< Josué 3 >
1 Ainsi, Josué se levant de nuit, leva le camp; et sortant de Sétim ils vinrent au Jourdain, lui et tous les enfants d’Israël, et ils demeurèrent là trois jours.
Yoshua aliamka asubuhi na mapema, nao walisafiri kutoka Shitimu. Walifika Yordani, yeye na watu wote wa Israeli, na wakapiga kambi hapo kabla hawajavuka ng'ambo.
2 Et ces trois jours écoulés, les hérauts passèrent par le milieu du camp,
Baada ya siku tatu, maafisa walienda katika kambi, wakawaagiza watu,
3 Et, commencèrent à crier: Quand vous verrez l’arche de l’alliance du Seigneur votre Dieu et les prêtres de la race lévitique qui la portent, vous aussi, levez-vous, et marchez à leur suite;
“Mtakapoona sanduku la agano la Yahweh Mungu wenu, na makuhani kutoka miongoni mwa Walawi wamelibeba, ni lazima muondoke sehemu hii na kulifuata.
4 Et qu’il y ait entre vous et l’arche l’espace de deux mille coudées, afin que de loin vous puissiez voir et connaître par quelle voie vous devez aller, parce que vous n’avez pas encore passé par cette voie; et gardez-vous d’approcher de l’arche.
Lazima kuwe na umbali wa dhiraa elfu moja kati yenu na sanduku. Msilisogelee karibu, ili muweze kuiona njia ya kupitia, kwakuwa hamjawahi kupita njia hii kabla.
5 Josué dit aussi au peuple: Sanctifiez-vous; car demain le Seigneur fera parmi vous des merveilles.
Yoshua akawaambia watu, “Jitakaseni ninyi wenyewe keso, kwa kuwa Yahweh atafanya maajabu miongoni mwenu.”
6 Puis il dit aux prêtres: Portez l’arche du Seigneur, et précédez le peuple. Et ceux-ci accomplissant ces ordres, la portèrent, et marchèrent devant le peuple.
Kisha Yoshua akawaambia makuhani, “Chukueni sanduku la agano, na kulipitisha mbele za watu.” Hivyo, wakalichukua sanduku la agano na wakaenda mbele za watu.
7 Alors le Seigneur dit à Josué: Aujourd’hui je commencerai à t’exalter devant tout Israël, afin qu’ils sachent que, comme j’ai été avec Moïse, ainsi je suis avec toi aussi.
Yahweh akamwambia Yoshua, “Siku hii nitakufanya kuwa mtu mkubwa katika macho ya Waisraeli wote. Watajua kuwa kama nilivyokuwa na Musa ndivyo nitakavyokuwa pamoja na wewe.
8 Pour toi, commande aux prêtres qui portent l’arche de l’alliance, et dis-leur: Lorsque vous serez entrés dans une partie de l’eau du Jourdain, arrêtez-vous-là.
Utawaamuru makuhani ambao hulibeba sanduku la agano, 'Mtakapofika katika ukingo wa maji ya Yordani, ni lazima msimame katika Mto Yordani.'”
9 Et Josué dit aux enfants d’Israël: Approchez-vous ici, et écoutez la parole du Seigneur votre Dieu.
Kisha Yoshu akawaambia watu wa Israeli, “Njooni hapa na msikilize maneno ya Yahweh Mungu wenu.
10 Et de nouveau: En cela vous saurez que le Seigneur Dieu vivant est au milieu de vous, et qu’il détruira en votre présence le Chananéen, l’Hétéen, l’Hévéen, le Phérézéen, le Gergézéen, le Jébuséen et l’Amorrhéen.
Kwa hili mtajua kwamba Mungu aliye hai yuko miongoni mwenu na kwamba atawaondosha mbele yenu Wakanaani, Wahiti, Wahivi, Waperizi, Wagrigashi, Waamori na Wayebusi.
11 Voilà que l’arche de l’alliance du Seigneur de toute la terre marchera devant vous à travers le Jourdain.
Tazama! Sanduku la agano la Bwana wa nchi yote litavuka mbele yenu katika Yordani.
12 Préparez douze hommes des tribus d’Israël, un de chaque tribu.
Sasa chagueni wanaume kumi na wawili kutoka katika makabila ya Israeli, mmoja katika kila kabila.
13 Et lorsque les prêtres qui portent l’arche du Seigneur Dieu de toute la terre auront posé la plante de leurs pieds dans les eaux du Jourdain, les eaux d’en bas s’écouleront et se dissiperont, mais celles qui viennent d’en haut se condenseront en monceau.
Wakati nyayo za miguu ya makuhani walichukualo sanduku la Yahweh, Bwana wa nchi yote, zitakapogusa maji ya Yordani, maji ya Yordani yatatindika, na hata maji yatiririkayo kutoka juu yatakoma kutiririka nayo yatasimama kama chuguu.
14 Ainsi le peuple sortit de ses tabernacles pour passer le Jourdain; et les prêtres qui portaient l’arche de l’alliance marchaient devant lui.
Hivyo wakati watu walipotoka ili kuvuka Yordani, makuhani waliobeba sanduku la agano waende mbele ya watu.
15 Mais eux étant entrés dans le Jourdain, et leurs pieds commençant à être mouillés (car le Jourdain avait couvert ses rives au temps de la moisson),
Mara tu wale walichukuao sanduku wakiisha kufika Yordani, na miguu ya watu wale waliobeba sanduku itakapotiwa katika ukingo wa maji (maana sasa Yordani hujaa hadi katika kingo zake zote katika kipindi chote cha mavuno),
16 Les eaux qui descendaient s’arrêtèrent en un seul lieu, et, s’élevant comme une montagne, elles paraissaient de loin, depuis la ville qui est appelée Adom jusqu’au lieu nommé Sarthan; mais celles qui étaient au-dessous, descendirent dans la mer du désert (qui maintenant est appelée la mer Morte), jusqu’à ce qu’elles fussent entièrement écoulées.
maji yote yaliyotiririka kutoka juu yalisimama katika chuguu kimoja. Maji yakakoma kutiririka kutoka katika umbali mrefu. Maji yaliacha kutiririka kutoka Adam, mji ulio karibu na Zarethani, hadi bahari ya Negevu, Bahari ya Chumvi. Na watu walivuka ng'ambo karibu na Yeriko.
17 Or, le peuple marchait contre Jéricho, et les prêtres qui portaient l’arche de l’alliance du Seigneur se tenaient sur la terre sèche au milieu du Jourdain tout prêts; et tout le peuple passait à travers le lit desséché du fleuve.
Makuhani waliolibeba sanduku la agano la Yahweh walisimama katika nchi kavu katikati ya Yordani mpaka watu wote wa Israeli walipokwisha kuvuka katika nchi kavu.