< Lévitique 1 >

1 Or le Seigneur appela Moïse, et il lui parla du tabernacle de témoignage, disant:
Bwana akamwita Mose na kusema naye kutoka kwenye Hema la Kukutania, akamwambia,
2 Tu parleras aux enfants d’Israël et tu leur diras: Un homme d’entre vous qui offrira au Seigneur une hostie de bêtes à quatre pieds, c’est-à-dire qui offrira des bœufs et des brebis comme victimes,
“Sema na Waisraeli na uwaambie, ‘Yeyote miongoni mwenu aletapo sadaka ya mnyama kwa Bwana, alete mnyama kama sadaka yake kutoka kundi lake la ngʼombe au la kondoo na mbuzi.
3 Si son oblation est un holocauste, et de gros bétail, c’est un mâle sans tâche qu’il offrira, à la porte du tabernacle de témoignage, pour fléchir le Seigneur;
“‘Kama sadaka hiyo ni ya kuteketezwa kutoka kwenye kundi la ngʼombe, atamtoa ngʼombe dume asiye na dosari. Ni lazima amlete kwenye ingilio la Hema la Kukutania ili aweze kukubalika kwa Bwana.
4 Et il mettra la main sur la tête de l’hostie qui sera acceptable, et servira à son expiation;
Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka ya kuteketezwa, nayo itakubaliwa kwa niaba yake ili kufanya upatanisho kwa ajili yake.
5 Puis il immolera le veau devant le Seigneur, et les fils d’Aaron, prêtres, en offriront le sang. le répandant autour de l’autel qui est devant la porte du tabernacle;
Atamchinja yule fahali mchanga mbele za Bwana, kisha wana wa Aroni walio makuhani wataleta damu na kuinyunyiza pande zote za madhabahu yaliyo penye ingilio la Hema la Kukutania.
6 Et, la peau de l’hostie enlevée, ils en couperont les membres par morceaux,
Ataichuna hiyo sadaka ya kuteketezwa na kuikata vipande vipande.
7 Ensuite ils mettront du feu sous l’autel, un tas de bois ayant été auparavant disposé;
Wana wa Aroni kuhani wataweka moto juu ya madhabahu na kupanga kuni juu ya huo moto.
8 Et arrangeant au-dessus les membres coupés, c’est-à-dire, la tête et tout ce qui tient au foie,
Kisha wana wa Aroni walio makuhani watapanga vile vipande vya nyama, pamoja na kichwa na mafuta ya huyo mnyama juu ya zile kuni zinazowaka juu ya madhabahu.
9 Les intestins et les pieds ayant été auparavant lavés dans l’eau; puis le prêtre les brûlera sur l’autel en holocauste et en suave odeur pour le Seigneur.
Ataziosha sehemu za ndani na miguu yake kwa maji, naye kuhani atavichoma vyote juu ya madhabahu. Hii ni sadaka ya kuteketezwa, sadaka iliyotolewa kwa moto, yenye harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
10 Que si l’oblation de bêtes à quatre pieds est un holocauste de brebis ou de chèvres, c’est un mâle sans tache qu’il offrira;
“‘Kama sadaka ni ya kuteketezwa kutoka kwenye kundi la kondoo au mbuzi, atamtoa mnyama dume asiye na dosari.
11 Et il l’immolera au côté de l’autel qui regarde l’aquilon, devant le Seigneur; pour son sang, les fils d’Aaron le répandront sur l’autel tout autour;
Atamchinjia upande wa kaskazini wa madhabahu mbele za Bwana, nao wana wa Aroni walio makuhani watanyunyizia damu yake pande zote za madhabahu.
12 Et ils couperont les membres, la tête et tout ce qui tient au foie, et ils les placeront sur le bois au-dessous duquel doit être mis le feu.
Atamkata vipande vipande, naye kuhani atavipanga, pamoja na kichwa na mafuta ya mnyama juu ya zile kuni zinazowaka juu ya madhabahu.
13 Mais les intestins et les pieds, ils les laveront dans l’eau. Et le prêtre brûlera toutes ces choses offertes sur l’autel, en holocauste et en odeur très suave pour le Seigneur.
Ataosha sehemu za ndani na miguu kwa maji, naye kuhani atavileta vyote na kuvichoma juu ya madhabahu. Hii ni sadaka ya kuteketezwa, sadaka iliyotolewa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
14 Mais si c’est en oiseaux que se fait l’oblation de l’holocauste au Seigneur: en tourterelles, et petits de colombe,
“‘Kama sadaka ya kuteketezwa inayotolewa kwa Bwana ni ndege, atamtoa hua au kinda la njiwa.
15 Le prêtre offrira la victime à l’autel, et lui tournant la tête en arrière sur le cou, et ouvrant une plaie, il fera couler le sang sur le bord de l’autel;
Kuhani atamleta kwenye madhabahu, naye atamvunja shingo na kumnyofoa kichwa na kumchoma juu ya madhabahu. Damu yake itachuruzishwa ubavuni mwa madhabahu.
16 Mais la vésicule du gosier et les plumes, il les jettera auprès de l’autel, du côté oriental, au lieu dans lequel les cendres ont coutume d’être répandues.
Ataondoa kifuko cha chakula pamoja na uchafu wake na kuvitupa upande wa mashariki wa madhabahu, mahali pale penye majivu.
17 Il lui rompra les ailes, et il ne la coupera, ni ne la divisera par le fer, mais il la brûlera sur l’autel, le feu ayant été mis sous le bois. C’est un holocauste et une oblation d’une très suave odeur pour le Seigneur.
Atampasua na kumweka wazi katika mabawa yake, lakini asimwachanishe kabisa, kisha kuhani ataichoma juu ya zile kuni zinazowaka juu ya madhabahu. Hii ni sadaka ya kuteketezwa, sadaka iliyotolewa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.

< Lévitique 1 >