< Josué 8 >
1 Or, le Seigneur dit à Josué: Ne crains pas et ne t’effraie pas: prends avec toi toute la multitude des combattants, et te levant, monte à la ville de Haï: Voilà que j’ai livré en ta main son roi et son peuple, sa ville et sa terre.
Yahweh akamwambia Yoshua, “Usiogope; usivunjike moyo. Chukua pamoja nawe watu wa vita. Pandeni kwenda Ai. Tazama nimemtia mkononi mwako mfalme wa Ai, watu wake, mji wake na nchi yake.
2 Et tu feras à la ville de Haï et à son roi, comme tu as fait à Jéricho et à son roi, mais le butin et tous les animaux, vous les prendrez pour vous: dresse une embuscade à la ville par derrière.
Mtafanya hivyo pia huko Ai na mfalme wake kama mlivyofanya kwa Yeriko na mfalme wake, isipokuwa mtachukua nyara na mifugo kwa ajili yenu. Pangeni mashambulizi ya uviziaji nyuma ya mji.”
3 Josué se leva donc et toute l’armée de combattants avec lui pour monter vers Haï, et il envoya la nuit trente mille hommes choisis des plus vaillants,
Basi Yoshua aliinuka na akawachukua kwenda Ai watu wote wa vita. Kisha Yoshua akachagua watu elfu thelathini - wenye nguvu na ujasiri - na aliwatuma waende wakati wa usiku.
4 Et il leur ordonna, disant: Dressez une embuscade derrière la ville, et ne vous éloignez pas trop; et vous serez tous prêts;
Aliwaamuru, “Tazama, mtalala katika hali ya mashambulizi ya uviziaji dhidi ya mji, kwa nyuma yake. Usiende mbali sana na mji, lakini ninyi nyote muwe tayari.
5 Pour moi et le reste de la multitude qui est avec moi, nous avancerons du côté opposé contre la ville. Et lorsqu’ils sortiront contre nous, comme déjà nous avons fait, nous fuirons, et nous tournerons le dos,
Mimi pamoja na watu wote walio pamoja nami tutaukaribia mji. Na wakati watakapokuja kutushambulia sisi, tutawakimbia kama tulivyofanya hapo mwanzo.
6 Jusqu’à ce que, nous poursuivant, ils soient entraînés plus loin hors de la ville; car ils croiront que nous fuyons comme auparavant.
Watatoka nje watukimbize mpaka hapo tutakapokuwa tumewavuta mbali sana na mji, watasema, “Wanatukimbia kama walivyofanya mara ya mwisho.' Hivyo tutawakimbia na kwenda mbali.
7 Ainsi, nous fuyant et eux nous poursuivant, vous vous lèverez de l’embuscade, et vous ravagerez la ville; et le Seigneur votre Dieu la livrera en vos mains.
Kisha mtapanda kutoka sehemu mliyojificha, na mtauteka mji. Yahweh Mungu wenu atawapa mkononi mwenu.
8 Et lorsque vous l’aurez prise, mettez-y le feu; et c’est ainsi que vous ferez toutes choses, comme j’ai commandé.
Tazama nimewaamuru, mtakapouteka mji, mtauchoma moto. Mtayafanya haya wakati mtakapotii agizo lililotolewa katika neno la Yahweh.”
9 Et Josué les envoya, et ils allèrent au lieu de l’embuscade, et se tinrent entre Béthel et Haï, au côté occidental de la ville de Haï; mais Josué, cette nuit-là, demeura au milieu du peuple;
Yoshua akawatuma, na wakaenda sehemu ya uviziajia, na wakajificha kati ya Betheli na Ai sehemu ya magharibi ya Ai. Yoshua akalala miongoni mwa watu usiku ule.
10 Et, se levant au point du jour, il fit la revue de ses gens, et il monta avec les anciens à la tête de l’armée, protégé par le secours des combattants.
Yoshua aliamka asubuhi na mapema na akawaandaa tayari wanajeshi wake, Yoshua na wazee wa Israeli walishambuliwa watu wa Ai.
11 Et, lorsqu’ils furent arrivés, et qu’ils eurent monté du côté opposé de la ville, ils s’arrêtèrent au côté septentrional de la ville, entre laquelle et eux était la vallée.
Watu wote wa vita waliokuwa pamoja naye walipanda na kuukaribia mji. Walisogea karibu na mji na wakapiga kambi sehemu ya kasikazini mwa Ai. Kulikuwa na bonde kati yao na Ai.
12 Mais il avait choisi cinq mille hommes et les avait placés en embuscade entre Béthel et Haï, à la partie occidentale de la même ville.
Alichukua watu wapatao elfu tano hivi na akawaweka katika hali ya kuvizia katika upande wa magharibi mwa mji kati ya Betheli na Ai.
13 Quant à tout le reste de l’armée, il se dirigeait en bataille rangée vers l’aquilon, en sorte que les derniers de cette multitude atteignaient au côté occidental de la ville. Josué partit donc cette nuit là, et s’arrêta au milieu de la vallée.
Waliwapanga wanajeshi wote, jeshi kuu katika upande wa kasikazini mwa mji, na walinzi wa nyuma upande wa magharibi mwa mji. Yoshua alilala bondeni usiku ule.
14 Ce qu’ayant vu le roi de Haï, il se hâta dès le matin, et sortit avec toutes les troupes de la ville, et dirigea l’armée vers le désert, ignorant que derrière il y avait une embuscade.
Na ilikuwa alipoona hilo mfalme wa Ai, yeye pamoja na jeshi lake, waliamka asubuhi na mapema na walitoka kwa haraka kwenda kuwashambulia Israeli katika eneo linalokabili bonde la Mto Yordani. Hakujua kuwa kulikuwa na shambulizi la kuvizia lilikuwa linasubiria kushambulia kutokea kwa nyuma ya mji.
15 Or, Josué et tout Israël abandonnèrent ce lieu, et feignant la peur, ils s’enfuirent par la voie du désert.
Yoshua na Waisraeli wote walikubali wenyewe kushindwa mbele yenu, na wakakimbia kuelekea nyikani.
16 Mais ceux de Haï poussant tous ensemble de grands cris, et s’encourageant mutuellement les poursuivirent; et, comme ils se furent éloignés de la cité,
Watu wote waliokuwa kwenye mji waliitwa kwa pamoja waende mbele yao, na walienda mbele ya Yoshua na kwa jinsi hiyo walivutwa mbali na mji.
17 Et que pas même un seul ne resta dans la ville de Haï et de Béthel, afin de poursuivre Israël (comme ils étaient sortis précipitamment, laissant leurs villes ouvertes),
Hapakuwa na mtu mme aliyesalia Ai na Betheli ambaye alikuwa hajaenda nje kuwafuatilia waisraeli. Na walipokuwa wanawafuatilia Waisraeli, Wakatoka na waliuacha mji wazi.
18 Le Seigneur dit à Josué: Lève le bouclier qui est dans ta main contre la ville de Haï, parce que je te la livrerai.
Yahweh akamwambia Yoshua, “Nyosha mkuki huo ulio mkononi mwako kuelekea Ai, kwa kuwa nitaitia Ai mikononi mwako.” Yoshua akaunyosha mkuki uliokuwa mkononi mwake kuuelekea mji.
19 Et lorsqu’il eut levé le bouclier contre la ville, ceux qui étaient cachés en embuscade, se levèrent aussitôt, et marchant vers la ville, ils la prirent et y mirent le feu.
Wanajeshi waliojificha katika hali ya kuvizia walitoka upesi katika eneo lao mara tu alipounyosha mkono wake. Walikimbia mbio na kuuingia mji na kuuteka. Na kwa haraka wakauchoma moto mji.
20 Mais les hommes de la ville qui poursuivaient Josué, regardant et voyant que la fumée de la ville montait jusqu’au ciel, ne purent plus fuir ni d’un, côté, ni de l’autre, surtout lorsque ceux qui avaient feint une fuite et se dirigeaient vers le désert, résistèrent très fortement à ceux qui les poursuivaient.
Watu wa Ai waligeuka na kuangalia nyuma. Waliona moshi kutoka katika mji ukipanda kwenda angani, na hawakuweza kutoroka kwa njia hii au ile. Kwa kuwa wanajeshi wa Israelei waliokuwa wamekimbia katika nyika, sasa walirudi kuwakabili wale waliokuwa wanawafuatilia.
21 Alors Josué et tout Israël, voyant que la ville était prise, et que la fumée montait de la ville, se retournèrent et battirent les hommes de Haï,
Na wakati Yoshua na Israeli wote walipoona kuwa wale watu wa kuvizia wameuteka mji kwa ule moshi uliokuwa ukipanda, waligeuka nyuma na kuwaua watu wa Ai.
22 Attendu que ceux-mêmes qui avaient pris et brûlé la cité, étant sortis de la ville au-devant des leurs, commencèrent à frapper les ennemis au milieu d’eux. Comme donc des deux côtés les ennemis étaient taillés en pièces, de manière que pas un seul d’une si grande multitude ne fut sauvé,
Na wanajeshi wengine wa Israeli, wale waliokuwa wameingia ndani ya mji, walitoka nje ili kuwashambulia. Hivyo, watu wa Ai walikamatwa katikati ya majeshi ya Israeli, baadhi katika upande huu na wengine katika upande ule.
23 Ils prirent aussi vivant le roi de la ville de Haï, et le présentèrent à Josué.
Lakini walimhifadhi mfalme wa Ai, ambaye walimteka akiwa hai, na kisha wakamleta kwa Yoshua.
24 Ainsi, tous ceux qui avaient poursuivi Israël se dirigeant vers le désert, ayant été tués, et étant tombés sous le glaive dans le même lieu, les enfants d’Israël revinrent et ravagèrent la ville.
Ilikuwa baada ya Israeli walipokuwa wamemaliza kuuwaua wenyeji wote wa Ai katika uwanda kariibu na nyika mahali walipowafuata, na baada ya wao wote, hata yule wa mwisho, walipokuwa wamekwisha kulala kwa ncha ya upanga, Waisraeli wote walirudi Ai. Waliuteka mji kwa ncha ya upanga.
25 Or, ceux qui, en ce même jour, succombèrent, depuis l’homme jusqu’à la femme, étaient au nombre de douze mille hommes, tous de la ville de Haï.
Wale wote walikufa siku hiyo walikuwa watu elfu kumi na mbili elfu, wanaume na wanawake, wote ni watu wa Ai.
26 Quant à Josué, tenant son bouclier, il ne baissa pas la main qu’il avait élevée, jusqu’à ce que tous les habitants de Haï fussent tués.
Yoshua hakuukunja mkono wake ambao alikuwa ameunyosha huku akishikilia mkuki wake, mpaka pale alipowateketeza kabisa watu wote wa Ai.
27 Et pour les bestiaux et le butin de la ville, les enfants d’Israël se les partagèrent, comme avait ordonné le Seigneur à Josué.
Waisraeli walichukua tu wanyama na nyara kutoka katika mji kwa ajili yao wenyewe, kama Yahweh alivyokuwa amemwagiza Yoshua.
28 Et Josué mit le feu à la ville et en fit un monceau de ruines éternel;
Yoshua aliichoma Ai na kuigeuza kuwa kichuguu cha mapango. Ni mahali palipoachwa ukiwa hata leo.
29 Il en suspendit aussi le roi à la potence jusqu’au soir et au coucher du soleil. Ensuite Josué ordonna, et on descendit son cadavre de la croix; on le jeta à l’entrée même de la ville, en élevant sur lui un monceau de pierres qui est demeuré jusqu’au présent jour.
Alimtundika mfalme wa Ai juu ya mti mpaka jioni. Na jua lilipokuwa linaenda kuzama, Yoshua aliwaagiza na wakautoa mwili wa mfalme wakaushusha chini ya mti na kuutupa mbele ya malango ya mji. Huko wakaweka kichuguu kikubwa cha mawe juu yake. Kichuguu hicho kimebaki huko hata leo.
30 Alors Josué bâtit un autel au Seigneur Dieu d’Israël sur le mont Hébal,
Kisha Yoshua akajenga madhabahu kwa Yahweh, Mungu wa Israeli katika Mlima wa Ebali,
31 Comme avait ordonné Moïse, serviteur du Seigneur, aux enfants d’Israël, et comme il est écrit dans le livre de la loi de Moïse: Un autel de pierres non polies que le fer n’a pas touchées; et il offrit dessus des holocaustes au Seigneur, et il immola des victimes pacifiques.
kama vile Musa mtumishi wa Yahweh alivyowaagiza watu wa Israeli, kama ilivyoandikwa katika kitabu cha sheria ya Musa: “Madhabahu ya mawe yasiyochongwa, ambayo juu yake hakuna mtu yeyote aliyetumia zana ya chuma.” Na allimtolea Yahweh sadaka ya kuteketezwa juu yake na wakatoa sadaka ya amani.
32 Et il écrivit sur les pierres le Deutéronome de la loi de Moïse, que celui-ci avait exposé devant les enfants d’Israël.
Na huko aliandika juu ya mawe nakala ya sheria za Musa mbele ya watu wa Israeli.
33 Or tout le peuple et les anciens, les chefs et les juges étaient debout des deux côtés de l’arche, en présence des prêtres qui portaient l’arche de l’alliance du Seigneur, l’étranger comme l’indigène. Une moitié était près du mont Garizim, et l’autre moitié près du mont Hébal, comme avait ordonné Moïse, serviteur du Seigneur. Et d’abord il bénit le peuple d’Israël.
Waisraeli wote, wazee wao, maafisa, na waamuzi wao walisimama katika sehemu mbili za sanduku mbele ya makuhani na Walawi ambao hulibeba sanduku la Agano la Yahweh - wageni pamoja na wazalia, nusu yao walisimama mbele ya Mlima Gerizimu na nusu walisimama mbele ya Mlima Ebali. Waliwabariki watu wa Israeli kama Musa mtumishi wa Yahweh alivyowaagiza hapo mwanzo.
34 Après cela il lut toutes les paroles de bénédiction et de malédiction, et tout ce qui était écrit dans le livre de la loi.
Baada ya hayo, Yoshua alisoma maneno yote ya sheria, baraka na laana, kama zilivyoandikwa katika kitabu cha sheria.
35 Il ne laissa rien, sans le rappeler, de tout ce que Moïse avait commandé; mais il retraça toutes choses devant toute la multitude d’Israël, les femmes, les petits enfants et les étrangers qui demeuraient parmi eux.
Halikusalia hata neno moja katika yote ambayo Musa alimwagiza Yoshua ambalo halikusomwa mbele ya kusanyiko la Waisraeli lilojumuisha wanawake, watoto wadogo na wageni walioishi miongoni mwao.