa kuhani.
15 Qui en sacrifiera un pour le péché et l’autre en holocauste; et le prêtre priera pour lui devant le Seigneur, afin qu’il soit purifié de sa gonorrhée.
Lazima kuhani awatoe, moja kama sadaka ya dhambi na nyingine kama ya kuteketezwa, na kuhani lazima afanye upatanisho kwaajili yake mbele za Yahwe kwaajili ya kisonono chake.
16 Un homme qui a usé du mariage, lavera dans l’eau tout son corps, et il sera impur jusqu’au soir.
Kama mtu yeyote ametokwa na shahawa, ndipo lazima aoge mwili wake wote katika maji; atanajisika mpaka jioni.
17 Il lavera dans l’eau le vêtement et la peau qu’il avait sur lui, et elle sera impure jusqu’au soir.
Kila vazi au ngozi ambayo juu yake kuna shahawa lazama paoshwe kwa maji; itakuwa najisi mpaka jioni.
18 La femme dont il se sera approché sera lavée dans l’eau, et elle sera impure jusqu’au soir.
Na kama mwanamke na mwanaume watalala pamoja na kunakutokwa kwa shahawa kwenda kwa mwanamke, lazima wote wawili waoge katika maji; watakuwa najisi mpaka jioni.
19 Une femme, qui au retour du mois éprouve un écoulement de sang, sera séparée pendant sept jours.
Mwanamke anapokuwa kwenye hedhi, ataendelea kunajisika kwa siku saba, na yeyote anayemgusa atakuwa najisi mpaka jioni.
20 Quiconque la touchera sera impur jusqu’au soir;
Chochote anacholala juu yake wakati wa hedhi kitakuwa najisi; kila kitu ambacho anakalia kitakuwa pia najisi.
21 Et l’endroit dans lequel elle aura dormi, ou se sera assise dans les jours de sa séparation, sera souillé.
Yeyote anayegusa kitanda chake lazima afue nguo zake na aoge kwa maji; mtu huyo atakuwa najisi mpaka jioni.
22 Celui qui aura touché son lit, lavera ses vêtements; et lui-même, s’étant lavé dans l’eau, sera impur jusqu’au soir.
Yeyote anayegusa chochote ambacho amekikalia lazima afue nguo zake na aoge kwa maji; mtu huyo anakuwa najisi mpaka jioni.
23 Quiconque aura touché un meuble, quel qu’il soit, sur lequel elle se sera assise, lavera ses vêtements; et lui-même, s’étant lavé dans l’eau, il sera souillé jusqu’au soir.
Iwe juu ya kitanda au kitu chochote juu ya popote atakapokaa, kama akikigusa, mtu huyo atakuwa najisi mpaka jioni.
24 Si un homme s’approche d’elle dans le temps de ses mois, il sera impur pendant sept jours; et tout lit sur lequel il dormira sera souillé.
Kama mwanaume yeyote akilala naye, na unajisi wa mwanamke ukamgusa, atakuwa amenajisika siku saba. Kila kitanda ambacho anakilalia mwanaume huyo kitanajisika.
25 Une femme, qui éprouve pendant plusieurs jours une perte de sang, hors le temps menstruel, ou qui après le sang menstruel ne cesse pas d’avoir cette perte, tant qu’elle sera atteinte de cette maladie, sera impure, comme si elle était dans le temps menstruel.
Kama mwanamke ametokwa damu kwa siku nyingi ambayo siyo kipindi cha hedhi yake, au ikitoka zaidi ya kipindi chake cha hedhi, wakati wote wa siku za kunajisika, atakuwa kama alikuwa kwenye siku zake za hedhi. Yeye ni najisi.
26 Tout lit sur lequel elle aura dormi, et tout meuble sur lequel elle aura été assise, sera souillé.
Kila kitanda anachokilalia wakati wote wa kutokwa damu itakuwa kwake sawa tu kama kitanda anacholalia wakati wa hedhi, na kila kitu ambacho anakalia kitakuwa najisi, kama tu unajisi wa hedhi yake.
27 Quiconque aura touché ces choses, lavera ses vêtements; et lui-même, s’étant lavé dans l’eau, sera impur jusqu’au soir.
Na yeyote anayegusa kitu kati ya vitu hivyo atakuwa najisi; lazima yeye afue nguo zake na aoge mwenyewe kwenye maji, na atakuwa amenajisika mpaka jioni.
28 Si le sang s’arrête, et cesse découler, elle comptera sept jours jusqu’à sa purification;
Lakini kama mwanamke ametakasika katika kutokwa na damu, ndipo atahesabu kwaajili yake siku saba, baada ya hizo atakuwa safi.
29 Et au huitième jour, elle offrira pour elle au prêtre deux tourterelles ou deux petits de colombes à la porte du tabernacle de témoignage.
Katika siku ya nane atachukua kwake njiwa wawili au kinda wawili wa njiwa na atawaleta kwa kuhani pakuingilia hema ya mkutano.
30 Le prêtre en sacrifiera un pour le péché et l’autre en holocauste; et il priera pour elle devant le Seigneur, et pour la cause de son impureté.
Huyo kuhani atatoa ndege mmoja kama sadaka ya dhambi na mwingine kama sadaka ya kuteketezwa, na atafanya upatanisho kwaajili ya huyo mbele ya Yahwe kwaajili unajisi wa mwanamke atokwaye damu.
31 Vous instruirez donc les enfants d’Israël, afin qu’ils se gardent de l’impureté, et qu’ils ne meurent point dans leurs souillures, lorsqu’ils auront profané mon tabernacle, qui est au milieu de vous.
Hivi ndivyo lazima uwatenge watu wa Israeli katika unajisi wao, hivyo hawatakufa tokana na unajisi wao, kwa kuchafua hema langu, ambapo naishi kati yao.
32 Telle est la loi de celui qui a la gonorrhée, et qui se souille en usant du mariage,
Huu ndio utaratibu kwa kila ambaye anakisonono, kwaajili kila mwanaume ambaye shahawa yake inatoka na inamfanya kuwa najisi,
33 Et de celle qui est séparée à cause de ses mois, ou qui éprouve une perte de sang continuelle, et de l’homme qui aura dormi avec elle.
kwaajili ya mwanamke ambaye yuko katika kipindi cha hedhi, kwaajili ya yeyote aliye na kisonono, awe mwanaume au mwanamke, na kwaajili ya yeyote anayelala na mwanamke najisi.

< Lévitique 15 >